kataza
Member
- Sep 5, 2014
- 20
- 50
Hello ladies and gentlemen,
Katika maisha ya shule kuna visa na mikasa mingi sana tupe kisa chako.
Changu mimi ni;
Kuna siku tulichelewa kurudi shule kulikuwa na ile ratiba ya unatoka shule saa sita then unarudi saa saba kasoro. Sasa mimi nilipoenda home bi mkubwa ndio kwanza anabandika mboga dah, nikaanza msaidia kupika nikachelewa.
Sasa nafika shule nakuta shule nzima ipo kimyaaaaaaa, nikaona sio kesi ngoja niambae na korongo then nitokee class kwa nyuma.
Sasa nimeambaa na korongo ile natokeza tu ghafla teacher on duty huyu hapa, dah akaniita we fulani nimekuona njoo hapa then nifuate ofisi ya nidhamu. Dah, ticha mnoko kinoma, sasa tumefika ofisini nikajua nikiingia tu ni stiki tu so nikaacha atangulie then nikafunga mlango kwa nje nikasepa class.
Sasa kumbe nyuma ticha kaita sana msaada lakini wapi, maana ofisi ilikuwa imejitenga kidogo but anakuja kufunguliwa mlango muda ushaenda kama saa tisa hivi. Ghafla kengele ikagongwa na mimi nikasepa zangu home muda huohuo. Dah, assembly natangazwa popote nilipo nijisalimishe na wanafunzi wanoko wakatumwa waje home.
Maisha haya, kesho yake nikaenda na namba nikawahi nikaulizwa kwanini ulimfungia mwalimu, nikasema sio mimi maana jana sikuja shule, dah sir ...... Mungu anakuona huko ulipo.
Tililika yako.
Sent from my SM-A145F using JamiiForums mobile app
Katika maisha ya shule kuna visa na mikasa mingi sana tupe kisa chako.
Changu mimi ni;
Kuna siku tulichelewa kurudi shule kulikuwa na ile ratiba ya unatoka shule saa sita then unarudi saa saba kasoro. Sasa mimi nilipoenda home bi mkubwa ndio kwanza anabandika mboga dah, nikaanza msaidia kupika nikachelewa.
Sasa nafika shule nakuta shule nzima ipo kimyaaaaaaa, nikaona sio kesi ngoja niambae na korongo then nitokee class kwa nyuma.
Sasa nimeambaa na korongo ile natokeza tu ghafla teacher on duty huyu hapa, dah akaniita we fulani nimekuona njoo hapa then nifuate ofisi ya nidhamu. Dah, ticha mnoko kinoma, sasa tumefika ofisini nikajua nikiingia tu ni stiki tu so nikaacha atangulie then nikafunga mlango kwa nje nikasepa class.
Sasa kumbe nyuma ticha kaita sana msaada lakini wapi, maana ofisi ilikuwa imejitenga kidogo but anakuja kufunguliwa mlango muda ushaenda kama saa tisa hivi. Ghafla kengele ikagongwa na mimi nikasepa zangu home muda huohuo. Dah, assembly natangazwa popote nilipo nijisalimishe na wanafunzi wanoko wakatumwa waje home.
Maisha haya, kesho yake nikaenda na namba nikawahi nikaulizwa kwanini ulimfungia mwalimu, nikasema sio mimi maana jana sikuja shule, dah sir ...... Mungu anakuona huko ulipo.
Tililika yako.
Sent from my SM-A145F using JamiiForums mobile app