Naliona anguko la Kibanda

Naliona anguko la Kibanda

SIO LAZIMA WOTE TUKUBALIANE NA SITTA NA HATA KIBANDA SIO LAZIMA TUKUBALIANE NAE NA HILI SIO SWALA LA KUJENGA CHUKI,TUNAWEZA KUMCRITISIZE LAKINI SIO KUMZUSHIA ETI YUKO KWENYE PAYROLL YA RA ,SIO POA KIBANDA NA SITA NI WATU NA WANA HAKI KIKATIBA KUTOA MAWAZO KAMA SITTA NAE KACHUKIA ARUDI KWENYE VYOMBO VYA HABARI ASEME ANAONAJE MAONI YA KIBANDA.

KIBANDA NI SHUJAA AMELIJENGA TANZANIA DAIMA KUTOKA ZERO MPAKA HAPO LILIPO NO ONE CAN SAY NO ON THIS EVEN AIKAELI FREEMAN MBOWE ANAJUA KAZI YA KIBANDA NI PERFECT ALWAYS,

HONGERA FREEMEDIA KWA UHURU WA MAONi.
 
Mkuu hata mimi niliisoma article ya Kibanda na niliona jinsi alivyoonesha chuki zisizo na msingi kwa mzee Sitta. At first nikashangaa namna ambavyo gazeti la TZ daima lilivyofanya U-Turn kwa mtu anayepiga vita malipo ya Dowans.

Nadhani watu wa Mwananchi nao hawakupendezwa na hiyo article ndio maana wakamhoji mzee Msuya waone kama kweli na yeye hajapendezwa na Sitta kama Kibanda alivyokuwa anaproject.

Mzee akaeleza bayana kuwa yupo upande wa Sitta. Nadhani anachofanya Kibanda ni kujaribu kuwafrustrate kimtindo watu wanaopingana na malipo ya Dowans. Sitta sio mkamilifu by any measure of standards lakini anaposimama upande wa wananchi lazima tumsapoti.

Mnaweza kutuwekea Article Nzima ili Tuijadili Hiyo Article? Maana msipoiweka watu wataanza Kumjadili Mtu badala ya Article yenyewe
 
SIO LAZIMA WOTE TUKUBALIANE NA SITTA NA HATA KIBANDA SIO LAZIMA TUKUBALIANE NAE NA HILI SIO SWALA LA KUJENGA CHUKI,TUNAWEZA KUMCRITISIZE LAKINI SIO KUMZUSHIA ETI YUKO KWENYE PAYROLL YA RA ,SIO POA KIBANDA NA SITA NI WATU NA WANA HAKI KIKATIBA KUTOA MAWAZO KAMA SITTA NAE KACHUKIA ARUDI KWENYE VYOMBO VYA HABARI ASEME ANAONAJE MAONI YA KIBANDA.

KIBANDA NI SHUJAA AMELIJENGA TANZANIA DAIMA KUTOKA ZERO MPAKA HAPO LILIPO NO ONE CAN SAY NO ON THIS EVEN AIKAELI FREEMAN MBOWE ANAJUA KAZI YA KIBANDA NI PERFECT ALWAYS,

HONGERA FREEMEDIA KWA UHURU WA MAONi.
We don't dispute this, we are only saying he's on RA's payroll and he can't deny that, so u shouldn't speak for him! He's a member here, he can pm me abt it
 
kuhusu dowans nadhani tdaima wana ajenda yao! tangia serikali ilipojaribu kununua mitambo ya kampuni hiyo. ninasikitika:sad:
 
Mnaweza kutuwekea Article Nzima ili Tuijadili Hiyo Article? Maana msipoiweka watu wataanza Kumjadili Mtu badala ya Article yenyewe

Mkuu Albedo, nimejaribu kuitafuta online kwenye toleo la tarehe 12 mwezi huu sijaiona, i only have the paper. Mwenye hiyo article please help.
 
...........Kwanza hakuna mahala popote ambapo mawaziri katika serikali ya sasa baada ya uchaguzi wamekaa kujadili kama baraza la mawaziri kuhusu hukumu ya ICC kati ya mafisadi Dowans na Serikali ya CCM. KWA HIYO, suala la uwajibikaji wa pamoja halipo kwa sababu mawaziri hawajawahi kukaa na kujadili na kuwa na uamuzi wa pamoja kuhusu hukumu ya ICC.


