Nani alikwenda shule kuchukua cheti chake akakuta amewekewa Deni ambalo halifahamu?

passion_amo1

JF-Expert Member
Dec 3, 2023
1,690
3,408
Wakuu Heshima mbele.

Juzi nilikuwa natokea PWANI nikakumbuka kwamba sikuwahi kuchukua cheti changu cha kidato cha sita. Sasa nilikuwa na mama watoto, nikamwambia sababu muda umeenda kesho unisindikize shule nikachukue cheti changu, akasema tutakwenda. Basi tulilala mjini pale na asubuhi yake mida ya saa nne nkawa naelekea shule.

Nilipofika shule nikakutana na mwalimu aliyekuwa akifundisha Jiongrafia alikuwa rafiki yangu sana.
Akaniambia Kama sura inakuja hivi inapotea, nikamwambia Mimi Passion mwalimu tulimaliza na watu fulani(nikiwa namkumbusha viongozi wa mwaka wangu)
Akasema ohoooo! sasa nimekupata

Mwalimu; na huyu dada mzuri hapa pembeni ni nani?

Mimi; Sir huyu ni Mke wangu.
Mwalimu; Hongera sana mwanangu.
Mimi; Ahsante sir.

Mke wangu; shkamoo mwalimu.
Mwalimu; marahaba, Hongereni sana japo passion alikuwa mchafu mchafu Kwa kweli umembadilisha(wote tukacheka ila mm nilicheka usoni nikaona huyu anaanza mazoea ya ovyo)

Nikamuuliza kuhusu mwalimu wa Taaluma akaniambia alihama na sasahivi ni mwalimu mkuu shule fulani, Basi nikaachana nae kuelekea ofisi ya Taaluma.

Nikafika ofisi ya Taaluma nikawasalimia walimu waliokuwepo.
Basi nikamkuta mwalimu wa Taaluma msaidizi.

Mimi; sir nina shida ya ofisi kidogo, nilimaliza mwaka fulani hapa lakini sikuwahi chukua cheti changu.

Msaidizi; sawa, unaitwa nani?
Mimi; Passion xxx xxx

Msaidizi; umekuja na leaving certificates au result slip?
Mimi; Hapana ninazo kwa mfumo wa soft.

Msaidizi; sawa nionyeshe.
Mimi; (nikatoa simu na kumuonyesha)

Msaidizi; Kwa protokali za ofisi unapaswa kuandika barua, haya njoo huku unifate.

Tukaongozana mpaka ofisi ya mkuu wa shule, nikakutana na sekretari wa mkuu wa shule, bas mwalimu akamuelekeza nikampa jina na mwaka akaingia ndani.

Sektetari; Passion xxx xxx
Mimi; yes Madam

Sekretari; Kwanini huku- clear hii clearance form yote?

Mimi; madam sikufanikiwa kukamilisha sababu nilikuwa naumwa na nilifanya mtihani nikiwa naumwa, hivyo sikufanikiwa ku- clear.

Sekretari; kutokana na clearance yako Mr Passion and your beautiful wife unadaiwa kiasi cha shilingi 245000.

Mimi; (nilamuangalia Mke wangu nikacheka na yeye akacheka) madam hilo deni limekujaje? Ninaweza kukutana na Bursar?

Sekretari; sure Mr passion.

Akachukua simu ya mezani akampgia mhasibu.

Sekretari; Passion nenda ofsini kwake, by the way you have a beautiful wife lakini hilo haliondoi uhalisia kwamba lazima ulipe deni.
Mimi; Thanks madam. I’ll be back in a minute to take my cerficate.

Nikatoka kuelekea kwa mhasibu, baada ya kufika nikaingia ofisini.

Mimi; Sir shikamoo?
Mhasibu; Marahaba karibu bwana.

Mimi; ahsante, naitwa Passion xxx xxx nimekuja hapa kuja kuchukua cheti changu nilimaliza mwaka xxxx hapa. Lakini nimekuta deni ambalo binafsi silielewi

Mhasibu; ndugu Passion ile clearance ndio inakuonyesha kwamba wewe unadaiwa kiasi gani, hapo sina cha kukusaidia unapswa kulipa. Halafu nyinyi vijana hamna shukrani, tumekutunzia cheti, tumekufundisha, umeenda kusoma huko na mpaka umeoa lakini shilingi laki 2 tu unaanza kulalamika?!

