Nape, Lusinde walichokuta Mwanza kimewatosha

Nape, Lusinde walichokuta Mwanza kimewatosha

Waandishi wetu wana matatizo makubwa, ukimsoma Fredrick Katulanda wa Mwananchi unapata picha kama vile Nape hakuongea lolote la maana kwenye huo mkutano, lakini ukisoma gazeti la Majira unapata vitu vingi vya msingi vilivyoongelewa kwenye huo mkutano, vitu ambavyo Mr. Katulanda hakuona kama ni vya msingi kuviandika, huu ni upumbavu mkubwa.

Ni vizuri waandishi waache upenzi, wafanye kazi yao kitaaluma, wajitahidi kubalance story zao kwa kadri ya uwezo wao ili umma ujue kilichofanyika kwa usahihi, sina hakika kama Katulanda sio kanjanja, lakini ata kama ni Kanjanja, akili za kawaida zingemtuma kuelezea zaidi "maudhui" kuliko "chombezo" zisizo na msingi.

MAJIRA - GAZETI HURU LA KILA SIKU:: Magamba yazidi kuiandama CCM

....Wakati kumekuwapo na msuguano na maelezo kuwa Katibu wa Halmashauri Kuu, Itikadi na Uenezi, Bw. Nape Nnauye anapotosha maagizo ya chama chake kuhusu dhana hiyo, yeye ameibuka na kusema mageuzi yanayoendelea ndani ya chama hicho maarufu kama kujivua gamba ni ya kweli, na yakifanyika ipasavyo ni ukombozi kwa wananchi wanyonge wa Tanzania lakini machungu kwa kundi linalofaidika na jasho lao.

Akihutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara jijini Mwanza jana kwenye viwanja vya Magomeni, Kirumba, Bw. Nnauye alisema mageuzi hayo ni ukombozi kwa wanyonge kwa kuwa yamelenga kuimarisha misingi ya uadilifu na kuwajibika kwa viongozi waliopewa dhamana.

"Ni rahisi leo kumkuta kiongozi anamiliki utajiri wa kutisha na kufuru kuliko hata kipato chake halali, tukisema tukae kimya nchi hii haitatawalika. Dawa ni kufanya mageuzi haya leo kabla hali haijachafuka sana," alisema na kuongeza.

Kwa mujibu wa Bw. Nnauye, kufanikiwa kwa mageuzi hayo kutasaidia kuhakikisha kunakuwapo mgawanyo mzuri wa rasilimali za nchi, hivyo kulewa ukombozi wa moja kwa moja kwa wanyonge nchini.

"Tusisahau ndugu zangu, nguvu ya chama hiki na heshima yake imekuwa ni kutetea wanyonge nchini, Afrika na duniani kwa ujumla. Kutetea wanyonge lazima uhakikishe rasilimali za nchi zinanufaisha wanyonge, bila uadilifu na kuwajibika haitawezekana, ndio malengo ya mageuzi tuyafanyayo," alisema Bw. Nnauye.

Alisisitiza kuwa misingi ya CCM na imani yake vikifuatwa na kusimamiwa vizuri kwa dhati bila unafiki kelele zinazosikika leo za matumizi mabaya ya rasilimali za nchi hazitakuwepo na kuweka wazi kuwa kundi linalofaidika na hali ya sasa, ndilo linalopotosha maana ya mageuzi hayo kwa kutoa hoja alizoita dhaifu.

Alisema kumejengeka utamaduni na hasa kwa baadhi ya watu wenye dhamana kujijali wao wenyewe zaidi kuliko wananchi wanaowaongoza, tabia ambayo imeongeza tofauti ya kipato kati ya wananchi wa chini na viongozi wao, huku wengine wakiwa na kipato kisichokuwa na maelezo sahihi.

"Mwalimu (Nyerere) aliwahi kuwahoji viongozi waliotaka uongozi wa juu wakati huo, kwa umri wenu na kipato chenu mmetoa wapi utajiri huu? Na hiyo ilitosha kumzuia mtu asigombee uongozi, leo ukihoji uadilifu wa baadhi ya viongozi utaandamwa wewe, usipokuwa makini wanakutoa roho," alisisitiza Bw. Nnauye.