Kama Kibanda ni ''member'' humu ndani, basi apate hii taarifa na hivyo aachane na uandishi wa mwaka 47. Uwajibikaji wa pamoja unakuwa valid tu kwa jambo lililojadiriwa na WOTE na kupitishwa/kukubaliwa na MAJORITY.

JK, Werema na Ngeleja hawawezi kukaa kama kamati and then wakurupuke na story kwamba Serikali imeridhia kuwalipa DOWANS
 
Waliosema pesa ni shetani hawakukosea.Sitta anachopigania kina manufaa kwa sisi wananchi wa kawaida,hata akitokea fisadi yoyote akapinga malipo ya Dowans nitamuunga mkono bila kumwangalia yeye.Dowans wakilipwa ninaamini hiyo pesa itatumika kuvuruga mambo mengi, katiba ikiwa ni moja wapo.
 
Sakata la Absolom Kibanda na Samuel Sitta

Dowans yawa ‘tunda la katikati’
la kujua mema na mabaya!


Na Simon Mhina



Sakata la kampuni hewa ya kufua umeme ya Richmond na baadaye Dowans, ambalo linaelezwa kuwa ni vita baina ya wananchi wengi wanyonge na kundi la wanyonyaji wachache, limetoa funzo kubwa kwa mustakabali wa taifa letu.
Funzo kubwa lililotokana na mjadala huo, ni kujua yupi yuko upande upi na kwa maslahi yepi!
Ni sakata gumu la kufa na kupona, ambalo limefanya mashetani waonekane malaika, na Malaika watakatifu wang’arao waitwe mashetani tena waasi.
Katika sakata hilo, tumeshuhudia wananchi wanyonge wanaolazimika kutembea kwa miguu kutokana na kukosa Sh. 250 ya nauli ya kukweka daladala, wakiitwa wajinga kwa vile wamepaza sauti zao wakipinga kukamuliwa Bilioni 94, ili wanyonyaji hao wachache walipwe.
Jumatano iliyopita siku ya kusherehekea Mapinduzi ‘matukufu’ ya Zanzibar, ni sku ambayo binafsi siwezi kuisahau maishani mwangu, kwani nilisoma makala iliyoandikwa na mwanahabari mwenzangu Absolom Kibanda ambaye ni Mhariri wa gazeti nilipendalo la Tanzania Daima, ambaye alisema aliyekuwa Spika wa Bunge lililopita Samuel Sitta ni muasi, dhaifu asiyefaa kuongoza zaidi ya watu wawili na wala asiye na uwezo wa kujiongoza hata yeye mwenyewe. Haya ni matusi!
Hapa nanukuu maneno ya Kibanda katika makala hiyo, “Kwangu mimi Sitta ni kiongozi na mwanasiasa muasi.Ni mtu asiyestahili kabisa kupewa jukumu la kuongoza watu wanaoanzia wawili, zaidi ya kujiongoza yeye binafsi. Hata hili la kujiongoza mwenyewe nina mashaka nalo”
Awali ya yote huyo anayekashifiwa hivi ni mtu ambaye ameshikilia na bado anaendelea kushikiliwa nafasi kubwa za juu serikalini, bila yeye kuandika barua ya maombi.
Mwaka 2005 Sitta alipigiwa kura na wabunge wote akawa Spika wao. Mwaka 2010, Rais wa Jamhuri ya Muungano akamteua kuwa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Lakini Bwana mhariri anasema huyu hafai kuongoza zaidi ya watu wawili na ana mashaka kuwa hawezi hata kujiongoza mwenyewe! Ndio maana nikatanguliza kusema hayo ni matusi.
Kama Sitta ni duni kwa kiwango hicho, wabunge waliomchagua awe kiongozi wao Bwana mhariri anawaweka kwenye kundi gani?
Kama Sitta ni duni kiasi cha kushindwa kujiongoza mwenyewe, huyo Rais Kikwete aliyempa wadhifa wa uwaziri bila kuombwa, Bwana Kibanda anamuweka kwenye kundi gani? Ama kweli tunda la katikati (Dowans) Tamu!
Awali nilidhani huenda Bwana Mhariri huyo ana ugomvi binafsi na Sitta, lakini baadaye nikagundua kwamba kinachosababisha yote haya ni Dowans, ambayo imegeuka kuwa “Tunda la katikati” la kujua mema na mabaya. Nitafafanua baadaye.
Bwana mhariri wa gazeti hilo ambalo binafsi naliheshimu, hakuishia kumtusi Sitta pekee, bali akawaita wajinga watanzania walio wengi.
Naomba nimnukuu tena “ Ni wazi kwamba Sitta anafanya yote haya kwa sababu anatambua kwamba machoni mwa watanzania wengi waliowajinga, yeye ndiye shujaa wao na kwa hakika ndiye anayeonekana kuwa na jicho moja miongoni mwa vipofu wengi” Astaghafilulaaa!
Katika Makala hayo Bwana mhariri hakusita kutaja kuwa sababu za kumsema vibaya Sitta ni Dowans.
Anasema Sitta hakustahili kutoa kauli za kuashiria kukataa ‘mbinu’ za kuilipa Dowans mabilioni hayo ya Shilingi.
Anasema kitendo hicho kinaenda kinyume na uwajibikaji wa pamoja na kwamba Sitta ametoa siri za baraza za mawaziri! Bwana mhariri Kibanda, akasisitiza kwamba kuna umuhimu Waziri Mkuu amshauri Rais amfukuze Sitta.