Mimi; Sir Tatizo si kulalamika, japo sina muda sana, nitalipa hilo deni niondoke na cheti changu.

Mhasibu akaniangalia usoni kuhakikisha nachoongea.

Mhasibu; okay utaipeleka pale kwa sekretari Halafu vitu vingine viendele
Mimi; kupeleka nini Sir?

Mhasibu; utapeleka hiyo pesa kwa mhasibu na utapatiwa cheti chako.
Mimi; kwani mhasibu ananidai nini? Sir ninaomba Akaunti namba ya shule nilipe hiyo pesa hapa.

Akaniambia nsubiri hapa, akanyanyuka kutoka ofisini na mimi nikatoka kumfata. Nikawaona wanateta na sekretari kwa sauti ya chini.

Mhasibu; sasa kwa sasa hatuwezi kupokea kwa mfumo wa kibenki kutumia akaunti namba ya shule, sababu ya wanafunzi waliomaliza kipindi cha zaidi ya miaka MItano

Nikafikiri yale maneno yake nikaona hata mtoto asingeyakubali.
Mimi; Sir mimi sitalipa pesa kwa kumpa mtu hela mkononi. Ninadaiwa na shule na si mtu, hivyo nitalipa pesa yote hapa kwa akaunti namba ya shule.

Bursar akaniita pembeni sababu nilikuwa na Mke wangu karibu.

Mhasibu; sasa Mr passion sikia wewe fanya ulipe deni, Kwanini usilipe in cash sababu sasahiv hata ada imeondolewa hivyo unapswa kulipia.

Kiukweli siwasemi walimu ila binafsi naona wanapitia wakati mgumu, maana saa nne wanakunywa chai wanaletewa na mihogo ya kuchemsha.

Mimi; Sir mimi nitalipa hiyo pesa kwa akaunti namba ya shule(nikamuita Mke wangu anipe simu yangu ili nilipie lakini uhalisia hiyo pesa nilikuwa siwezi kulipa ila niligundua wanahitaji pesa)
Mhasibu; Sawa Basi ngoja nijaribu kuongea na sekretari tuone tunafanya vipi.

Baada ya kama dakika 10 walitoka pale wakiwa na cheti changu.

Mhasibu; Passion hichi hapa cheti chako.
Mimi; mwalimu Ahsanteni sana( nikaingia mfukoni nikakunja elf10 nne nikampatia mkononi)
Mhasibu; Ahsante sana mwanangu.

Nilichogundua ukienda shule walimu wakikuona umevaa umependeza, umenenepa, umeenda na gari magari yenyewe si yetu ya baba mkwe wanaona una pesa kumbe bado tunapambana.

Nani alikutana na kisanga kipindi anaenda kuchukua cheti.l chake shule?
 
Pugu sekondari hapo nilienda kwa mtaaluma akaleta tamaa oohhh unadaiwa sijui 80k ......nikaachana nae nikapanda kwa second master ambako ndiko vyeti vinatoka kule nikatoa 15k shughuli picha likaishia hapo nakipewa chet changu easy nashuka chini nakutana na yule madam wa taaluma ananitolea mimacho.
 
Mimi pia nilikuta nina sehemu sijaclear...aliekuwa academic akaniuliza hapa mbona hukuclear sikuwa na jibu. Baadae akaona anipe tu cheti sikuombwa hata kumi.....
 
nlikuwa nadaiwa lakin kwakuwa performance yangu ilikuwa nzuri mkuu wa shule akanipa bure tu..., kuna jamaa nlikuwa nae pia alikuja kufuata chet yeye alinyimwa akaambiwa akalipe deni kwanza
 
