Namuunga mkono Ray C kwa anachofanya Shigongo kwake

Namuunga mkono Ray C kwa anachofanya Shigongo kwake

Wamajanga

Senior Member
Joined
Jun 24, 2014
Posts
133
Reaction score
47
Niliangalia mahojiano aliyokuwa anafanyiwa msanii wa muziki wa kizazi kipya Rehema Chalamila maarufu kama Ray C alikuwa anamlalamikia mmiliki wa kampuni ya Global Publisher Bw Erick James Shigongo kwamba magazeti yake yanamfanya aishi maisha ya tabu kwa kuwa anajitahidi kuacha madawa lakini magazeti yake yanaandika anaendelea kutumia hay madawa ya kulevya kwa hiyo yanamvunja nguvu yeye na yanampa presha mama yake mzazi.
Ukiangalia ni kweli mana yeye mwenyewe Shigongo anasema anatetea vijana katika nyanja mbalimbali za kujikwamua katika umasikini lakini kwa mambo anayomfanyia Ray C kama kijana ni kama kumuharibia maisha yake Ray C na tena kama mmojawapo wa vijana.
Aache kumuandama ili maisha yake yarudi kama zamani.
 
Huyo rehema anahitaji kuwajibika kwa ajili yake mwenyewe. You are not who they say you are. Yeye amdhihirishie mama yake kuwa ameacha na ahakikishe dua la shigongo halimpati. Shigongo anamvunja moyo akiwa kama nani wake?
 
Huyu Ray C anatafuta huruma za umma..amesahau alivyokuwa akiwatukana Watanzania wenzake alipokuwa Mombasa
 
Huyu shigongo hajielewi anadai mlokole lakini magazeti yake ni umbeya mtupu na machombezo ya kishetani ndio yanamuweka mjini
 
Ray c kaongea point na anahusika kuwaharibu vijana kwa habali zake za uongo
 
hayo magazeti ndo ya wanaume wa dar wanaojalidili maisha ya wemasepetu saiv ana mpododo mkubwa.
gazeti lenyewe lina ukurasa 6 tu eti limeisha nawashanga sana wanao nunuaga hayo magazeti ya vyanzo ya habari visivo sibitishwa kama ni kweli?
 
Unajua nini, watumiaji madawa siku zote huwa hawakubali. Lakini ninachoupendea unga huwa haukopeshi lazima ukuumbue, kwa hiyo mwache tu akanushe iko siku atakimbilia tena msoga
 
Erick Shigongo anajitangaza ni Mlokole na kila mara neno Yesu halimtoki mdomoni lakin matendo yake ni mushkel mkubwa.


Walokole (baadhi) ni wanafki wa kutupwa

wengi wao ni wazinzi, wanafki, washirikina na wadhulumati

mwimbaji wao yule mkubwa ana kesi lundo la utapeli

mchungaji wao yule mwingine kavunja ndoa ya kondoo wake yaani vurugu mechi
 
Niliangalia mahojiano aliyokuwa anafanyiwa msanii wa muziki wa kizazi kipya Rehema Chalamila maarufu kama Ray C alikuwa anamlalamikia mmiliki wa kampuni ya Global Publisher Bw Erick James Shigongo kwamba magazeti yake yanamfanya aishi maisha ya tabu kwa kuwa anajitahidi kuacha madawa lakini magazeti yake yanaandika anaendelea kutumia hay madawa ya kulevya kwa hiyo yanamvunja nguvu yeye na yanampa presha mama yake mzazi.
Ukiangalia ni kweli mana yeye mwenyewe Shigongo anasema anatetea vijana katika nyanja mbalimbali za kujikwamua katika umasikini lakini kwa mambo anayomfanyia Ray C kama kijana ni kama kumuharibia maisha yake Ray C na tena kama mmojawapo wa vijana.
Aache kumuandama ili maisha yake yarudi kama zamani.
Ray C anasema "Anajitahidi kuacha madawa" kumbe bado anavuta?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom