goroko77
JF-Expert Member
- Jul 9, 2019
- 8,855
- 12,984
Mtaa ganinhuo mkuu2016 kitaani kwetu kulizuka huu upumbavu wa hivi vitoto tena bado vinanuka maziwa kabisa, vimejiunga kundi kama la watoto 30 hivi mchana kutwa ni kuvuta bangi halafu usiku vinaingia kitaani kufanya matukio.
Vilibahatika kupiga matukio kwenye nyumba kama 3 hivi, vikawacharanga mapanga wenye nyumba na kuchukua pesa, simu, tv na vitu vingine vidogo vidogo.
Wanaume tukakaa chini kujadili eti watu wanadai tupeane zamu ya kulinda usiku (Sungusungu)
Katika huo mjadala tulikuwepo watu kama wanne tukapinga kabisa suala la kupeana zamu ya kulinda, yaani vitoto vya darasa la saba kweli vituzuie wanaume tusilale usiku?
huo tuliona ni zaidi ya upumbavu, yaani mchana kutwa tunashinda kazini halafu inafika usiku tusipumzike kisa hivi vikinda vilivyokosa malezi.
Tuliitisha kikao na wananchi wote kitaani na kutoa onyo kwa wazazi wawakanye hao panya wao ili mbele ya safari tusije kulaumiana.
Katika kikao wananchi wakawa wanataja majina ya hao watoto wanaojihusisha na huo uhalifu, tukapata orodha ya majina kama 17 hivi ya watoto tunaowajua kabisa hapo mtaani kwetu na wazazi wengine kukiri kabisa kua watoto wao wamekua na mienendo ya hovyohovyo.
Siku ya pili baada ya kile kikao panya road wakatuma salamu kwa kumvamia kiongozi mmoja wa dini hapo kitaani kwetu wakamcharanga kidogo mapanga halafu wakaiba walivyoiba na kutokomea.
Asubuhi kumekucha baada ya taarifa kuenea tukaona huu ndio wakati muafaka sasa wa kuanza kuwawajibisha hawa watoto wanaoanza kuota mapembe,
pitia katika yale majina tukaanza kuingia nyumba kwa nyumba tukabahatika kuwadaka madogo wawili, tukawafinya haswa haswa wakakiri wenyewe walihusika kwenye tukio la jana na wakataja majina ya wenzao, baada ya kumaliza kutaja majina wananchi wenye hasira kali wakaanza kutembezea mapanga na matofali kisha wakamalizia na kidumu cha petrol.
Ukaanza msako wa majina yaliyobakia jioni akamdakwa dogo mwingine, nae akafanyiwa vilevile kama walivyofinyiwa wale wenzake wawili.
Wazazi waliowapenda watoto wao baada ya kuona wananchi tumeamua kua serious faster wakawakimbiza mikoani ili kukwepa hukumu ya wanachi wenye hasira kali.
Zile sura kwenye ile orodha yetu tulikaa zaidi ya mwaka hatukuziona tena mtaani, na hua ndio ukawa mwisho wa upumbavu wa aina yoyote hapa mtaani kwetu.
Kikubwa hawa madogo ni kuwachekea chekea ndio wanajifanya manunda ila wananchi wenyewe wakiamua kua serious huu upumbavu hauwezi kuwepo kwenye jamii yoyote.