Nani anaiongoza CCM?

Mwanakijiji,
Shida sasa hivi si kusikilizwa na wananchi. Wanaweza kuwakemea wanamtandao? Na watawasikiliza? Nadhani kwangu hilo ndilo swali muhimu.
 
Mzee ES,
Nilishawahi kusema kuwa BM is Iskariot. Tanzania hakuna kiongozi aliyetajirika kihalali. Akina EL, akina Karamagi, na sasa akina Diallo wote wametajirika kwa kuhujumu nchi. Na ndiyo maana watu wanakimbilia ubunge wa CCM (Masha) hata kama mtazamo wao haujawahi kuwa wa Ki-CCM ili nao wapate nafasi ya kujitanua.
Jasusi, viongozi waliotajirika siyo wote walijinufaisha kwa madaraka yao. Baadhi ya uliowataja walikuwa na pesa yao kabla ya kuupata uongozi.
 
Joka Kuu, swali langu haswa kwenye hii mada ni kujaribu kufikiri kama hao watu wanne uliowataja wakisimama hadharani na kusema "CCM hapa imekosea" na "kuikemea hadharani" kama alivyofanya Mwalimu wanaweza kusikilizwa na wananchi? Je wakifanya hivyo wanaweza kubadilisha mwelekeo mzima wa CCM?


Una maanisha kusikilizwa na wananchi au viongozi wa ccm?
 
Mwanakijiji,
Jibu kwa swali lako ni NDIYO. Hao wanne wakiikemea CCM hadharani basi Chama kinaweza kujirekebisha, ninaamini vilevile wananchi watawasikiliza.

Hao wengine uliwataja CCM inaweza kukaa kimya na kuwapuuza, mfano Joseph Warioba. Wengine kama Cleopa Msuya, na John Malecela, CCM yenyewe ilishawabomoa. Msuya ana "laana" ya kauli yake, "kila mtu atabeba msalaba wake", na Malecelea ana "laana" ya Baba wa Taifa.
 
Mlalahoi,

No comments.

Kwa ES, poa, nilimaanisha kuwa: watu wanakuchokoza maksudi, sometimes inabidi uelewe hivyo, wao kikandia wewe cheka tu utaona wanaacha taratibu.
Joka kuu,

Sidhani kama JM amechoka au amebomolewa (whatever term u have used), kilichopo ni kuwa wazee wengi wasio na tamaa ya kujitajirisha wanamuunga mkono. Vijana hawamuungi mkono. Ila pamoja na mapungufu yake (aliyoyaona JKN na kutuambia na ambayo sote tunayaamini ingawa hatujayathibitisha) bado ni kiongozi imara. Actually ningependa kumuona akiwa mwenyekiti wa CCM (vyeo/kofia vitenganishwe), hii ingeweza kuleta challenge kwa serikali kwa ujumla na kuwapa wapinzani changamoto, ili waache kulia kuwa serikali inawaonea!. Kuhusu Kawawa na mwinyi nadhani hawana influence kubwa, so is Kingunge na mawaziri wakuu waliopita (excl JM)

Kwa sasa chama kipo mikononi mwa Mtandao.

FD
 
Salmin sidhani kama anaweza kusikilizwa Especially kwa kile alichotaka kufanya Zanzibar nadhani naye wamemtuliza Mji mwema avue samaki tuu.
Mwinyi aka mzee jangala(from Mlimani) huyu watu wengi wataona anatania tuu na kuwa kwake nje ya ulingo wa siasa muda mrefu na kama mnakumbuka ile skandali ya kwamba alizabwa kibao na Nyerere or alifuatwa Ikulu na kufokewa ilimshushia hadhi kwenye macho ya jamii.
Malecela-Labda atumie Influence yake kwa kuwa yuko ndani ya CCM other than that laana ya Nyerere itamuandama mpaka atoke CCM.
 
JM nilishasema hana lolote, yaani ni kama maji ya mtungi. Halafu hakuna mtu anayemchokoza yeyote hapa, seems like one person is using a bunch of names.. endelea tu kujisifia mwenyewe kijana kwa kutumia majina tofauti..
 
