Naomba kujua faida za kusoma nje ya Nchi (Bachelor of Science In Agricultural Engineering)

Chiefff

Member
Oct 22, 2015
17
6
Naomba kujua faida za kusoma nje ya Nchi (Bachelor of Science In Agricultural Engineering).

Habari ndugu zangu,
Mimi ni kijana, nimezaliwa na kukulia katika kijiji kimoja kilichopo Mkoani Shinyanga. Nilihitimu stashahada ya uhandisi Kilimo miaka kadhaa iliyopita kutoka chuo cha Wizara ya Kilimo hapa nchini. Nilifanikiwa kuwa mwanafunzi bora wa mwaka.

Baada ya kuhitimu, nimeweza kufanya kazi za mikataba katika taasisi binafsi mbili na taasisi ya Umma moja. Katika kuendelea kutafuta fursa mbalimbali niliweza kufanya maombi ya ufadhili wa masomo ya Elimu ya juu nje ya Nchi Kwa ngazi ya Shahada. Mungu amenisaidia nimepata ufadhili kwenda kusoma Shahada ya Kwanza ya uhandisi wa Kilimo katika Bara la Ulaya.

Naandika Uzi huu kuomba kujua faida za kusoma nje ya Nchi Kwa kozi ya Bachelor of Science in Agricultural Engineering, Fursa katika kujiajiri, pia naomba kujua ni organizations zipi za kimataifa naweza kufanya kazi kama nikihitimu Shahada hii.

Natanguliza shukrani.
 
Naomba kujua faida za kusoma nje ya Nchi (Bachelor of Science In Agricultural Engineering).

Habari ndugu zangu,
Naitwa Chiefff, Nimezaliwa na kukulia katika kijiji kimoja kilichopo Mkoani Shinyanga. Nilihitimu stashahada ya Zana za Kilimo (Diploma in Agro-Mechanics) miaka kadhaa iliyopita kutoka chuo cha Wizara ya Kilimo hapa nchini. Nilifanikiwa kuwa mwanafunzi bora wa mwaka.

Baada ya kuhitimu, nimeweza kufanya kazi za mikataba katika taasisi binafsi mbili na taasisi ya Umma moja. Katika kuendelea kutafuta fursa mbalimbali niliweza kufanya maombi ya ufadhili wa masomo ya Elimu ya juu nje ya Nchi Kwa ngazi ya Shahada. Mungu amenisaidia nimepata ufadhili kwenda kusoma Shahada ya Kwanza ya uhandisi wa Kilimo katika Bara la Ulaya nchini Hungary.

Naandika Uzi huu kuomba kujua faida za kusoma nje ya Nchi Kwa kozi ya Bachelor of Science in Agricultural Engineering, Fursa katika kujiajiri, pia naomba kujua ni organizations zipi za kimataifa naweza kufanya kazi kama nikihitimu Shahada hii.

Natanguliza shukrani.
Hiki ulicho andika sioni kama kina mantiki, umepata nafasi nenda kasome!

NB: Nje ni nje huwezi linganisha na bongo!
 
Nenda kafungue macho, huko utapata elimu sio tu ya darasani bali ya duniani kujua jamii zingine zinaishi vipi kulinganisha na ulikotoka....
Au unaweza hata pata mdada wa kihangaria uje kuturingishia huku...
 
Nenda kafungue macho, huko utapata elimu sio tu ya darasani bali ya duniani kujua jamii zingine zinaishi vipi kulinganisha na ulikotoka....
Au unaweza hata pata mdada wa kihangaria uje kuturingishia huku...
Kwahiyo Kiongozi Faida ya kusoma nje ya Nchi Bachelor of Science in Agricultural Engineering ni kupata mdada wa Kihangaria?
 
Kwahiyo Kiongozi Faida ya kusoma nje ya Nchi Bachelor of Science in Agricultural Engineering ni kupata mdada wa Kihangaria?
Nenda utawakuta watz uko budapest wanaassociation yao wana wake kabisa na watoto wakihungary na kuna mgahawana wa african food kuna mnigeria na mtz wte wanapiga kiswahili.

Maisha yako juu kidogo hii nchi but yanahimilika
 
Nenda utawakuta watz uko budapest wanaassociation yao wana wake kabisa na watoto wakihungary na kuna mgahawana wa african food kuna mnigeria na mtz wte wanapiga kiswahili.

Maisha yako juu kidogo hii nchi but yanahimilika
Kaka inaonekana unapafahamu vizuri huko. Safi Sana. Asante Kwa Information.
 