Akitoa ufafanuzi zaidi Bw. Nnauye alionya kuwa kama tofauti ya kipato isiposhughulikiwa mapema na hasa kuwadhibiti wale wanaojilimbikizia mali kwa njia haramu wakiwemo viongozi na kugeuza chama kichaka chao, nchi itavurugika kwa kuwa wanyonge ni wengi na watatumia nguvu kudhibiti rasilimali zao na kudai usawa.

Huu ni upupu mtupu.Hakuna la maana aliloongea zaidi ya vita ya wenyewe kwa wenyewe ya kuvuana magamba.Kwani ukimvua gamba Lowassa au Chenge mtanzania wa kawaida atafaidika na nini? Ajira zitaongezeka? Madini yetu yataacha kutoroshwa?
 
magamba mwanza hawana chao, nilikutana na msafara wa wao pale nyamanoro wakitokea airport yaani hadi huruma, hawakuwa na amani kabisa make watu walikuwa wakiwanyoshea ishara ya vidole viwili na hakuna aliyekuwa anatembea kwa miguu kama ilivyo kawaida ya cdm, walikuwa wako kwenye magari na vipikipiki kadhaa vilivyo kuwa vinaendeshwa na wazee kadhaa, yote tisa kumi tuna wasubiri kwa hamu kwenye uchaguzi mdogo wa diwani pale kirumba

mkurugenzi hajatangaza nafasi wazi?
 
Akili ya Nape inakwenda iki-deteriorate kadiri ya siku zinavyosonga. Mbowe na Slaa kuguswa au kutoguswa na risasi si kigezo cha uungwana wa CCM ikiwa Watanzania wengine huko migodini wanauawa na risasi hizo hizo.

Uungwana pia ungeonekana ktk utashi wa kisiasa wa chama katika kutatua matatizo ya wananchi na sio kwenye majukwaa ya kuhubiri amani kwa mdomo. Ikiwa rushwa limekuwa jambo la kawaida kiasi wanaotuhumiwa kwayo hawachukuliwi hatua badala yake wanaombwa kujiuzulu uko wapi uungwana wa CCM?

Kwa maneno mengine Nape anamaanisha kuwa, KATIBA inawaruhusu CCM kupiga watu risasi ila its just a matter of old friendship that they don't do so to CDM leaders. Na kudhihirisha hilo, polisi walipofika hakuna hatua zilizochukuliwa dhidi ya Green Guards waliokuwa wanatumia haki yao ya kikatiba kuadhibu watu walioleta fujo.

Hiyo ndio CCM (inayonadi amani mdomoni ilhali matendo ni hatarishi) hao ndio vijana wa Tanzania (waliochoka kusikia maneno ya kujazilishia mistari) na hizo ndio sera za CCM (kwa kuwa fulani katembea nchi nzima akipanda majukwaani basi na sisi tupande hata kama hatuna cha kuongea)

By the way nichukue nafasi hii kumpongeza mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Nishati na Madini Mh. January Makamba kwa ukomavu wa kisiasa na uthubutu wa (japo maongezi) kuikosoa serikali mbovu iliyopo madarakani. Yeye kama mimi, ameshangazwa na hatua ya AG ambaye awali alikuwa wa kwanza kutangaza kuwa hamna namna ya Tanzania inaweza kukwepa kulipa deni la DOWANS kuwa wa mbele tena kuisimamia TANESCO kuweka pingamizi la usajili wa TUZO mahakamani. Nilijiuliza sana, wkt anasema hatuna namna ya kuepuka deni alikuwa ameazima ubongo wa nani na wakati anapeleka pingamizi mahakamani aliazima wa nani.

Angalizo kwa wananchi walio bado na matumaini kwa AG. Frederick Werema ni mwanasheria mkuu wa serikali na kamwe msidhani ni mwanasheria mkuu wa Tanzania. Kazi yake ni ku-justify madudu ya serikali na wala sio kuitetea Tanzania kama nchi.

Mungu wabariki Watanzania, kama vile ulivyoibariki nchi uliowapa. Ukawajalie hekima ya kumtambua mwizi wa mali uliyowapa ambaye kwa kutotambulika kwake ameaminiwa kuwa mlinzi. Uwajaalie watanzania akili na ufahamu wa kuzitambua haki zao, ili hata ufikapo uchaguzi ujao wakipewa mahindi ya msaada wajue ya kwamba ni haki yao kuyapata na wala hayatoki ghalani kwa chama kwa hiyo bado wajione wenye nafasi ya kupiga kura bila kushawishika kwa unga wa sembe, AMINA!

