Nape, Lusinde walichokuta Mwanza kimewatosha

Uongo mtupu...angalieni marudio ya Taarifa ya habari ya Star TV kesho asubuhi mtaona...anasingizia eti mimi nilikatisha hotuba yangu wakati niliongea dakika zote nilizokuwa nimepangiwa!

Vijana wa CDM waliokuwepo pale ni wachache sana, kama 15 hivi ukilinganisha na wengi wenye hekima na busara waliokuwa wametulia na kufuatilia hotuba zetu.

WanaJF hebu jiulizeni kitu hapa, kama watu wa CDM walikuwa wengi kushinda wa CCM na walikuwa wanazomea na greenguards wakaenda wakamkamata mfanya fujo mmoja, CDM si wangeleta vurugu mbaya kabisa, pengine hata mauaji? Iliwezekana vipi CCM kuendesha mkutano wake vizuri na kwa amani na utulivu kabisa mpaka mwisho kama kweli kulikuwa na fujo za kiasi kilichoelezewa namna hii?

Waandishi ni mhimili wa nne wa dola, fanyeni kazi yenu kwa ufanisi na kimaadili. Nchi yetu sote basi tuilinde!

TUILINDE VIPI WAKATI NINYI WENYE DHAMANA MNAIMALIZA? Shimbo, Kikwete, Rostam, Ridhiwan,Lowassa, Mkapa. Hao utajiri wao ni bajeti ya serikali miaka 5! Be serious mheshimiwa
 
kaka nina mambo machache naomba unijibu kuhusiana na hiyo sehemu niliyo weka nyekundu

1. Vipi ni halali kwa kila chama kuwa najeshi lake kama hivi mnavyofanya na kuwapeleka makambini kwa ajili ya mafunzo ya kijeshi au ni ruksa kwa ccm tu?

2. Je vijana hawa hulipwa kiasi gani na nani na kwa kufungu lipi au wanajitolea tu kwa mapenzi waliyonayo katika chama chao?

3. Vipi mkuu vijana hawa khali yao kimaisha ikoje wapo angalau wanaomiliki walau nyumba moja ya kisasa au hapana?

4. Mkuu nijuze kuhusu elimu ya vijana wetu hawa kwa wastani elimu yao ni ya kiwango gani ?naomba unijibu hili niweze kuwafahamu kwa kina hawa vijana


mkuu ukiwa kiongozi na ukategemea walinzi na bastola pale unapoenda kuonana na wale unaowaongoza wewe si kiongozi .

Jibu sasa si umejitokeza?
 
walikosea kutuma mashoga, wangetuma wenye akili timamu na wanaume halisi ambao nina wasiwasi kama ccm bado inao. Ccm exit door
 
Vipi hawakuimba ile single yao mpya?JK chama kinamfia mikononi kwa kushindwa kufanya maamuzi sahihi,kwa kuwachagua watu Type za kiNape nape wao wanafikili wanajenga Chama kumbe wanakibomoa kabisa, R.I.P CCM tulikupenda sana lakini SHETANI amekupenda zaidi.
 
I go through the lines sijakutana na sentensi inayozungumzia mimba na kupanda ukuta, sijui kama ndio uandishi wa kisasa ama mpasha habari alikuwa miongoni wa walipokuwepo mkutanoni?!!!!
 
Source yako ambayo ni gazeti la Mwananchi haina matusi ambayo umeandika ktk thread hii sasa tukuaminije au umewalisha maneno?
Sehemu pekee ambapo unaweza kuupata ukweli kama ulivyo ni JF....gazeti sitegemei kama wataandika matusi hayo ya Nape
 
Ndg wa JF msiangaike kujadili anguko la CCM Mwanza kwanza rejea maneno ya NAPE alivyokuwa akiongelea CHADEMA kuleta watu kutoka mikoa ya Mwanza,Arusha na kwingine inadhihirisha kabisa Mwanza ni wapenzi wa sera za Chadema.

