Nani aliagiza na waliohusika kumshambulia Tundu Lisu? Serikali itoe kauli au ifunge jalada

Kuna shahidi yoyote wa hilo tukio mkuu aliyekueleza alichokiona hadi sasa?
Inawezekana ndio maana wanasema muhusika wa ushahidi ni tundu mwenyewe na associates wake. Hii kesi haina hata mpita njia anayefahamu kilichotokea.
Au mimi ndio sijui?
-Lissu amesema muhusika ni Jiwe, ukimya/kigugumizi cha serikali kukanusha wanamlinda nani?
-Footages za CCTV cameras huwa zinabaki kwenye severs hivyo kung'oa cameras si kikwazo cha footages kutokupatikana. Polisi kwa nini wanakalia kimya suala la hizo footages ambazo ndiyo kielelezo kisicho na longolongo?
 
Na kumbuka.mchezo wa kuchezea katiba na chaguzi vimegharimu maisha ya wengi. Akwilina aliuawa akiwa siyo mshiriki wa maandamano.

Aliyesababisha maandamano sasa ndo boss Tume ya Uchaguzi. Je unadhani haya ni bahati mbaya?
Bas hatuna la kusema mkuu
 
Camera za CCTV eneo la tukio ndiyo msema kweli.

Kuna nini hadi zitolewe baada ya tukio?
Hata kama waling'oa zile CCTV cameras lakini footages huwa zinakuwepo kwenye severs, cameras huchukua footages na kuzirekodi.
Kwanini polisi(hasa awamu ya Jiwe) walizificha? Walikuwa wakimlinda nani? Je inawezekana waliziharibu kabisa kuficha/kuharibu ushahidi?
 
Hata kama waling'oa zile CCTV cameras lakini footages huwa zinakuwepo kwenye severs, cameras huchukua footages na kuzirekodi.
Kwanini polisi(hasa awamu ya Jiwe) walizificha? Walikuwa wakimlinda nani? Je inawezekana waliziharibu kabisa kuficha/kuharibu ushahidi?
Tangu miaka ya 2000 inaanza ninajua uwepo wa softwares za kuretrive deleted data. Hata ukiiformat server mara kumi bado data zote zilizokuwepo zinaweza kuwa reatored.

Nini kinazuria utaalam wa kurudisha data kutumika ili ku unveil ukweli?
 
Kwa mujibu wa yanayoendelea nchini sasa ni kwamba wananchi wengi hawaamini kauli nyingi za serikali hususani zinazotolewa na Jeshi la Polisi kuhusu masuala ama matukio ya kinyama waliyofanyiwa upinzani.

TUndu Antipas Lisu ni Mtanzania anayestahili haki zote za kikatiba na kisheria. Haki yake ya kuishi iliingia majaribuni baada ya tukio la kinyama dhidi yake lililomlazimu kukimbia nchi huku akiwa anapatiwa matibabu.

Tumemsikia akisema waziwazi kuwa mkuu wa awamu ya Tano ndiye aliyeamuru kushambuliwa kwake kwa lengo la kutoa uhai wake. Mpaka sasa ninavyoandika hapa hakuna mtuhumiwa yeyote aliyehojiwa wala kushtakiwa kwa tukio hilo la unyama wa mchana kweupe.

IGP mstaafu alisema kuwa mwenye ushahidi tosha ni mtendewa yaani Lisu. Hivyo anatuaminisha kuwa endapo Lissu angekufa basi case ingekuwa closed kitambo. Tumejulishwa na wasamaria wema kuwa CCTV kamera zilizorekodi tukio ziliondolewa mara baada ya tukio.

Ni jambo gani linaloipa serikali kigugumizi kuchunguza na kuchukua hatua dhidi ya walioitia doa baya sana nchi kwa tukio lile?

JPM ni mwaka wa pili sasa hayupo na hana amri ya kuzuia uchunguzi. Je tunapaswa kuendelea kuamini kuwa aliamrisha yale yaliyotokea? Kuna uzito gani kumpatia Tundu Lisu haki yake kwa kuwahoji na kuwashtaki waliohusika na shambulizi lile?
Lisu na Mbowe ilibidi hii ndiyo iwe agenda ya kwanza kwenye huu upatanishi. Mkuu wa nchi yupo na wahujumiwa (Lisu na Chadema) mpo, this was the first issue to be raised otherwise you are taking us for granted !
 
Tangu miaka ya 2000 inaanza ninajua uwepo wa softwares za kuretrive deleted data. Hata ukiiformat server mara kumi bado data zote zilizokuwepo zinaweza kuwa reatored.

Nini kinazuria utaalam wa kurudisha data kutumika ili ku unveil ukweli

ipo siku itaeleweka
saSA kuna AI it is a far advanced tech
 
Back
Top Bottom