Haya ndiyo matokeo ya tunda la katikati, ambapo baada ya Adamu na Hawa kuonjeshwa na kulila, licha ya kwamba walinogewa, lakini matokeo yake walijiukuta wako uchi!
Hawakupata kile walichoahidiwa na nyoka (kufanana na Mungu) badala yake wakatengana naye.
Awali nyoka aliwadanganya binadamu hao wa kwanza kwamba Mungu alikuwa amewakataza kwa makusudi ula tunda hilo, kwa vile alifahamu wakilionja watafanana naye.
Hata hivyo walivyoleweshwa na ushawishi wa nyoka yule na kula tunda, walijiona wako uchi tofauti na mategemeo yao kuwa wangefanana na Mungu.
Hata hivyo yule nyoka aliyemdanganya Adamu na Hawa alishakufa, lakini kwa hili la tunda la Dowans bila shaka nyoka ‘R.A’ au kwa kirefu ‘red action’ ametumika kumdanganya Bwana mhariri! Ila Bustani ya Eden iliyotumika kumdanganya inabaki kuwa siri yao (Siku hizi bustani ziko nyingi).
Nyoka amemdanganya akampa tunda, kweli amenogewa lakini matokeo yake badala ya kufanana na hicho alichoahidiwa, amebaki uchi machoni mwa watanzania, kwani bila woga amewaita wajinga na vipofu!
Kiburi cha kufanya hivyo kinatokana na yeye kujiaminisha kwamba atafanana na ‘Mungu’ kwani ndivyo alivyoambiwa na nyoka ‘RA’ kabla hajapewa tunda. Hivyo tunda likamlewesha akajikuta anawaita ‘wajinga na vipofu’ watanzania ( wakiwemo kaka na dada zake).
Nasisitiza tena Bwana mhariri huyu tunayemjua, mtu mwema, mwenye waledi, asingefikia hatua ya kutoa maneno haya ya dharau bila kudanganywa.
Aidha kutokana na kuleweshwa na tunda hilo Bwana mhariri Kibanda mtu mwenye waledi, akapotosha kwa makusudi maana halisi ya “Uwajibikaji wa Pamoja”.
Na hapa tena naomba ni mnukuu “ Kosa la tatu ambalo Sitta anapaswa kukabiliana nalo ni lle la kuwadharau wakuu wake wa kazi. Anatoa kauli kuhusu serikali kukataa kulipa Dowans wakati akijua fika kwamba Waziri Mkuu Pinda alipata kulizungumzia jambo hili na akasema iwapo mwanasheria mkuu wa serikali ataridhia suala la kulipa Dowans litakuwa halina mjadala”
Kwa kifupi Bwana Mhariri ametoa makosa mengi ambayo ameyatafsisi kwamba Sitta amekiuka uwajibikaji wa pamoja. Akaenda mbali zaidi akamfananisha na Agustine Mrema enzi zile za sakata la Chavda.
Lakini Bwana Mhariri Kibanda anapaswa kuelewa kuwa tunaposema ‘uwajibikaji wa pamoja’ awali tunapaswa kujiuliza ‘kuwajibika’ katika nini?
Uwajibikaji wa pamoja, hususan kweye baraza la mawaziri ni kusimamia na kutetea maamuzi mema ambayo washiriki wameyakubali na kuyapitisha hata kama mmoja wao hakukubaliana.
Nimesema ‘maamuzi mema’kwa sababu maamuzi hayo lazima yazingatie katiba, haki za binadamu na kanuni za uongozi.
Kwa hiyo Bwana Mhariri asifikiri kwamba ‘uwajibikaji wa pamoja’ wa baraza la mawaziri utakuwa halali, kama utahusu kuyavunja majeshi ya ulinzi na usalama na kubakisha wanamgambo!
Hata hivyo hakuna ukiukwaji wa uwajibikaji wa pamoja uliofanywa na Sitta katika sakata la Dowans, kwa vile hilo suala halikupata kujadiliwa na baraza la mawaziri wala chombo chochote cha serikali!
Badala yake, Sitta ndiye amekuwa mtetezi mzuri wa baraza la mawaziri, pale alipomshangaa waziri mwenzake kufanya maamuzi makubwa kama hayo ya kuilipa Dowans bila kujadiliwa na baraza hilo.
Vilevile Bwana mhariri amepotosha kwa makusudi kauli ya waziri Mkuu ambayo yeye mwenyewe ameiandika na mimi nikamnukuu hapo juu. Narudia tena kunukuu kwa uchache, “…Waziri Mkuu Pinda alipata kulizungumzia jambo hili na akasema iwapo mwanasheria mkuu wa serikali ataridhia suala la kulipa Dowans litakuwa halina mjadala”
Hapa neno ‘iwapo mwansheria Mkuu ataridhika” maana yeke ni kwamba jambo hilo bado lina utata, halifahamiki hata na waziri mkuu wenyewe hivyo ni jipya. Ndio maana akatumia neno ‘iwapo’.
Kama lingekuwa neno la kiofisi linalotokana na baraza la mawaziri au angalau ana kumbukumbu nalo, Pinda asingetumia neno ‘iwapo’. Angesema moja kwa moja ‘Tutalipa”.