Tahadhari kwa wageni mnaoingia Mwanza msivae manguo wala kofia zenu mlizopewa na CCM 2010. Muulize mwenyekiti wa soko la Mlango Mmoja kilichomtokea............ ukiwa Mlango Mmoja, Makoroboi, Kirumba na maeneo mengine hutakiwi kuongelea CCM hata kidogo.
 
Nape anaamini hivi pia?
Hawa jamaa wamechanga nyikiwa huyu anasema hivi huku mwingine anasema kinyume chake...Nape alisema nchii hii ina wenyewe Kimwangalla ana sema nchii ni yetu sote sasa sijui wana amini lipi............
 
Frederick Katulanda, Mwanza-Mwananchi

MKUTANO wa hadhara wa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye uliofanyika jana kwenye Uwanja wa Magoneni, Kirumba jijini hapa,

Nape alianza kwa kuwapongeza Nchemba na Lusinde akisema walipokuwa wakizungumza walikuwa wakikamata pua za wagonjwa wakorofi ili yeye aweze kuwanywesha dawa.

Wakati akihutubia, vijana wa Green Guard walianza kufanya doria kuwasaka wazomeaji na kijana wa kwanza alikamatwa na kushambuliwa na vijana zaidi ya saba kiasi cha kumfanya Nape kukatisha hotuba yake kumuokoa.

Hali ilichafuka tena pale aliposema viongozi wa upinzani hawana uchungu na nchi na kwamba CCM ni waungwana na ndiyo maana Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Katibu wake Mkuu, Dk Wilibroad Slaa hawajawahi kuguswa kwa risasi huku akiwahoji kuwa tangu siasa za vyama vingi zianze ni wapi ambako viongozi hao walifanyiwa hivyo? Hata hivyo, alijibiwa kwa nguvu na kundi la watu ... "Arusha."

Majibu hayo yalisababisha vurugu nyingine kwani kijana mwingine alikamatwa na kuanza kupigwa na vijana hao wa CCM kabla ya gari la Polisi kuwasili na kuanza kuzunguka katika uwanja huo kulinda amani.

Waandishi wetu wana matatizo makubwa, ukimsoma Fredrick Katulanda wa Mwananchi unapata picha kama vile Nape hakuongea lolote la maana kwenye huo mkutano, lakini ukisoma gazeti la Majira unapata vitu vingi vya msingi vilivyoongelewa kwenye huo mkutano, vitu ambavyo Mr. Katulanda hakuona kama ni vya msingi kuviandika, huu ni upumbavu mkubwa.

Ni vizuri waandishi waache upenzi, wafanye kazi yao kitaaluma, wajitahidi kubalance story zao kwa kadri ya uwezo wao ili umma ujue kilichofanyika kwa usahihi, sina hakika kama Katulanda sio kanjanja, lakini ata kama ni Kanjanja, akili za kawaida zingemtuma kuelezea zaidi "maudhui" kuliko "chombezo" zisizo na msingi.

MAJIRA - GAZETI HURU LA KILA SIKU:: Magamba yazidi kuiandama CCM

....Wakati kumekuwapo na msuguano na maelezo kuwa Katibu wa Halmashauri Kuu, Itikadi na Uenezi, Bw. Nape Nnauye anapotosha maagizo ya chama chake kuhusu dhana hiyo, yeye ameibuka na kusema mageuzi yanayoendelea ndani ya chama hicho maarufu kama kujivua gamba ni ya kweli, na yakifanyika ipasavyo ni ukombozi kwa wananchi wanyonge wa Tanzania lakini machungu kwa kundi linalofaidika na jasho lao.

Akihutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara jijini Mwanza jana kwenye viwanja vya Magomeni, Kirumba, Bw. Nnauye alisema mageuzi hayo ni ukombozi kwa wanyonge kwa kuwa yamelenga kuimarisha misingi ya uadilifu na kuwajibika kwa viongozi waliopewa dhamana.

"Ni rahisi leo kumkuta kiongozi anamiliki utajiri wa kutisha na kufuru kuliko hata kipato chake halali, tukisema tukae kimya nchi hii haitatawalika. Dawa ni kufanya mageuzi haya leo kabla hali haijachafuka sana," alisema na kuongeza.