Laiti Malecela angekuwa na influence inayodhaniwa hapa basi asingefeli kwenye majaribio yake yote (nadhani matatu kama sijakosea) ya kutaka kupitishwa kuwa mgombea urais wa CCM.Yeye mwenyewe ni majeruhi wa wanamtandao,na kama hoja ni kuwa alishiriki (au aliombwa kama wajuzi wa mambo wanavyodai) kumpigia debe Muungwana huko Songea wakati wa kampeni,hoja-pingamizi (counter-arguement) inaweza kuwa alifanya hivyo sio kwa kuombwa bali kwa kutetea ulaji wake once Muungwana akishaingia madarakani.Kwa kifupi,alishasoma dalili za nyakati.Mbona Mkapa nae alijikuta kwa shingo upande akipanda majukwaani kumpigia debe Muungwana japo yafahamiaka hakuwa chaguo lake?

Malecela ana maumivu makubwa ya harakati za uongozi ndani ya CCM.Alishajaribu ku-raise funds kutoka nje (ile stori ya Jumanne) akaangukia pua.2005 mkewe Anna Kilango alishachapisha flana kwa ajili ya "ushindi" wa mumewe.Akaishia kupigwa bao la kisigino.Ni kichekesho kusikia mtu anadai kuwa huyu mtu ana influence.Influence inamaanisha kupandikiza matakwa yako kwa watu wengine na wakayafuata.Sasa kama matakwa yake ya kutaka uongozi yamekataliwa kila anapojaribu,hiyo infleunce tunayozungumzia hapa ni ipi?

Let no one underestimate nguvu ya mtandao.Watu kama Malecela wanaweza kuwa na sauti ya namna flani ndani ya Chama (kuna watu bado wanadaiwa fadhila na Mzee huyo) lakini wanamtandao wamepenya katika kila nyanja ya maisha ya Mtanzania.Wapo kwenye taasisi za dini,za usalama,kwenye vyombo vya habari,michezoni,na hadi nje ya nchi (na wengine sasa wamepewa ofisi za kudumu nje ya nchi).

Kufupisha hoja yangu,regardless of the original connotation of the term "vigogo" hatamu za kila kitu kwa sasa nchini mwetu imeshikiliwa na wanamtandao.Rais ni mwanamtandao,as is the PM,Spika,Foreign Minister,etc.Kamati Kuu ya CCM,the most powerful organ ndani ya chama hicho imejaa wanamtandao.Sasa hiyo infuence ya Malecela (assuming bado anayo) itapenyea wapi?

Kuna mtu kasema Malecela ana laana aliyopewa na Mwalimu,mie nasema ana laana ya kuwaambia Watanzania (including wanaomtetea) "they can go to hell..." Ngoja uchaguzi upite na jina la Malecela likitajwa watu watakuwa wanauliza "John who...?"And he can go to hell too.Quid pro quo.
 
Mlalahoi.. maneno mazito na hoja zako zinaweza kupanguliwa tu kwa hoja nyingine, ili zina nguvu ya kuweza kusimama zenyewe. Sasa, labda tuulize ni nani sasa hivi ana influence ya kuweza kukionesha kidole CCM na wana CCM wakasikiliza au ndio kusema kuwa katika CCM (kama alivyosema mtu mwingine hapo juu) hakuna tena mtu mmoja mwenye influence hiyo kama alivyokuwa Mwalimu. Kwa sababu ni wazi kuwa influence ya JK sasa hivi inatokana na nafasi yake kama Rais, na hao wengine ni kwa sababu wanahusiana na yeye.

Kwa maneno mengine CCM imekuwa game kwa wote wenye uwezo!!
 
Mlalahoi

Nakubaliana na wewe mia kwa mia! pointi nzito kuliko zote ni kama angekuwa na influence angekuwa rais yeye mwenyewe, maana huyo mzee mpaka leo anautaka urais.
 