Mwalimu mmoja wa GS akasema tumeiba kitabu tulipe 25,000 kila mtu lasivyo hamna cheti wala leaving. Wanafunzi wa EGM, PGM na PCM wote alikuwa anatufundisha kwa pamoja imagine hicho kitita, kisa tu alikuwa akiingia kwenye kipindi watu hawatokei class akaona tunadharau somo lake. Ukiacha kitabu chake (ambacho alisema tumeiba) alikuwa ametugawia vitabu vya kuazima vile, basi mjuba nikapiga hesabu zangu nikasepa nacho kile cha kuazima sikurudisha na sikuchukua leaving, nikasubiri vyeti vimetoka nikafata nikaenda na kile kitabu mpaka kwa Head master nikamwambia nilisahau nikaondoka nacho, yeye akajua ndio kile watu walilipishwa 25,000 akanipa vyangu, kumbe yule mwalimu kaniona akaja mbio kumweleza HM, mie nna vitu vyangu HM akacheka tu akasema dogo ana bahati muache tu. Wasichojua niliplan kabla hata ya kufanya clearance kuwa nasepa nacho ntakileta vyeti vikitoka na watajua ndio kilichopotea kumbe sio. Yule mwalimu alikuwa adui yangu sana na alishajaribu kuhakikisha napewa adhabu kali kwa kutoonekana darasani mda wa vipindi so nilisema hali pesa yangu na atajua hajui.
 
Nilienda nikakuta deni la 230,000/= nikalikataa, nikaamua kurudi maana sikuwa na haraka nacho.

Likapita zoezi la uhakiki wa vyeti aka kuwatumbua wenye vyeti feki. Nikalazimika kurudi kukichukua kwa gharama za safari sh. 60,000/=, nikalipia deni 230,000/=, na bado jamaa wa masijala akanitoa sh. 20,000/= za kukitafuta, maarufu kama za maziwa ya kusafishia vumbi. Nilijuta kukiacha mara ile ya kwanza!
 
Nilienda after 8 years na sikulipishwa chochote. Nilikwenda na leaving certificate. Ila chuo ndiko nilinyooshwa, deni la milioni hata sijui lilitoka wapi🙆🙆🙆
 
Wakuu Heshima mbele.

Juzi nilikuwa natokea PWANI nikakumbuka kwamba sikuwahi kuchukua cheti changu cha kidato cha sita. Sasa nilikuwa na mama watoto, nikamwambia sababu muda umeenda kesho unisindikize shule nikachukue cheti changu, akasema tutakwenda. Basi tulilala mjini pale na asubuhi yake mida ya saa nne nkawa naelekea shule.

Nilipofika shule nikakutana na mwalimu aliyekuwa akifundisha Jiongrafia alikuwa rafiki yangu sana.
Akaniambia Kama sura inakuja hivi inapotea, nikamwambia Mimi Passion mwalimu tulimaliza na watu fulani(nikiwa namkumbusha viongozi wa mwaka wangu)
Akasema ohoooo! sasa nimekupata

Mwalimu; na huyu dada mzuri hapa pembeni ni nani?

Mimi; Sir huyu ni Mke wangu.
Mwalimu; Hongera sana mwanangu.
Mimi; Ahsante sir.

Mke wangu; shkamoo mwalimu.
Mwalimu; marahaba, Hongereni sana japo passion alikuwa mchafu mchafu Kwa kweli umembadilisha(wote tukacheka ila mm nilicheka usoni nikaona huyu anaanza mazoea ya ovyo)

Nikamuuliza kuhusu mwalimu wa Taaluma akaniambia alihama na sasahivi ni mwalimu mkuu shule fulani, Basi nikaachana nae kuelekea ofisi ya Taaluma.

Nikafika ofisi ya Taaluma nikawasalimia walimu waliokuwepo.
Basi nikamkuta mwalimu wa Taaluma msaidizi.

Mimi; sir nina shida ya ofisi kidogo, nilimaliza mwaka fulani hapa lakini sikuwahi chukua cheti changu.

Msaidizi; sawa, unaitwa nani?
Mimi; Passion xxx xxx

Msaidizi; umekuja na leaving certificates au result slip?
Mimi; Hapana ninazo kwa mfumo wa soft.

Msaidizi; sawa nionyeshe.
Mimi; (nikatoa simu na kumuonyesha)

Msaidizi; Kwa protokali za ofisi unapaswa kuandika barua, haya njoo huku unifate.

Tukaongozana mpaka ofisi ya mkuu wa shule, nikakutana na sekretari wa mkuu wa shule, bas mwalimu akamuelekeza nikampa jina na mwaka akaingia ndani.

Sektetari; Passion xxx xxx
Mimi; yes Madam

Sekretari; Kwanini huku- clear hii clearance form yote?

Mimi; madam sikufanikiwa kukamilisha sababu nilikuwa naumwa na nilifanya mtihani nikiwa naumwa, hivyo sikufanikiwa ku- clear.