 
Ipo siku mtanielewa hata kama ni baada ya miaka 20, nilisema, kwa mtaji wa siasa unaoendeshwa na ccm, na mtazamo na maadili ya viongozi wa ccm, hata tuwape miaka 100 mingine, hakuna kitu kitaonekana juu ya ardhi hapa tanzania! Tukisema wameshindwa kuleta maendeleo tunamaanisha nini???ukienda mbele hatua 5, ikarudi nyuma hatua kumi na moja! Umepoteza hatua 6.what we have compare what has been done in 50yrs, almost is nothing!!!!
 
kama watu wa CDM walikuwa wengi kushinda wa CCM na walikuwa wanazomea na greenguards wakaenda wakamkamata mfanya fujo mmoja....... Nchi yetu sote basi tuilinde!
HK,
hivi polisi hawana kazi mpaka mtumie hao GG? Uhalali wao upo ktk sheria gani ya JMT?
 
Ipo siku mtanielewa hata kama ni baada ya miaka 20, nilisema, kwa mtaji wa siasa unaoendeshwa na ccm, na mtazamo na maadili ya viongozi wa ccm, hata tuwape miaka 100 mingine, hakuna kitu kitaonekana juu ya ardhi hapa tanzania! Tukisema wameshindwa kuleta maendeleo tunamaanisha nini???ukienda mbele hatua 5, ikarudi nyuma hatua kumi na moja! Umepoteza hatua 6.what we have compare what has been done in 50yrs, almost is nothing!!!!

Kaka mbona Lunyungu nilisha kuelewa .Ila nimesha waonya kujadili mada za huyu Nape ni kutupotezea mjuda haoa .Huyu ache wakamse huko michuzi na facebook si JF jamani .
 
Katika watu amabo siwezi kuwaweka akilini hata kidogo ni huyo kibajaji mwenye elimu darasa la saba Lusinde
 
Waandishi wetu wana matatizo makubwa, ukimsoma Fredrick Katulanda wa Mwananchi unapata picha kama vile Nape hakuongea lolote la maana kwenye huo mkutano, lakini ukisoma gazeti la Majira unapata vitu vingi vya msingi vilivyoongelewa kwenye huo mkutano, vitu ambavyo Mr. Katulanda hakuona kama ni vya msingi kuviandika, huu ni upumbavu mkubwa.

Ni vizuri waandishi waache upenzi, wafanye kazi yao kitaaluma, wajitahidi kubalance story zao kwa kadri ya uwezo wao ili umma ujue kilichofanyika kwa usahihi, sina hakika kama Katulanda sio kanjanja, lakini ata kama ni Kanjanja, akili za kawaida zingemtuma kuelezea zaidi "maudhui" kuliko "chombezo" zisizo na msingi.

Mkuu it depends Mwandishi ameona News ni nini ..?
Labda kaona tukio la greenguard kupiga watu ndio News..., lakini hayo mengine Nape aliyosema sio News sababu ni the same old stories anazotoa kila siku... Mwandishi anaweza kuangalia story from different angle, na sio kuwa reporter na kutoa report ya kila kilichotokea
 
Aaah! Shit yaani wanatukana vijana af hawakupondwa mawe. Ngoja tunawasubili A town walete hizo pumba waone mandazi ya Mungu yatakavyo washusha jukwaani kama Mtikila kule Tarime, hizo pumba wazipeleke huko huko wakofanyia.
 
mkurugenzi hajatangaza nafasi wazi?


Bado mkuu cjui ni kwanini, ukweli makamanda tuna hamu kubwa sana maana magamba wana kahisia fulani kwamba cdm imepooza hapa mwanza si kama ilivyokuwa 2010 kwenye uchaguzi, na kuna tetesi kwa mbali kuwa kifo cha kamanda wetu pale kirumba kina mkono wa magamba, inabidi tuwaonyeshe kazi hawa magamba this time mgombea wa magamba atalamba kura yake na wife wake period.
 
Huu ni upupu mtupu.Hakuna la maana aliloongea zaidi ya vita ya wenyewe kwa wenyewe ya kuvuana magamba.Kwani ukimvua gamba Lowassa au Chenge mtanzania wa kawaida atafaidika na nini? Ajira zitaongezeka? Madini yetu yataacha kutoroshwa?

Kama hauwezi kuona umuhimu wa uadilifu na uwajibikaji wa viongozi katika ustawi wa nchi na watu wake, i am disappointed.

