Kesho Jumatano katika Tanzania Daima nimeandika sehemu ya pili ya makala hiyo. Kwanza nimemuomba radhi Sitta na Watanzania kwa lugha kali niliyotumia dhidi yake na dhidi ya Watanzania wenzangu. Naamini katika kukosoana. Nimekiri mapungufu katika maandishi yangu. Hata hivyo nimesisitiza msimamo wangu kuhusu Sitta uko pale pale. Nimejaribu kutumia lugha ya staha kueleza kile ninachoamini kuhusu sakata la Dowans na vitanzi tulivyojifunga
Kibanda to be honest wengi hatujapendezwa na makala yako, si kwamba hatuna uwezo wa kuchambua mambo. Kwanza uliandika kwa hasira na kuonyesha kuwa ni wewe tu ndio mwenye mtazamo sahihi kiasi cha kusema wote wanaomuunga mkono Sitta ni mazuzu(ingawa hukutumia neno zuzu).
Katika makala yako, tofauti kabisa na makala za wapambanaji wengi unaonekana kabisa kutokuchukizwa na malipo ya dowans bali wanaopinga ndio hutaki hata kuwasikia. Hiyo imewapa wasiwasi watu wengi sana wanaofuatilia makala zako na especially ile ya jumatano.
To me naona TZ Daima polepole limeanza kuchukua direction tofauti kidogo na hasa makala zako, ushauri wangu kwako ni kuwa jitathmini upo wapi kwa sasa vinginevyo ukiendelea hivi hilo gazeti la TZ Daima hasa la j5 tutaliweka pembeni tutaendelea na Mwanahalisi na Raia Mwema. Don't say i didn't warn you!