Hivyo kitendo cha kulinganisha sakata la Mrema na Sitta ni upotoshaji wa makusudi kwa vile Chavda alijadiliwa kwenye baraza la Mawaziri, lakini sio tu Dowans haijapata kujadiliwa, lakini hata majina ya wamiliki wake rasmi hayafahamiki.
Hata hivyo mimi na watanzania wenzangu (wajinga na vipofu) ni heri yetu kupata mtu ambaye yupo tayari kwenda kinyume na maamuzi yenye kuliangamiza taifa letu na sisi wenyewe.
Lakini kinachofurahisha ni jinsi Bwana Mhariri Kibanda alivyoumbuliwa na Waziri Mkuu mstaafu Cleopa Msuya, ambaye katika makala yake ndiye alikuwa ‘somo wake’
Alisema wazi kuwa anaamini Msuya angekuwa waziri Mkuu leo, Sitta asingekuwa na kazi kama ilivyotokea kwa Mrema.
Siku chache baadaye Msuya akatoa taarifa ndefu kwenye gazeti moja akisisitiza kumuunga mkono Sitta na kulilaani tunda la Kati kati (Dowans)! Akasema hajui ni kwasababu gani Dowans walipwe! Kibanda tafuta taulo ujisitiri!
Ni jambo la kusikitisha kuona hasara ya Bilioni 94 inayowakabili watanzania Bwana Mhariri haioni, kwake anachoona ni tatizo ni Sitta!
Aidha Bwana mhariri haoni umuhimu wa kujadili kesi iliyoipa ushindi Dowans, kufunguliwa kinyemela huko ICC na kusikilizwa kwa siri kubwa kama maazishi ya Daudi Balali, ila kwake yeye tatizo ni Sitta. Kumbe tunda la katikati linalewesha, badala ya kujuza mema na mabaya! Au labda Bwana Kibanda ameahidiwa kuwa Ghorofa!
Ni katika ulevi huo, Bwana mhariri Kibanda ametoa kauli zinazoelekea kutoboa siri iliyojificha, pale aliposema “Sitta ni mwanasiasa aliyekosa ustahimilivu na uvumilivu ni mtu aliyekosa upendo kwa maadui zake,”.
Jamani kumbe Sitta ana maadui? Lakini ametakiwa eti awe na uvumilivu kwao.
Katika makala hayo Bwana Mhariri akawataka wanasiasa aliodai wananyooshwa kidole na Sitta kwamba ni Rostam Aziz, Nimrod Mkono na Edward Lowassa.
Kwa hiyo anataka kutueleza nini kuhusu uhusiano wa Dowans na hayo majina aliyoyataja? Anataka kusema hao anaowaita maadui wa Sitta, chanzo cha uadui wao ni Dowans? Ndio maana nikatangulia kusema hapa ametoboa siri aliyojitahidi kuificha, tangu mwanzo hadi mwisho wa makala yake hiyo. Kama aliowataja hawahusiki, iweje uadui wa jamaa hao na Sitta, uibuliwe kwenye sakata la Dowans? Ama sivyo, kwanini azungumzie ‘uadui’ binafsi wa watu katika mjadala wa Dowans?
Nafikiri wakati mwingine atatueleza kwamba hao maadui wa Sitta chanzo cha uadui wao ni nini, kama sio Dowans!
Tunavyojua Sitta ameshatoa msimamo wake wa kukataa Dowans walipwe, hivyo bila shaka maadui wake walio kinyume chake, wanataka Dowans ilipwe. Na kama wanataka ilipwe katika mazingira yaliyojaa dhambi nyeusi kiasi hiki, maana yake ni kwamba watafaidika na malipo hayo.
Kesho yake tena kwenye gazeti hilo hilo, ikaandika taarifa inayomnukuu mwanasheria Kennedy Fungamtama akiitaka serikali kupuuza kauli za Sitta kwamba Dowans isilipwe.
Fungamtama alichukua muda mwingi kuitetea Dowans na kuwatisha watanzania kwamba wasipolipa fedha hizo, eti watajiingiza kwenye matatizo ya kunyimwa misaada na wafadhili pamoja na kukosa wawekezaji.
Huyu Fungamtama anafanya kazi hii ya kuitetea Dowans kwa maelekezo ya nani? Kwanini Dowans wenyewe wasiwe mstari wa mbele kutetea hukumu ya ICC? Bila shaka Fungamtama ‘alishafungashiwa mtama’ wake, akawake kibindoni, vinginevyo asingeweza kufanya kibarua kisichomhusu.
Mimi sina mgogoro na Fungamtama kutoa maoni yake, lakini kinachoshangaza ni jinsi anavyotetea uhalali wa Dowans kulipwa, kuliko wenye Dowans wenyewe! Hili linatia shaka kwamba huenda amefanya kazi hiyo kwa malipo kwa vile kabla mtanzaia yoyote hajapata hukumu hiyo ya ICC, Fungamtama anasema yeye ameipata na ameisoma mara kibao! Kazi tunayo. Ninachosema hapan ni kwamba kama Fungamtama amefungashiwa mtama wake akaweka kibindoni, aseme kwani sio dhambi, kwavile wakili kama yeye anaruhusiwa kumtetea mtu kwa malipo, lakini asiwe mnafiki wa kutoa utetezi unaoelea hewani.
Ulevi wa tunda la katikati utafanya mengi yafahamike, nasi wananchi tunaoitwa wajinga na vipofu, tunamuomba mwenyezi Mungu iwe hivyo (Amen) kwani yafahamika ni faida yetu na siku ya siku Goliati atadondoka mwenyewe!
 