Kuingizxa majina mengi ili uonekane una point ni mufilisi wa mawazo na kuishusha heshima ya forum, Mtandao wangekuwa na hiyo nguvu basi wangechukua madaraka ya kina makamba, mwanri, na wote waliochaguliwa karibuni na muungwana mwenyewe, en angekuwa katibu wa ccm kama alivyokuwa akilalia macho,

jm ni mwanasiasa mkomavu aliyegombea urais mara mbili akashindwa, na hakuleta makelele wala kilio maana anajua kuwa siasa ni mchezo wa aina gani, na anajua kuwa kushindwa urais sio mwisho wa maisha kama wenzetu mnaotumia majina mengi mnavyotuambia, sasa ningependa kuwauliza kuwa baada ya Freeman kushindwa urais anatakiwa afanye nini aache siasa, au ajitayarishe kugombea tena?

Mzee MMJ, tunaelewa kuwa nia na madhumuni ilikuwa kubadili topic ili ile ya Zeee ipotee, goood works ila sio wote wajinga hapa, kuhusu jm ninasema kuwa ccm bado tunamuhitaji na ni majuzi tu ameendelea na ile kali yake huko tunduru ya kuisambaratisha upinzani, ccm 62%, chadema 3%, kelele za mlango hazimzuiiii kiongozi yoyote wa taifa letu kukosa usingizi, kuanzia ccm wala upinzani, Mwalimu na maneno yake yote amemuacha the man anaendela tena bado mpaka leo, na inavyoelekea ni mpaka ccm wenyewe tutakapo mwambia kuwa imetosha, na wanachi wa jimbo lake watakapo sema basi, otherwise tutaendelea kulia lia tu malecela! malecela! malecela! ccm inaendelea tu kutawala, wabongo maneno mengi ukweli hatuna wala matendo! ndio maana jamaa wataendelea kutuzia busara zao kwa shillingi millioni 100, sisi tunalia malecela!!!!! tuuuuuu!

mimi sielewi kiongozi asiyekuwa na influence anapokuwa ndiye kichwa cha habari hapa forum kila kukicha, hebu waombe maderators uone humu forum kuna ishu ngapi zinazozungumzia malecela na viongozi wengine wa taifa, au hata wa vyama vya upinzani, utashangaa mwenyewe maana ni karibu 50 against 0, lakini tunaambiwa the man sio influencial, in the last six months mzee amekuwa huko majuu karibu mara 10, between Swiss, London, na NY, hebu tuambieni kama that is the case na wastaafu wengine, maana hizi safari anazifanya kama mstaafu, na sio kama Veep wa ccm,

Ninarudia maneno niliyowahi kuyasema huko nyuma kuwa kwa mwendo huu wa wananchi na haya mawazo ninayoyaona hapa, cccm itaendelea kutawala daima kama sio milele, unajua enzi za utumwa masters walikuwa na tabia ya kuwafungia watumwa ndani ya nyumba wakati wa usiku na kuwaambia wasitoke nje, na wao masters walikuwa wakikaaa madirishani kuwasikiliza wakiongea, to their suprise watumwa walikuwa wakiongelea na kubishana sana kuwa nani kati ya masters wao ana hela zaidi ya masters wengine, na mke yupi wa masters wao aliyekuwa mzuri kuliko wake wa masters wengine, hawa watumwa hata siku walipoachiwa walikataa kabisaaa kuondoka wakidai kuwa watakufa bure na njaaa wakitoka utumwani pale!

Here we are, masikini wananchi wa bongo, Mungu aibariki tu nchi yetu! Maana kama ni kutegemea wananchi waje waigeuze nchi yetu, wananchi wenyewe ndio sisi!

kama mzee Jasusi ulivyosema "what a country"
 
Mzee Es heshima mbele mkuu. Mi naona Malecela anakuwa kichwa cha habari mara kwa mara because of how worked up you get when he negatively gets mentioned. Honestly, some of us get a kick out it on how all out you go in defending him....Lol
 
EEeh bwana I get worked up anaposemwa negatively kiongozi yoyote ninayemfahamu kuwa ni makini ndani ya bongo, ila one thing hata siku moja sitakuja ku-back away kwenye hilo,

Yaaani kutetea viongozi makini hata kama ni wa upinzani, nilisema toka BCs kuwa ni my duty, ila kwa viongozi wa cccm mpaka asubuhi ambao ninawajua kuwa ni makini na huyo mzee ni mmojawapo! yaani ccm tunamuhitaji sana bro!
 
