Leo najiuliza swali jepesi nikiendelea kuandika makala mpya ambayo inakusudia kwa mara nyingine kuamsha mawazo na kuchochea hisia za ndugu zangu watanzania tunapoifikiria nchi yetu. Chama cha Mapinduzi kimekuwa na vinara wake, mashabiki wake n.k Lakini ndani ya chama hicho kuna watu ambao hujulikana kama "Wazee wa Chama", "Magwiji", "Vigogo", "Vingunge" n.k Watu hawa inasemekana 'wakikohoa' wajumbe wengine wanajikwaa, na 'wakimung'unya' vikao vinatikisika. Wanachama hawa ambao wengi ni wa lile kundi la Waasisi wana ujiko wa pekee ndani ya CCM na maneno yao yanabeba uzito mkubwa wakati mwingine kushinda wa mwenyekigoda wa chama hicho! Hata hivyo najiuliza hawa magwiji au vigogo wa CCM hasa ni kina nani? Na je kweli wana uwezo bado wa kulielekeza jahazi la chama wanakotaka wao? Wana CCM kama hawa:
John Malecela
Rashid Kawawa
Jackson Makweta
Chrisant Mzindakaya
Joseph Warioba
Salim Ahmed Salim
Salmin Amour
Kingunge Ngombare Mwiru
Cleopa David Msuya
Dr. Abdalah Kigoda
Getrude Mongella
Pius Msekwa
Joseph Mungai
Brig. Gen (mstf.) Hassan Ngwilizi
Anna Makinda
Philip Marmo
Kwa kuanzia na majina hayo machache, kuna yeyote kati yao mwenye hadhi kuonekana kweli ni "kigogo" wa CCM? Kuna majina niliyoyasahau? Je watu hao bado wanaweza kukitikisa Chama cha Mapinduzi au ujiko wao umeanza kufifia kama mbalamwezi changa? Je CCM bado ina nafasi kwa watu kama hao au ndio imeshakuwa ni chama kinachoongozwa na maslahi ya watu wachache, kikiwaweka pembeni vigogo wake na hakuna mtu mwenye ubavu wa kukinyoshea kidole?
Huu muda ndo mzuri CHADEMA kujipanga kwa haya mapungufu ya CCM tunayoyaona. Wangekuwa na Mgombea mzuri wa URAIS pasingetosha lakini naona bado hawataki kufanya mabadiliko. Kwa CCM sasa hivi wanachemsha JK kimyaa!! Zitto upo!!
Aksante kwa swali lako kijana, lakini ujue kuwa watu wanaozungumza nje ya vikao vya chama wanakiuka maadili ya chama chetu. Nikiongea na mimi leo hii nitafanana na watu hao, alisema. Subiri kikao ni kesho (leo) itajulikana kama tutazungumza kuhusu watu hao ambao wanazungumza mambo ya chama nje ya vikao au kama hatutazungumza hilo. Mara tutakapomaliza kikao, katibu wa Itikadi na Uenezi, Bwana Chiligati atazungumza na waandishi.
U got it right!!!Yayumkinika kusema u-kigogo umeathiriwa na ujio wa uanamtandao.I stand to be criticized,but nadhani kila mwananmtandao mwenye wadhifa ndani ya CCM ni "kigogo wa CCM".Yayumkinika pia kusema kuwa "ukongwe" ndani ya chama hicho sio suala lenye umuhimu tena.Most probably umuhimu wa "ukongwe" ulifutika baada ya kifo cha Mwalimu.Kawawa,Malecela,Makweta,etc wamebaki kuwa figures tu lakini trendsetters ni the likes of Rostam Aziz,Mwanri,Nchimbi,etc.Mantiki ni nyepesi:katika Tanzania ya leo it's not about what you know or how long you've been in the know but rather what you have (in monetary terms) or what you know about who you know.
Malecela alikumbatia watu ambao kwa tafsiri ya zamani ndio walikuwa vigogo wa CCM eg wenyeviti wa CCM wa mikoa,nk lakini akakumbana na watu wenye jeuri ya fedha (wanamtandao) ambao kwa namna flani wametuonyesha kuwa sio kweli kuwa in every long run it's experience that counts but money does.
Yebo Yebo.. umekuja na hawa ambao tunawaita ni vigogomamboleo! Watu ambao ujiko wao kwenye CCM hautokani ni historia yao katika chama bali uwezo wao. Tatizo langu na ambalo ndilo swali langu la msingi ni je watu hao wanauwezo wa kuikemea CCM wakasikilizwa? je RA kwa uwezo wake wote wa kifedha anaweza kuwaambia CCM "jamani hapa mmepotoka" akasikilizwa?