Kwahiyo Kiongozi Faida ya kusoma nje ya Nchi Bachelor of Science in Agricultural Engineering ni kupata mdada wa Kihangaria?
Yaani ukimpata dada wa kihangaria mka settle down, hiyo ndio passport ya kuishi nchi yoyote ya Umoja wa Ulaya, iwe Germany, France, mpaka hata nchi za Scandnavia...
 
Yaani ukimpata dada wa kihangaria mka settle down, hiyo ndio passport ya kuishi nchi yoyote ya Umoja wa Ulaya, iwe Germany, France, mpaka hata nchi za Scandnavia...
Kiongozi, Lengo siyo kupata dada wa Kihangaria na kuishi huko. Lengo ni kupata Elimu ambayo itakuwa msaada kwangu na Kwa jamii inayonizunguka nyumbani Tanzania.
 
Kiongozi, Lengo siyo kupata dada wa Kihangaria na kuishi huko. Lengo ni kupata Elimu ambayo itakuwa msaada kwangu na Kwa jamii inayonizunguka nyumbani Tanzania.
Wewe tu na uzalendo wake mkuu, , labda kama una koneksheni ukirudi na kupata kazi moja kwa moja badala kuhangaika na ajira portal
Zaidi ya hapo, hii ni fursa na inaweza kutokea mara moja tu maishani, na ukikaa zaidi huko ulaya , ni rahisi kutafuta fursa huko uje kuwekeza kwenye kilimo sio kurudi kuwa afisa kilimo unasubiri kupandishwa daraja la mshahara Kila Mei Mosi..
 
Wewe tu na uzalendo wake mkuu, , labda kama una koneksheni ukirudi na kupata kazi moja kwa moja badala kuhangaika na ajira portal
Zaidi ya hapo, hii ni fursa na inaweza kutokea mara moja tu maishani, na ukikaa zaidi huko ulaya , ni rahisi kutafuta fursa huko uje kuwekeza kwenye kilimo sio kurudi kuwa afisa kilimo unasubiri kupandishwa daraja la mshahara Kila Mei Mosi..
Akachungulie eduflyx insta aone Poland is hiring uko paid in dollars😄

Actually mimi isingekuw vita ningekuw Canada sahivi
 
Naomba kujua faida za kusoma nje ya Nchi (Bachelor of Science In Agricultural Engineering).

Habari ndugu zangu,
Naitwa Chiefff, Nimezaliwa na kukulia katika kijiji kimoja kilichopo Mkoani Shinyanga. Nilihitimu stashahada ya Zana za Kilimo (Diploma in Agro-Mechanics) miaka kadhaa iliyopita kutoka chuo cha Wizara ya Kilimo hapa nchini. Nilifanikiwa kuwa mwanafunzi bora wa mwaka.

Baada ya kuhitimu, nimeweza kufanya kazi za mikataba katika taasisi binafsi mbili na taasisi ya Umma moja. Katika kuendelea kutafuta fursa mbalimbali niliweza kufanya maombi ya ufadhili wa masomo ya Elimu ya juu nje ya Nchi Kwa ngazi ya Shahada. Mungu amenisaidia nimepata ufadhili kwenda kusoma Shahada ya Kwanza ya uhandisi wa Kilimo katika Bara la Ulaya nchini Hungary.

Naandika Uzi huu kuomba kujua faida za kusoma nje ya Nchi Kwa kozi ya Bachelor of Science in Agricultural Engineering, Fursa katika kujiajiri, pia naomba kujua ni organizations zipi za kimataifa naweza kufanya kazi kama nikihitimu Shahada hii.

Natanguliza shukrani.
Faida za kusoma nje kwanza ni kwamba unakuwa umeshindikana, mtu yeyote akikusogelea unamzibua!

Pili, kusoma nje ni kama kutoka nje ya ndoa, unaamua tu kwamba unaachana na mambo ya umanju unaanza kuimba ngonjera za hapa na pale..

Tatu, suala la saikomania halikupigi chenga, unakuwa intertwined katika michepuko.

Nne, sio tu kwamba ni psychological phenomena, it is AMBIQUITY!

Sababu nyingine ni wizi wa kukusudia, mfano mass media ikiamua kukukimbiza, inakuwa haina shobo..

Hoja ya mwisho ni kuangalia suala la global trend, maana ni hatari zaidi ukikuta kumbe hayawi hawayi yamèkuwa,

Mwisho kabisa nikutakie ibada njema shehe wangu, Alamsik.
 
Back
Top Bottom