Bw. Nnauye alisema mageuzi hayo ni ukombozi kwa wanyonge kwa kuwa yamelenga kuimarisha misingi ya uadilifu na kuwajibika kwa viongozi waliopewa dhamana.

"Ni rahisi leo kumkuta kiongozi anamiliki utajiri wa kutisha na kufuru kuliko hata kipato chake halali, tukisema tukae kimya nchi hii haitatawalika. Dawa ni kufanya mageuzi haya leo kabla hali haijachafuka sana," alisema na kuongeza.

Kwa mujibu wa Bw. Nnauye, kufanikiwa kwa mageuzi hayo kutasaidia kuhakikisha kunakuwapo mgawanyo mzuri wa rasilimali za nchi, hivyo kulewa ukombozi wa moja kwa moja kwa wanyonge nchini.

"Tusisahau ndugu zangu, nguvu ya chama hiki na heshima yake imekuwa ni kutetea wanyonge nchini, Afrika na duniani kwa ujumla. Kutetea wanyonge lazima uhakikishe rasilimali za nchi zinanufaisha wanyonge, bila uadilifu na kuwajibika haitawezekana, ndio malengo ya mageuzi tuyafanyayo," alisema Bw. Nnauye.

Alisisitiza kuwa misingi ya CCM na imani yake vikifuatwa na kusimamiwa vizuri kwa dhati bila unafiki kelele zinazosikika leo za matumizi mabaya ya rasilimali za nchi hazitakuwepo na kuweka wazi kuwa kundi linalofaidika na hali ya sasa, ndilo linalopotosha maana ya mageuzi hayo kwa kutoa hoja alizoita dhaifu.

Alisema kumejengeka utamaduni na hasa kwa baadhi ya watu wenye dhamana kujijali wao wenyewe zaidi kuliko wananchi wanaowaongoza, tabia ambayo imeongeza tofauti ya kipato kati ya wananchi wa chini na viongozi wao, huku wengine wakiwa na kipato kisichokuwa na maelezo sahihi.

"Mwalimu (Nyerere) aliwahi kuwahoji viongozi waliotaka uongozi wa juu wakati huo, kwa umri wenu na kipato chenu mmetoa wapi utajiri huu? Na hiyo ilitosha kumzuia mtu asigombee uongozi, leo ukihoji uadilifu wa baadhi ya viongozi utaandamwa wewe, usipokuwa makini wanakutoa roho," alisisitiza Bw. Nnauye.

Akitoa ufafanuzi zaidi Bw. Nnauye alionya kuwa kama tofauti ya kipato isiposhughulikiwa mapema na hasa kuwadhibiti wale wanaojilimbikizia mali kwa njia haramu wakiwemo viongozi na kugeuza chama kichaka chao, nchi itavurugika kwa kuwa wanyonge ni wengi na watatumia nguvu kudhibiti rasilimali zao na kudai usawa.
 
Jamani kumbe Tambwe Hiza mlikuwa mnamuonea bure huyu Nape bure kabsaa yaani anafuka daily na anakiua chama kwa speed na tunapoelekea ccm inakwisha kwa mchango mkubwa wa Nape.
 
MKAPA siku ya kufunga mkutano wa ccm jangwani alisema wapinzani sawa na kokoto,je huko hakuna walomzidi umri?
JK wanafunzi wa kata wapatao mimba shuleni ni kutokana na vihere here vyao.
Makamba alipokuwa Musoma alionyeshwa alama ya CHADEMA yaani vidole viwili yeye akaweka kidole katikati.

Fanya utafiti kwanza kabla ya kumtetea uharifu.
 
Kama hauwezi kuona umuhimu wa uadilifu na uwajibikaji wa viongozi katika ustawi wa nchi na watu wake, i am disappointed.

Kwahiyo mkuu na wewe huoni umuhimu wa gazeti kuandika yaliyotokea (yaani the so called green guards kutembeza kichapo..) au kwako wewe hii sio news..?

Huenda hayo Nape aliyoongelea Mwanza gazeti imeshaandika kila akitoa tamko... (yaani hakuna news hapo...) ila watu kupigwa na watu kutoa maneno ya kejeli na ya mitaani (mhh thats news according to me na wapenda amani..) na inabidi tuyakemee
 
Nape na Riz1 siku mtaingia kwenye Eighteen zangu brother mtaomba ardhi ipasuke.
 
Back
Top Bottom