Naomba kueleweshwa kuhusu hii tabia

Naomba kueleweshwa kuhusu hii tabia

Nilishamwambia mwenyewe na wala hakujishtukia uwa sipendi kuingiza masuala ya marafiki kwenye relationship yangu
Pole sana, labda jamaa hakuwa na lengo na wewe alitaka kula mzigo na kukimbia. Sasa ulipoanza kumpa majukumu akaona unataka kujiweka moja kwa moja ndiyo akaamua kukimbia.

Omba mungu utampata mwingine mwelevu.

Ila jihadhali na kueleza shida zako kabla hamjafamiana vya kutosha.

Mfanye utakaye mpata akuone ni mtu uliyetosheka na hali yako hiyo itakuongezea sana thamani.
 
Hope mpo poa
Jamani kwa mfano unakuwa na boyfriend na mmepanga kumeet vizuri tu baadae ikatokea kitu ukamwambia naomba unisaidie hela kwa maana kuna mtu anahitaji na mimi nipo mbali na sehemu ya kutuma hela isitoshe haujawahi kumuomba hata siku moja ni hiyo siku tu ndo imetokea ukamuomba hela......baadae unampigia simu kumwambia mambo mengine hapokei simu zako wala kukujibu text......hivi kwanini inakuwa hivi naomba kujua
Kama in MTU mzm Basi ujue hana hela ,,kama ni kijana ujue anachotaka kwako no mchezo tu
 
Mwenzako alitafsiri kuwa UMEMUINGIZA KWENYE MFUMO WA"PRE-PAID" yaani lipia kabla ya kutumia" mfumo ambao unatumika kiujanja sana na wanawake wengi siku hizi.
 
Kuna wanaume watasingizia pesa kwa sababu wanazo kuwa wakiombwa inakuwa kama wananua kitu. Ila wengine hawakumbuki mwanamke anaweza kuwa anamfanyia mengi wanapokuwa pamoja na hapo mwanaume hana kitu.. ila kumbe akija kupata anageuka.

Hiyo sio excuse kitu ni mwanaume kutojua mapenzi, mwanaume anayejua mapenzi na kumfurahisha mwanamke atajua pesa sio kitu bali furaha.
 
Na tabia ya wanaodai hawapendwi kuombwa ni ubahiri umewajaaa, mtu anaweza kuishi ukija sikia anakuambia yake unajiuliza huyu sasa mbona hajipendi!!!...mtu anajiweka low class huku haimsaidiii ubahiri wa nini.... ukifa kesho?... wengine tabu yao kubeba wanawake hawajui kujiongeza na kuwaongeza wapenzi wao.

Wengine ila kutojua kuongea na ukija kumchunguza lazima utakuta majanfa, ila haina haja.

Mwanamke kumuonyesha mwanaume unampenda naye akanyamazia au kukuignore.. mmmh jaribisha kumpima ki kila utofauti

One day utasikia roho yako inasema imetosha na unakuwa freee... hata ulichofanya au kumwambia siku 3 au 4 kabla unajikuta huwezi hata jaribu kwa sababy unamuona imetoka hiyooo.
 
Mapenzi ni kujipa furaha. Muwe marafiki mnaoelewana. Mawasiliano yanoge hata mkikaa siku nyingi ila mwingine anapokuandikia kitu unajibu...

Sasa utakuta mivianaume eti vinaamvia wanawake wapo buzy... eeeh hapi sasa wanajilazimisha kuwa kwenye level ambayo eeeee full uongo umewajaaa

Hao wanaume wa eti wapo bizi bila kukusalimu au kukujibu lolote umeandika kuvutia mapenzi kati yenu... muwaogopeee hawana upendo wapo kusumbua kichwa tu. Ni imejaaaa madharauuuuuu tupu

Nakomea hapa
 
Uchoyo tu na roho mbaya ndio maana wanatafutia na majina oooh "unajiuza" ili ujisikie vibaya usiombe, mara si umuombe mzazi wako, yeye why asimuombe mzazi wake!!!
Kama kapotezea nawe mpotezee tu, mwanaume mchoyo hivyo hata mkiingia kwenye ndoa atakuwa ni tatizo tu, ndio wale wa "nyumba yang,kochi langu,tv yangu" full uchoyo na ubinafsi.
Sio uchoyo wewe, kabla ya first date ushapiga mzinga...jistukieni sometimes!!!
 
Ukiachana na hiyo first date

Ila ujue wengine wanaume wanakuwa hawana hizo pesa... au unataka wakaibe?

Labda hapo analelewa bado...
 
Siku hizi umehama kambi? Haya mambo ya kuombana hela yanakihusu chama?

Waambie Assist haijawahi kumwacha mtu salama.
Kambi sihami labda mnifukuze kama Nape kisilencer
 
Sijakuelewa kivipi? We si ukiwa na shida unataka, na mkeo akiwa nayo anakupa right? Sasa na huyu nae kapata shida akataka mpenzi wake amsaidie.
Tofautisha kati ya mke na mpenzi
 
Hayana kichwa wala miguu, mmezidi dhiki nyinyi mnaomba km vipofu mnapenda maisha yenu yaende kupitia migongo ya wanaume na hamwishi vijisababu vya kuomba hela, kuhusu wanaume kuwa ndo ssb ya michepo hilo c kweli tamaa zenu ndo ssb ya michepuko, utakuta mke wa mtu anakushobokea kwa style za aina iliyo dhahiri kuwa anakutaka kisa anataka dira aende kitchen party au send off, harusini na kwengineko, next time
Bahati nzuri mpz wangu yupo humu sijawahi kumwomba hata senti. Sio mchangiaji sana if angekuja kukupa jibu.

Btw mm sio mtoto mdogo wa kuomba hiyo buku 10 ya dira. Pamoja na umasikini wangu ila naweza kukulisha bure ugari dagaa mwaka mzima.
 
Kwani wewe msemaji wa chama!? Naona matumizi ya "sisi" badala ya "Mimi".
Matumizi ya kukupa sina ila kama ukikosa chakula njoo tule wote ugari dagaa hata mwaka sio mbaya.

Wanasema mnyime binadamu kitu chochote ila sio chakula.
 
Wenzako wanapewa bila hata ya kuomba.mwanamke ukishakuwa na tabia kama paka shume hela ya mwanaume anaejitambua utaisikia tu.
Soma vizuri comment yangu sijawahi kuomba na sitoweza.

Nilikoment hivi kwa huyu mdogo wangu wenda hakuwa na pesa ndo maana alimwomba sasa mtu iweje hajawai kumwomba, amuone Mara moja hata kama ni siku ya kukutana si angempa tuu??
 
Hope mpo poa
Jamani kwa mfano unakuwa na boyfriend na mmepanga kumeet vizuri tu baadae ikatokea kitu ukamwambia naomba unisaidie hela kwa maana kuna mtu anahitaji na mimi nipo mbali na sehemu ya kutuma hela isitoshe haujawahi kumuomba hata siku moja ni hiyo siku tu ndo imetokea ukamuomba hela......baadae unampigia simu kumwambia mambo mengine hapokei simu zako wala kukujibu text......hivi kwanini inakuwa hivi naomba kujua
We mwenyewe ulikua na yako na wala si kwamba haukuwa mahali rafiki kutuma hela!Sema tu na wewe ulikuwa na dhamira gani ili tujudge both sides!
 
Back
Top Bottom