Sekretari; kutokana na clearance yako Mr Passion and your beautiful wife unadaiwa kiasi cha shilingi 245000.

Mimi; (nilamuangalia Mke wangu nikacheka na yeye akacheka) madam hilo deni limekujaje? Ninaweza kukutana na Bursar?

Sekretari; sure Mr passion.

Akachukua simu ya mezani akampgia mhasibu.

Sekretari; Passion nenda ofsini kwake, by the way you have a beautiful wife lakini hilo haliondoi uhalisia kwamba lazima ulipe deni.
Mimi; Thanks madam. I’ll be back in a minute to take my cerficate.

Nikatoka kuelekea kwa mhasibu, baada ya kufika nikaingia ofisini.

Mimi; Sir shikamoo?
Mhasibu; Marahaba karibu bwana.

Mimi; ahsante, naitwa Passion xxx xxx nimekuja hapa kuja kuchukua cheti changu nilimaliza mwaka xxxx hapa. Lakini nimekuta deni ambalo binafsi silielewi

Mhasibu; ndugu Passion ile clearance ndio inakuonyesha kwamba wewe unadaiwa kiasi gani, hapo sina cha kukusaidia unapswa kulipa. Halafu nyinyi vijana hamna shukrani, tumekutunzia cheti, tumekufundisha, umeenda kusoma huko na mpaka umeoa lakini shilingi laki 2 tu unaanza kulalamika?!

Mimi; Sir Tatizo si kulalamika, japo sina muda sana, nitalipa hilo deni niondoke na cheti changu.

Mhasibu akaniangalia usoni kuhakikisha nachoongea.

Mhasibu; okay utaipeleka pale kwa sekretari Halafu vitu vingine viendele
Mimi; kupeleka nini Sir?

Mhasibu; utapeleka hiyo pesa kwa mhasibu na utapatiwa cheti chako.
Mimi; kwani mhasibu ananidai nini? Sir ninaomba Akaunti namba ya shule nilipe hiyo pesa hapa.

Akaniambia nsubiri hapa, akanyanyuka kutoka ofisini na mimi nikatoka kumfata. Nikawaona wanateta na sekretari kwa sauti ya chini.

Mhasibu; sasa kwa sasa hatuwezi kupokea kwa mfumo wa kibenki kutumia akaunti namba ya shule, sababu ya wanafunzi waliomaliza kipindi cha zaidi ya miaka MItano

Nikafikiri yale maneno yake nikaona hata mtoto asingeyakubali.
Mimi; Sir mimi sitalipa pesa kwa kumpa mtu hela mkononi. Ninadaiwa na shule na si mtu, hivyo nitalipa pesa yote hapa kwa akaunti namba ya shule.

Bursar akaniita pembeni sababu nilikuwa na Mke wangu karibu.

Mhasibu; sasa Mr passion sikia wewe fanya ulipe deni, Kwanini usilipe in cash sababu sasahiv hata ada imeondolewa hivyo unapswa kulipia.

Kiukweli siwasemi walimu ila binafsi naona wanapitia wakati mgumu, maana saa nne wanakunywa chai wanaletewa na mihogo ya kuchemsha.

Mimi; Sir mimi nitalipa hiyo pesa kwa akaunti namba ya shule(nikamuita Mke wangu anipe simu yangu ili nilipie lakini uhalisia hiyo pesa nilikuwa siwezi kulipa ila niligundua wanahitaji pesa)
Mhasibu; Sawa Basi ngoja nijaribu kuongea na sekretari tuone tunafanya vipi.

Baada ya kama dakika 10 walitoka pale wakiwa na cheti changu.

Mhasibu; Passion hichi hapa cheti chako.
Mimi; mwalimu Ahsanteni sana( nikaingia mfukoni nikakunja elf10 nne nikampatia mkononi)
Mhasibu; Ahsante sana mwanangu.

Nilichogundua ukienda shule walimu wakikuona umevaa umependeza, umenenepa, umeenda na gari magari yenyewe si yetu ya baba mkwe wanaona una pesa kumbe bado tunapambana.

Nani alikutana na kisanga kipindi anaenda kuchukua cheti.l chake shule?
Kwahiyo ukapewa cheti bila kulipa "sentano"?
Ila hapo kwenye kusema walimu wana wakati mgumu kisa tu uliona wanaletewa mihogo wakati wa chai, umezingua!
 
Back
Top Bottom