Kwa mujibu wa Bw. Nnauye, kufanikiwa kwa mageuzi hayo kutasaidia kuhakikisha kunakuwapo mgawanyo mzuri wa rasilimali za nchi, hivyo kulewa ukombozi wa moja kwa moja kwa wanyonge nchini.

"Tusisahau ndugu zangu, nguvu ya chama hiki na heshima yake imekuwa ni kutetea wanyonge nchini, Afrika na duniani kwa ujumla. Kutetea wanyonge lazima uhakikishe rasilimali za nchi zinanufaisha wanyonge, bila uadilifu na kuwajibika haitawezekana, ndio malengo ya mageuzi tuyafanyayo," alisema Bw. Nnauye.

Alisisitiza kuwa misingi ya CCM na imani yake vikifuatwa na kusimamiwa vizuri kwa dhati bila unafiki kelele zinazosikika leo za matumizi mabaya ya rasilimali za nchi hazitakuwepo na kuweka wazi kuwa kundi linalofaidika na hali ya sasa, ndilo linalopotosha maana ya mageuzi hayo kwa kutoa hoja alizoita dhaifu.

Alisema kumejengeka utamaduni na hasa kwa baadhi ya watu wenye dhamana kujijali wao wenyewe zaidi kuliko wananchi wanaowaongoza, tabia ambayo imeongeza tofauti ya kipato kati ya wananchi wa chini na viongozi wao, huku wengine wakiwa na kipato kisichokuwa na maelezo sahihi.

"Mwalimu (Nyerere) aliwahi kuwahoji viongozi waliotaka uongozi wa juu wakati huo, kwa umri wenu na kipato chenu mmetoa wapi utajiri huu? Na hiyo ilitosha kumzuia mtu asigombee uongozi, leo ukihoji uadilifu wa baadhi ya viongozi utaandamwa wewe, usipokuwa makini wanakutoa roho," alisisitiza Bw. Nnauye.

Akitoa ufafanuzi zaidi Bw. Nnauye alionya kuwa kama tofauti ya kipato isiposhughulikiwa mapema na hasa kuwadhibiti wale wanaojilimbikizia mali kwa njia haramu wakiwemo viongozi na kugeuza chama kichaka chao, nchi itavurugika kwa kuwa wanyonge ni wengi na watatumia nguvu kudhibiti rasilimali zao na kudai usawa.
 
Mambo yanayofanywa na sisiem na green guard wao ni mwanzo wa civil war. Ninasubiri siku umma uki counter react kwa manyanyaso ya green guard.

Mimi nadhani wakati umefika wa sisiemu kumvote out jk ameshindwa kazi nafuu fisadi el
 
Siasa za Kuzomeana ni uhuni ambao wanasiasa pande zote lazima wazikemee! Hatuwezi kujenga na Kukuza Taifa la Wazomeaji! Tubishane kwa hoja na kumsikiliza kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni yake hapo ndipo tupime kama ni porojo au pointi!
 

Akihutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara jijini Mwanza jana kwenye viwanja vya Magomeni, Kirumba, Bw. Nnauye alisema mageuzi hayo ni ukombozi kwa wanyonge kwa kuwa yamelenga kuimarisha misingi ya uadilifu na kuwajibika kwa viongozi waliopewa dhamana.

"Ni rahisi leo kumkuta kiongozi anamiliki utajiri wa kutisha na kufuru kuliko hata kipato chake halali, tukisema tukae kimya nchi hii haitatawalika. Dawa ni kufanya mageuzi haya leo kabla hali haijachafuka sana," alisema na kuongeza.

"Tusisahau ndugu zangu, nguvu ya chama hiki na heshima yake imekuwa ni kutetea wanyonge nchini, Afrika na duniani kwa ujumla. Kutetea wanyonge lazima uhakikishe rasilimali za nchi zinanufaisha wanyonge, bila uadilifu na kuwajibika haitawezekana, ndio malengo ya mageuzi tuyafanyayo," alisema Bw. Nnauye.