Mzee Es,

Maneno yako yana ukweli mbali na ushabiki unaozungumzwa hapa. Ikiwa kweli Malecela hana ubavu ndani ya CCM inakuwaje yeye anavunja ma- jet kwa gharama za walipa kodi?..
Kisha tunapoteza sana muda kumjadili Malecela ambaye JK mwenyewe anampa heshima zake...maanake madaraka aliyokuwa nayo ndani ya chama, kila mwanamtandao anaitaka. Ni nafasi kubwa sana kichama na heshima yake ni kubwa...
Mimi naweza kusema malecela kairudisha hadhi yake baada ya kuondoka Nyerere na hata kuorodhesha jina lake tu ilikuwa ni jambo haliwezekani.
Ni kweli kuwa Malecela alizimwa ktk uchaguzi wa Chamwino lakini kati ya wanamtandao pia walikuwemo waliozimwa kwa sababu kiti cha Urais kina maslahi ya wengi. Influence peke yake ndani ya Mtandao haiwezi kuwa tiketi na kama tunakumbuka Mkapa mwenyewe aliwekwa pembeni (nje ya maadili ya chama) na kuambiwa mzee chaguo la watu ni huyu!..
Hata huyo RA mwenyewe akitaka urais hawezi kuupata pamoja na kwamba nyote mnasema ndiye mwenye sauti na ubavu... sauti yake na ubavu wake una sehemu yake kama vile Askari Polisi kituoni na Mwanajeshi kambini...
Jamani, mimi ningependa sana tuzungumzie watu ambao wanaweza kuleta mabadiliko, Malecela ana ubavu ama hana ni muhimu kwetu kufikiria uwezo wake tktk kuleta mabadiliko kwetu ikiwa hana nguvu basi tuzungumzie wale wenye nguvu. Kawawa, Mwinyi na Mkapa wote hawana nguvu leo hii na baadhi ya jamaa zangu wamekutana nao ktk maswala mengi tu ila majibu yao yamekuwa ushauri zaidi ya uwezo wao kufanya jambo. Kuna mabaya wanayaona lakini hawana nguvu na yawezekana wakihofia mabaya yao wenyewe!...
Kama alivyosema JK, tumwache mzee Mkapa ale pension yake, ndio ya Mwinyi, Kawawa na wengine wote hawa wankula pension yao hawana ubavu tena.
Ni akina nani wenye ubavu hilo ndio kichwa cha mada...nadhani Mwanakijiji ana lengo kuuliza swali hili.
Malecela hana OK!....who has!
 
Mkandara well put... Mzee ES.. sina sababu ya kubadilisha mada ya Zitto.. sina maslahi na kiongozi yeyote wa Tanzana na wote kwangu ni fair game! Swali alilozua Mlalahoi ni muhimu:

Kama kweli JM ana influence na ndiyo "king maker" na "power broker".. kwanini alishindwa kujitengenezea mazingira ya kushinda katika kugombea nafasi ya Urais? Mbona watu wengi walishajua tangu 1995 kuwa timu itakayomfuata BM itakuwa ni ya JK na EL (mkataba..??) Kama angekuwa na influence hiyo kubwa angeweza kubadilisha kabisa hilo. Nasubiri hoja yako mzee?
 
