Naomba kujua tabia za wasukuma

Naomba kujua tabia za wasukuma

stable woman

JF-Expert Member
Joined
Nov 12, 2013
Posts
3,883
Reaction score
4,484
Habarini,

Natumaini mu wazima, leo hebu tugeukie kanda ya ziwa tupeane tabia za wasukuma. Mdogo wangu anatarajia kuolewa hivi karibuni na msukuma mmoja hivi, sasa naombeni mtusaidie kujua tabia zao. Kama kuna mila na akitakiwa kwenda ukweni usukumani inabidi afanye mambo gani kufanana nao ili wamfurahie?

Ni hayo tu ahsanteni.
 
Wewe ushaolewa? Kama bado nikwambie tabia za kwetu
 
....

Tuko powa tu wasiwasi wako tu muulize mdogo wako kaingiaje kwenye 18 !!!!
 
Duh, wana haiba ya kufa mtu lakini waongo, matapeli kwa ujumla siyo waoaji, mimi mwanangu aliolewa usukumani cha moto alikiona, kapigishwa hadi matofali
Lakini wakarimu sana, ukiwa kwao ukiomba maji ya kunywa wanakupa buyu la maziwa
 
He he he, huyo binti akitaka kuja huku, awe na kanga pair walau 2, prefarably njano.
Awe na raba, urembo wa binti ni kuvaa raba, tena kijani ama bluu
Awe na gauni la maua meeengi, rangi za kung'aa ndio swagger
Awe kasuka twende kilioni
Asikose mafuta ya mamiz
Ajifunze kupiga goti, tena lile la kusalimia watu 20 mmoja mmoja iukiwa chini. Au akitumwa mwaji anapiga goti hadi mnywaji amalize.
Ajue salam. 'lwembo' la mumewe lazima ajue
Ajue kusonga ugali, uwe mgumu sio huu uji tunaopikiwa huku Dar tunadanganywa ni ugali

Nitarudi...
 
Duh, wana haiba ya kufa mtu lakini waongo, matapeli kwa ujumla siyo waoaji, mimi mwanangu aliolewa usukumani cha moto alikiona, kapigishwa hadi matofali
Lakini wakarimu sana, ukiwa kwao ukiomba maji ya kunywa wanakupa buyu la maziwa

Hahahahah
 
Oooh madam! Uliwahi kumwuliza mdogo kama alimgoogle huyu msukuma kwenye internet kabla ya kuamua kuwa nae?
Sorry kaswali ka nyongeza please! Naaaa kama kuna katabia ka huyo msukuma ambapo hakakufai wewe ila kanamsuite mdogo wako inaaa....inaaa..ina maana utamshauri asiolewe? One more question please! Unaweza kututajia kabila la mumeo/mchumba wako ili tukupe sifa za kabila lake ili tuone kama utaendelea kuwa nae? Thanks
 
Anakaribishwa sn,mawifi tupo tumejaa tele. Wasukuma tuko wakarimu sn lkn cha msingi ajue kupiga magoti,salam za lwimbo ni muhimu kujua,asiwe mzembe yaan kufanya kazi hd mama mkwe aseme hiyo haipo kwet usukumani. Ajue kupika ugali wa asb wa " ndemi" na watoto,ajiandae kupata brekfast ya maziwa mgando na viazi au mchembe.
Kiufupi usukumani ni raha sana,atajua hd kukamua maziwa ya ng'ombe. Ngoja nikomee hapa,bhagwiza na bhichane ogongeja gange enguno kaliho minge nno.
 
Mfumo dume ndio mpango mzima. Jiandae kwa suprise za kutosha. Uchawi ni jambo la kawaida nk
 
Duh, wana haiba ya kufa mtu lakini waongo, matapeli kwa ujumla siyo waoaji, mimi mwanangu aliolewa usukumani cha moto alikiona, kapigishwa hadi matofali
Lakini wakarimu sana, ukiwa kwao ukiomba maji ya kunywa wanakupa buyu la maziwa

huyu uvivu ulimtoa sukuma land sisi hatujazoea kuomba omba kama jamaa zetu wa kanda ile ya akina Matonya tunakula kwa jasho.....hivyo ajiandae kuja kula kwa jasho lake.

.......Ni wakarimu uchoyo tunasikia kwa majirani tu

.........Hatupendi mwanamke anaye ongea kama chiriku maana sisi ni watu wa kazi hatupendi longolongo.
.........Zile sketi fupi,vinguo vya kuonyesha maziwa aziache hukohuko atazikuta akija kuwasalimia baada ya kutuzalia watoto wa kutosha.
...........Ruksa ndugu zako kuja kukutembelea hata wasipotoa taarifa maana kinachowafanya watu wapige kelele wakitembelewa bila taarifa ni njaa tu,sisi njaa tunasikia hatujui inafananaje.

Baada ya kuyajua hayo karibu sana shemeji wise.
 
Mfumo dume ndio mpango mzima. Jiandae kwa suprise za kutosha. Uchawi ni jambo la kawaida
nk

Operesheni tokomeza wachawi ilisha pita usimtishe shemeji yetu siku hizi tulishakuwa watoto wa Mungu

........hata imekuwa mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya ya kale yamepita tazama yamekuwa mapya"
 
huyu uvivu ulimtoa sukuma land sisi hatujazoea kuomba omba kama jamaa zetu wa kanda ile ya akina Matonya tunakula kwa jasho.....hivyo ajiandae kuja kula kwa jasho lake.

.......Ni wakarimu uchoyo tunasikia kwa majirani tu

.........Hatupendi mwanamke anaye ongea kama chiriku maana sisi ni watu wa kazi hatupendi longolongo.
.........Zile sketi fupi,vinguo vya kuonyesha maziwa aziache hukohuko atazikuta akija kuwasalimia baada ya kutuzalia watoto wa kutosha.
...........Ruksa ndugu zako kuja kukutembelea hata wasipotoa taarifa maana kinachowafanya watu wapige kelele wakitembelewa bila taarifa ni njaa tu,sisi njaa tunasikia hatujui inafananaje.

Baada ya kuyajua hayo karibu sana shemeji wise.

Wabheja kulomba bhabha...

Namkaribisha wifiii kwa mikono na miguu.. Masato na masangara ghete yamejaaga!!!
 
Anakaribishwa sn,mawifi tupo tumejaa tele. Wasukuma tuko wakarimu sn lkn cha msingi ajue kupiga magoti,salam za lwimbo ni muhimu kujua,asiwe mzembe yaan kufanya kazi hd mama mkwe aseme hiyo haipo kwet usukumani. Ajue kupika ugali wa asb wa " ndemi" na watoto,ajiandae kupata brekfast ya maziwa mgando na viazi au mchembe.
Kiufupi usukumani ni raha sana,atajua hd kukamua maziwa ya ng'ombe. Ngoja nikomee hapa,bhagwiza na bhichane ogongeja gange enguno kaliho minge nno.

Tuko juu .....

.... na watoto asisahau kuwatunza haswa misosi ya nguvu katika umri mdogo !!!




dsc_0087.jpg
 
yaani kwetu ukitaka kuja hakuna haja ya taarifa unakuja tu hata kama muwe wa5 mtakula na kushiba ila asiwe mzembe na muongeaji sana kupiga magoti ndio kila kitu na muhimu kuliko vyote ajifunze kisukuma na aijue salamu mazungumzo mengine tutavumilia mwanzoni
 
Back
Top Bottom