Akitoa ufafanuzi zaidi Bw. Nnauye alionya kuwa kama tofauti ya kipato isiposhughulikiwa mapema na hasa kuwadhibiti wale wanaojilimbikizia mali kwa njia haramu wakiwemo viongozi na kugeuza chama kichaka chao, nchi itavurugika kwa kuwa wanyonge ni wengi na watatumia nguvu kudhibiti rasilimali zao na kudai usawa.

Kumbe ni mamia ya watu na sio maelfu ya watu?
umenithibitishia hata 1000 walikuwa hawafiki. nashukuru sana.

Nape ni mwizi wa mali za umma, unaomfanya aendelee kukaa CCM. Kama sio uchu wa kujilimbikizia mali, nadhani nape asingekuwa CCM. Alitishia kujiondoa kwenye chama, kumpoza akapewa ukuu wa wilaya huko mkoani mtwara.

kuendelea kumshikilia, amepandishwa daraja na kupewa ukatibu wa majungu, ili atengeneze pesa zaidi na awasaidie kutawala hawa wezi wanakwapua kila uchwao.

ipo siku haya yote, yatakoma. Mwanza, Arusha, Mbeya, Kigoma tayari wameamka. Na ushindi kiduchu wa CCM tena wa hila kule Igunga, ni ushahidi kuwa CCM wajiandae kukabidhi viongozi mbadala ili waisafishe nchi iliyojaa harufu ya wizi na ufisadi.
 
Siasa za Kuzomeana ni uhuni ambao wanasiasa pande zote lazima wazikemee! Hatuwezi kujenga na Kukuza Taifa la Wazomeaji! Tubishane kwa hoja na kumsikiliza kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni yake hapo ndipo tupime kama ni porojo au pointi!

ni nadra sana kusikia CDM, CUF, NSSR, na wengine wakizomewa. hawa wanapewa uhuru wa kujieeleza, kwani wananadi sera zao ambazo hazijawahi kutumika au kusimamiwa tangu miaka 50 ya uhuru ipite.

CCM watazomewa sana kwani hakuna jipya wanalokuja nalo, na wananchi tayari wamewachoka, kwani pamoja na nchi kuwa tajiri wa rasilimali, bado wananchi na bajeti ya taifa tumekuwa ombaomba kwa wezi wa rasilimali zetu. katika mazingira haya, nani wa kuwasikiliza CCM kama sio kuwazomea na kuwataka wakae kando kama mwasisi alivyofanya?
 
Nape umeishiwa na busara wewe hufai kuwa kiongozi na hufai kuigwa na jamii. kama kweli umesema maneno hayo shame be upon you!!!!!!!
Nape anachama chake anataka kuuiua CCM ili aibukie chama chake cha CCJ......
 
Siasa za Kuzomeana ni uhuni ambao wanasiasa pande zote lazima wazikemee! Hatuwezi kujenga na Kukuza Taifa la Wazomeaji! Tubishane kwa hoja na kumsikiliza kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni yake hapo ndipo tupime kama ni porojo au pointi!
Ukiona unachangiliwa kumbuka IKO SIKU UTAKUWA UNAZOMEWA SASA KIPINDI CHA KUSHANGILIWA KWA ccm KIMEISHA NA SASA NI KUZOMEWA NDIYO MPANGO MZIMA...ccM WASHANGILIWE KWA LIPI SASA HIVI HAWANA JIPYA ACHA WAZOMEWE KWANZA WAKAZI WA MWANZA WAMEONYESHA UVUMILIVU KAMA WALITUKANWA MATUSI YOTE HAYO HAWAKUWAPOPOA MAWE....
 
Magamba mwanza hawana chao, nilikutana na msafara wa wao pale nyamanoro wakitokea airport yaani hadi huruma, hawakuwa na amani kabisa make watu walikuwa wakiwanyoshea ishara ya vidole viwili na hakuna aliyekuwa anatembea kwa miguu kama ilivyo kawaida ya cdm, walikuwa wako kwenye magari na vipikipiki kadhaa vilivyo kuwa vinaendeshwa na wazee kadhaa, yote tisa kumi tuna wasubiri kwa hamu kwenye uchaguzi mdogo wa diwani pale kirumba
 
Back
Top Bottom