Nafikiri mjubu ya swali lako yako kwenye post yangu ya kwanza na ya pili, unless una maswali mapya kuhusu Makamu Wa Mwenyekiti wa CCM, DR. John Malecela, nitakusaidia, ila hilo nilishalijibu,

ila kwa nyongeza ni kwamba Makamu wetu wa ccm, aliiahidi kamati kuu ya ccm mwaka 2000, kuwa hatagombea tena urais, kwa hiyo it was a big shock hasa kwa bm alipochukua fomu mwaka 2005, pamoja na mengine yote ya mtandao ni hilo tu lililompa nguvu bm kumuondoa mapema kwenye mchujo wa wagombea,

sasa kuhusu ubavu na the rest alionao, mimi nimetoa mifano hai ya kuthibitisha msimamo wangu, so far sijasikia dtata wala facts against, zaidi tu yale yale ambayo tumezoea kuyasikia bongo ya Mwalimu, go to hell, na laana za Mwalimu, so far sijaliona jipya kama tulivyoahidiwa na na jamaa anayetumia jina lingine this time arround,

Mzee Mkandara,

Heshima mbele na nimekusikia, ninarudia kuwa kwa uelewo wangu wa cccm chama changu, maamuzi ya mwisho ya ccm toka baada ya muungwana kuwa rais, hufanywa na wao wawili na nimeweka mifano, so far siiioni majibu ya kweli zaidi ya kustarehesha baraza, isipokuwa I find it to be very interesting on wananchi wa Tanzania na what should be a national debate, na ninarudia kuwa kwa mwendo huu cccm itatawala daima, na kahuna hope kabisaaaa!
 
Mzee Es how well do you know Dr. John Malecela? Nauliza tu maana inaonekana unamjua kwelikweli huyu bwana?
Halafu nina swali jingine ambalo nimekuwa najiuliza kwa muda mrefu. Mwaka 2005 wakati wa uchaguzi na enzi za bcstimes.com, kama sikosei, ulisema kuwa uko bongo na unagombea ubunge na ukashinda. Je, bado uko mbunge, kama sivyo, je ulijiuzulu lini? Kama nimekosea kufikiri ninavyofikiri au kama kumbukumbu yangu si sahihi naomba unisahihishe.
 
Hapana nilifahamishwa siku nyingi sana na wamiliki wa forum zote ninazohusika kuwa mambo yangu binafsi ni ya kwangu na ya kwako ni ya kwako, BCS sikuwa na tatizo kusema maana kule agenda zilikuwa tofauti na hapa, baada ya tu kuingia hapa niligundua hilo, lakini still mambo yangu binafsi hayaihusu hii forum kama vile yako, halafu nafikiri unakumbuka kule BCs kuna watu walifikia kuanza kunitafuta mpaka cccm Dodoma, message Ikulu zilikuwa haiziishi, wakali wa mambo wakanibonyeza kuwa ngoma inalia mno itapasuka karibuni ndio maana nikaamua ku-tone down kidogo!

Makamu wa Mwenyekiti wa CCM, ninamfahamu sana kama ninavyowafahamu viongozi wengi wa bongo wa cccm na upinzani, na wewe unakumbuka toka BCS kuwa sijawahi kuficha hilo hata siku moja, ni majuzi tu nilikuwa ninatetea PHD ya DR. Mzindakaya, na nikasema kuwa nimewahi hata kuitembelea ranchi yake, ila sikusikia haya maswali, sasa vipi nikisema ninamjua makamu kunakuwa na tatizo? nilishasema kuwa ninamjua kwa karibu mwenyekiti wa chadema ambaye nimekua naye toka utotoni mbona hakukuwa na tatizo? Halafu pia nikasema kua hata Muuungwana ninamjua, kaborou huyo alinifundisha kule US, Lipumba alikuwa akija kila mara kwenye shule yangu US kama guest professor, yaaani mzee wangu hawa wakali ninawajua unajua kwenye maisha kuna kuzaliwa at the right time na the right the place bro!

Halafu vipi ukisema tu yanayokusumbua kuhusu mimi, badala ya kuendelea kuzunguka? sina noma bro kujibu maswali yako as long tu yanaulizwa kistaarabu! kama ulivyoanza so far! Hlalafu kumbuka kuwa hapa mahali ni pakubwa kuliko mimi, yaani ni pa mjadala wa taifa, unaweza kunitafuta kwenye pm au mtuwamel@yahoo.com
 
Back
Top Bottom