Masokotz
JF-Expert Member
- Nov 26, 2018
- 3,495
- 5,529
Mkuu labda kwa faida ya wengi;asante sana Mkuu, natafuta jina ambalo mteja akiliona tu anakumbuka kitu kuhusu gali lake au chombo chake na pia kuona kituo chetu ndio soluhisho la tatizo lake.
Mteja wako ni nani?
Atakuwa wapi wakati anaona kituo chako?
Utataka akumbuke nini?
Utataka afanye uamuzi gani?
Katika mambo ya branding kuna kitu kinaitwa "brand engagement" Unataka wateja wako waioneje branda yako.Ni muhimu sana uelewe kwamba JIna ambalo litakuvutia wewe linaweza lisimvutie mteja wako.Pia tambua kwamba kujenga jina la biashara ni kama tu jina lako.Ukipewa jina jipya sasa hivi litakukaa sana by association mfano.Kama Nyamusa sio jina lako halisi naamini kabisa wakati unalichagua kulikuwa na kaprocess kafupi na kama hukukafuata ungesahau hili jina minutes baada ya kulichagua.
Ndivyo inavyokuwa hata kwenye kutafuta Password.
Binafsi najua hii njia ni rahisi but imagine kuna wachangiaji zaidi 200 wamekupa majina na bado unaweza usipate jina sahihi kama hutatumia standards za kuchagua jina.Ama la ukajikuta unarudi mezani tena kulitafutia jina mantiki.
Nasema hivi kwa sababu ya uzoefu na pia kwa sababu hii ni kazi ambayo nimeona watu wengi wanaifanya kienyeji baadae BRAND yako inapokuwa kubwa unaanza kuchukia jina ulilochagua kwa sababu haliendani na kiwango chako.
Do it right now kwa sababu naamini kwamba you have the time,energy and the resources.RIGHT BRANDING attracts RIGHT type of Clients