Nataka kwenda kuchora Tatoo

Nataka kwenda kuchora Tatoo

Bongo hamna artist wa tatu, kama unabisha kachore ndo utajuta kuchafua ngozi yako na hicho utakachokichora hautatamani hata kukiangalia. Kuna jamaa mmoja yuko kenya na pia hua anakuja bongo kwa appointment ni artist mzuri na pia gharama zake ziko juu lakini akikuchora tatoo utatamani kila mtu aione. Good tattoo is not cheap, cheap tattoo is not good.

Sent using Jamii Forums mobile app
Acha kukariri wewe, kitu kama hukijui kaa kimya. Kama umezoea za elf 50 sijui laki, funga kopo lako. Kuna watu wapo hapa uswahilin, unachorwa kutokana na rangi yako na sehemu unayoitaka
 
Najua ni haramu lakini nahisi nataka hicho kitu,nataka kuweka alama ya ukumbusho wa jina la mtu muhimu sana kwangu!! Hivyo nimevutiwa kwenda kuchora sehemu ya mwili wangu (mkononi) kama ishara yeye kuishi daima mwilini mwangu.
Wazoefu naomba mnipe location ya fundi mzuri wa Tatoo na approximation ya gharama zake.

Sent using Jamii Forums mobile app
Wapo wachoraji wengi tu.kwani upo mkoa gani
 
Mwenyewe anajua ni haramu.hajaja kuomba kujua ni halal au haram.
Kauliza bei na mchoraji.naona mnamletea ngonjera nyiiingi

Sent using Jamii Forums mobile app
Mimi mwenyewe ndio nashangaa! Watu humu ndani wangeulizwa pombe wala wa kusema haram wasingepatikana,wameng'ang'ana wee kutoa ushauri kama vile wao ni malaika,hawana dhambi! Hawajawahi kutenda dhambi! Mtu ananishauri hivyo Mimi kua ni dhambi,ni haram huku yeye kalala na hawala sasa si ni sawa tu na mie nimelala na mume wa ndoa alafu nawaza Tatoo wakati yeye kalala na hawala anaiwaza haram yangu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Achana na hiyo mambo.

Watu wengi waliojichora, nimegundua wengi wanajuta na wanataka wazifute.

Ni mambo ya mpito tu.

Huyo Mtu muhimu kwako kama ni Mpenzi, nakushauri usipoteze muda wako.

Mapenzi yenyewe haya tuliyonayo kudumu ni ngumu sana
Usikariri kua kila binadamu ana matatizo na mapenzi,alafu nielewe vizuri kwenye Uzi wangu sikuomba ushauri,mengine niachie mwenyewe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chora tu dada, fanya kitu roho inapenda maisha mafupi haya. Hii miili ya dhambi haitaingia peponi kwani biblia inasema tutavikwa miili mipya.

Nina tattoo moja begani mwaka wa sita huu na sijawahi jutia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapa begani nimechora tatoo yenye maneno John 3:16 ambayo tafsiri yake haraka haraka ni Kwa maana Mungu aliupenda ulimwengu kiasi cha kumtoa Mwanae pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.. Alinichora jamaa mmoja anaitwa Pollo, nilimuita akanifata ninapoishi, saivi kawa staa kidogo sijui hata huduma yake ipoje, lkn ana ofisi Bamaga
Amina, ni maneno mazuri sana hayo na yana maana.

Mimi nikichora tattoo nitachora Msalaba mzuri sana.
 
Unaweza kusema vyovyote unavyojisikia,tukana vyovyote vile ila hainishtui hainisumbui kile naweza kukwambia sichori kwa ajili ya wengine

Sent using Jamii Forums mobile app
Kama watu wanaojielewa kama rubii wakiniruhusu nitakuonyesha ambavyo ulivyo mtu mzima ila akili zako aliyejuu ndiye anajua. Usisahau ulianza kuonyesha PM wewe na HR666 mlivyokuwa mnaombana, ukatueleza jinsi mume wako alivyotenguka kiuno, hukusita kutueleza unavyotaka kumfukuza mama mkwe ila ulinikosha ulivyosema wewe ni mtoto uliyezaliwa Tanga. Nakumbuka nilimuomba Sky Eclat asaidie wa kunyumba na nikamuomba pia mama wa shoka hapa JF NIMPENDENANI akusaidie. Mama hizi tatoo huwezi kuchora wakati una watoto (huo ni ulimbukeni na inaonyesha mumeo kiuno hakijapona unatafuta). Nitaendelea baada ya kukamua ng'ombe wa boss
 
Mwana kwetu vip ten usifurahishe nafsi yako ukasahau kumfurahisha Alosimamisha mbingu bila ya nguzo kama umeamua kumfurahisha huyo umpendae unaweza ukamfanyia chochote ambacho hatakisahau katk kumbukumbu zake tattoo ni haramu na ni dhambi pia ngoj niishie hapa.
Maashallah
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom