Nyota njema ilianza kuonekana mapema kwa rafiki yangu .

passion_amo1

JF-Expert Member
Dec 3, 2023
1,578
3,148
Ndugu zangu wana JF nafikiri wengi tulipata kusikia Msemo wa nyota njema huanza kuonekana mapema.

Siku za nyuma kidogo nilileta uzi nilivyokutana na mwalimu wangu m- polish alikuwa akinifundisha biblia, sasa pale shuleni nilikuwa na rafiki tulikuwa tunafananishwa sura kasoro tu yeye alinizidi weupe kiasi.

Rafiki yangu huyu yeye harakati alizianza shule mapema sana, alikuwa anaondoka shule kwa kutoroka mara nyingi siku za jumapili. Muda ambao tunajiandaa kuingia church kwa ajili ya service(huduma) yeye alikuwa anapitia kwenye miti mingi iliyopandwa pembeni ya mabweni na kuingia katika mashamba ya mahindi na kuanza safari ya kwenda mjini.

Pili, alikuwa yupo ontime yaani nakumbuka service ilikuwa inaisha saa4, saa 3:40 mpaka 45 tayari alishafika maeneo ya shule anasubiri tuanze kutoka na yeye anatokea kwenye mashamba na kujiunga nasi kujiandaa kwa ajili ya chai(breakfast).

siku moja mwalimu wetu mkenya na yeye Alikuwa amenikariri sana sababu mara nyingi kwenye kipindi chake cha biblia tulikuwa tunagombana na ananitoa nje.

Alikutana na rafiki yangu huyo mjini, maana alikuwa akienda anatuletea mikate, sausage(soseji) na alikuwa ana kiredio chake tukitaka kusikiliza mziki anatuambia tuchangie pesa.
Basi tunajichanga tunampa tunasikiliza, na akituletea hivyo vitu anatuuzia kwa bei ya juu. Hiyo siku akamkimbia madam alivyorudi ule msala ukaniangukia mimi nikapewa adhabu ya kusafisha vyoo wiki nzima mbali na juhudi za kujitetea.


Kitu alichokuwa akikipenda ni magari, yaani ilikuwa ikija suala la magari huwezi kumwambia kitu.

Siku moja nakumbuka tukiwa paredi mkuu wa shule alikuwa anatoka kwake ndani ya shule humo humo anakuja ofisini, sasa alipofika karibia na madarasa ambayo gari ikawa imezima, mkuu akawa anaongea na simu apate mtu wa kumtengenezea akilalamika tangu jana inazima, jamaa akatoka nyuma akasema SIR hilo tatizo ni dogo ngoja nije kukurekebishia basi wote tukageuka kumwangalia hapo tupo form two.
Akafika kwa mkuu pale akafungua bonet akaingia ndani akawa anaiwasha inazima baada ya muda wa kushikashika pale kwenye boneti akarudi kuwasha kitu kikawaka.

Basi tangu hapo fundi magari, Fundi magari ndo likawa jina lake, na stori zake zote akawa anasema hakuna biashara inayolipa kama masuala ya spare.

Tangu tulivyomaliza shule Tuapoteana, nikaja kuonaga post zake amepiga kwenye duka amekalia kiti pembeni kuna matairi.
Nikaanza kumtafuta, tukawa tunaongea tu kawaida kila mtu akiendelea na mishe zake na akaniambia siku nkipata muda tutaonana ndugu yangu passion.

Jana jumapili mara zote napumzika nikashangaa namba ngeni, baada ya kupokea.

Mimi; Haloo nani?

JD; pacha wako
Mimi; nilivyosikia sauti tu nikajua huyu ni JD, daah pacha za siku nyingi? Hata hatuonani hapa hapa dar?
JD; Mimi mbona nipo passion, majukumu tu yanatubeba.
Mimi; kweli kaka, maisha yanasemaje?
JD; mdogo mdogo tu, kesho jtatu kama una muda nitakuwa kariakoo mida ya mchana unicheki.
Mimi; pacha hilo halina shida nitakucheki, akakata simu.

Leo sasa baada ya kutoka naelekea kusubiri treni nikiwaza namna TT wanavyozingua na walivyoniudhi wiki ile. Nikaondoka mpaka kazini, mchana nikamcheki akaniambia mtaa aliopo ikabidi nimuache Mke wangu nimuage nitoke.

Nikaenda mpaka kule, daah kanenepa sana nikasema kweli pesa hazimkatai mtu. Tukasalimiana pale nikamuacha amalizane na wahindi wale wa spare baadae tukavuka nga’mbo sehemu ya parking nikamuona anawasha Harrier, miguu ikaisha nguvu nikajisemea moyoni rafiki yangu huyu si level zangu tena.

Basi kwenye gari stori za hapa na pale, huku nikimdadisi, niseme tu kama kuna watu mpo na marafiki waliofanikiwa zaidi yenu utaona hata mentality yake imebadilika ndio maana huwa wanabadilisha marafiki kabisa.
Basi safari mpaka kigamboni mji mwema kwa mbele. Tumefika pale kwenye buti alikuwa ameweka perfume na android akazitoa tukaingia ndani akaniambia passion karibu nyumbani, nikamuuliza kaka hapa ni kwako? Akasema ndio karibu sana daah nilimpa hongera sana ila nilijiona mnyonge sana.

Nyumba ni nzuri kiasi lakini ni maendeleo makubwa sana kapiga huyu rafiki yangu, basi muda kama masaa mawili tukatoka akanipeleka dukani kwake kigamboni daah nikasema kaka hongera sana kweli ulichokuwa unafanya shule ndio hichi unachokiishi sasa.

Ni rafiki yako yupi ambaye ushakutana naye amepiga hatua kubwa Sana kimaendeleo?
Japo wengine huwa wakitoboa wanatusahau wenzao ambao bado hatujafika level zao.

Kila kitu kinawezekana nimejifunza.
 
Mpaji sema wapo wazazi wenye uwezo huo, km yule dgo wa scott pizza baba yake alimnunulia gari kipind anamlza fom4 ndio akaliuza kuongezea mtaji wa kfungua scott
Hata nampinga bas! Ila hlo nakubaliana na ww Kuna watu lile andiko la kula kwa jasho haliwahusu ila alichokisema huyu Mwenyekiti mstaafu wa Ukwata Arusha Sec Mshamba hachekwi na wasi wasi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom