Resilience
JF-Expert Member
- Jan 4, 2023
- 877
- 4,105
Kuna jamaa yangu kavamiwa jana huko maeneo ya Kinyerezi na kundi la vibaka wakamsachi na kuchukua kila alichokuwa nacho. Anachoshukuru ni kwamba amefanikiwa kuondoka akiwa mzima wa afya na sasa yupo njiani kurejea Mwanza. Naongea naye ananiambia kwa idadi ya vijana waliomvamia aliona kifo kimekaribia; kila akikaa anashtuka akidhani wanamvamia upya aaaaahaaa. Omba yasikukute.
Naamini Kamanda Mlilo Jumanne ataangaika na hawa wajinga wajinga wasiofanya kazi wanaotamani kula bila jasho. Soon nategemea kusikia jambo kutoka kwa Mzee Mlilo ili sisi tunapotegemea kuuza samaki tuwe free kuja kula maisha mwisho wa mwaka jijini huko.
Lakini pia Nimwombe Mzee Mlilo aongeze nguvu kwenye ufuatiliaji wa vifaa kama simu na laptop zinazoibiwa. Zitasaidia sana kukamata huu mtandao. Huyu ndugu yangu kaibiwa simu na laptop ila aliporipoti polisi nadhani wao siyo issue serious sana kuifanyia kazi.
Tukiwekeza kufuatilia simu zilizopotea tutapata wahalifu wengi sana na kuwaadhibu kwa makosa wanayotenda
Naamini Kamanda Mlilo Jumanne ataangaika na hawa wajinga wajinga wasiofanya kazi wanaotamani kula bila jasho. Soon nategemea kusikia jambo kutoka kwa Mzee Mlilo ili sisi tunapotegemea kuuza samaki tuwe free kuja kula maisha mwisho wa mwaka jijini huko.
Lakini pia Nimwombe Mzee Mlilo aongeze nguvu kwenye ufuatiliaji wa vifaa kama simu na laptop zinazoibiwa. Zitasaidia sana kukamata huu mtandao. Huyu ndugu yangu kaibiwa simu na laptop ila aliporipoti polisi nadhani wao siyo issue serious sana kuifanyia kazi.
Tukiwekeza kufuatilia simu zilizopotea tutapata wahalifu wengi sana na kuwaadhibu kwa makosa wanayotenda