"Kwa tunaomfahamu" huyu wa Pwani si tu anafaa kuwapo mkoani Dar Es Salaam au popote pale kama RC, bali anafaa zaidi kuwapo pale wizarani. (Ministri ov indastriz).
Mtaka pia wa Simiyu yuko njema sana, na kwa kifupi Mh. Mtaka na Mh. Eng Ndikilo, tunaweza kusema "they are more of the same''.
Kwa nafasi ya RC wa DSM, kwa maoni yangu, atafutwe tu mtu mwingine (kama kuna haja ya kufanya hivyo) na sio hao wawili kwa sababu kwa sasa, Simiyu na Pwani zinawahitaji hao wawili kuliko wakati wowote ule.
NB: Mimi bado naamini kwamba nafasi ya RC mkoani DSM bado ina mtu na mtu huyo ataendelea kuwapo hapo, hapa nimechangia tu kwa minajili ya hao ma RC wengine, kwa kadri ya "ninavyowafahamu"