GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,736
- 109,323
Kwa lugha nyingine ni kwamba badala ya kutushangaa na kututukana hadi kutudhihaki watu wa Simba SC GENTAMYCINE nikiwa kinara wao hapa JamiiForums, basi mngetupongeza! Kwani kwa 60% tumechangia kuwajaza ndimu (upepo) wachezaji wenu na wao kuamua kujitoa vile mpaka kushinda na kutinga makundi CAFCC.
Hivi mnadhani kweli GENTAMYCINE nisingekuwa nawacheka Yanga SC, nawatania hadi kuwakera huku muda mwingi nikiwasakama akina Rais Injinia Hersi Said na Msemaji Ally Kamwe wangeweza kujaa upepo na kujitoa kwa ajili ya timu?
Na kila wakikutana na wachezaji wa Yanga SC huwajaza ndimu (hasira), hali ambayo imekuwa ni kichocheo kikuu kwa wao kujituma kule na kuipambania jezi ya Yanga SC na bendera ya nchi (Tanzania).
Nasubiri sasa pongezi zenu nyingi tu kwangu kwani kuwasema kwangu nina uhakika kumechangia wachezaji wenu wote kuipambania timu hadi jana mkashinda vile, japo kwa ushindi kiduchu na wa kubahatisha kutokana na uzembe wa kipa wa Club Africaine ya nchini Tunisia.
Hivi mnadhani kweli GENTAMYCINE nisingekuwa nawacheka Yanga SC, nawatania hadi kuwakera huku muda mwingi nikiwasakama akina Rais Injinia Hersi Said na Msemaji Ally Kamwe wangeweza kujaa upepo na kujitoa kwa ajili ya timu?
Na kila wakikutana na wachezaji wa Yanga SC huwajaza ndimu (hasira), hali ambayo imekuwa ni kichocheo kikuu kwa wao kujituma kule na kuipambania jezi ya Yanga SC na bendera ya nchi (Tanzania).
Nasubiri sasa pongezi zenu nyingi tu kwangu kwani kuwasema kwangu nina uhakika kumechangia wachezaji wenu wote kuipambania timu hadi jana mkashinda vile, japo kwa ushindi kiduchu na wa kubahatisha kutokana na uzembe wa kipa wa Club Africaine ya nchini Tunisia.