Uongo mtupu...angalieni marudio ya Taarifa ya habari ya Star TV kesho asubuhi mtaona...anasingizia eti mimi nilikatisha hotuba yangu wakati niliongea dakika zote nilizokuwa nimepangiwa!
Vijana wa CDM waliokuwepo pale ni wachache sana, kama 15 hivi ukilinganisha na wengi wenye hekima na busara waliokuwa wametulia na kufuatilia hotuba zetu.
WanaJF hebu jiulizeni kitu hapa, kama watu wa CDM walikuwa wengi kushinda wa CCM na walikuwa wanazomea na greenguards wakaenda wakamkamata mfanya fujo mmoja, CDM si wangeleta vurugu mbaya kabisa, pengine hata mauaji? Iliwezekana vipi CCM kuendesha mkutano wake vizuri na kwa amani na utulivu kabisa mpaka mwisho kama kweli kulikuwa na fujo za kiasi kilichoelezewa namna hii?
Waandishi ni mhimili wa nne wa dola, fanyeni kazi yenu kwa ufanisi na kimaadili. Nchi yetu sote basi tuilinde!