Hebu tuwe na culture ya kusoma. Tuache uvivu. Yaani pages 2 watu mnalalamika. By the way hayo yalishajadiliwa hapa JF
 
Kama nilivyochangia kule kwenye thread ya hoja kwenda kwa Balile wa Mtanzania, mathinkers wengi humu tunaelekea kuwa mediocres-hatusomi.Mwandishi anafanya kitu ambacho watanzania wengi na hata wachambuzi makini wameshindwa kukifanya. Kibanda amekuwa akindika kila wiki kwa takribani mwezi sasa katika Tanzania Daima la Jumatano kumkashifu Sitta na akionekana kuchekelea zigo la mabilioni wanayotakiwa kulipwa Dowans. Kibanda amekuwa akichekelea lakini kwa ujanja ambao si wake, amekuwa akisukuma zigo hilo eti ni lawama kwa Sitta na Bunge lake lililozikataa Richmond na Dowans.

Balile amekuwa akiandika upuuzi huo na hakuna wa kumjibu, mathinker wanapotumia jukwaa hili kujibu kwa hoja sadifu, mathinker wanaotakiwa kusoma wanaishi aya ya kwanza na kuanza kulaumu, kama si ujinga wa kweli, basi nadhani kuna watu wanahujumu hili jukwaa kwa kuanzisha mada za kupuuza michango yenye nguvu matokeo yake jukwaa hili litakosa maana.
 
Jamani, ni uchambuzi mzuri usiochosha. Kibanda amejidhihirisha katika makala zake nyingi kwamba yu mnufaikaji wa DOWANS. Ni makala za utetezi kwa EL, RA, Karamagi na members wa hilo kundi. Sitta kwa Kibanda ni adui na huwezi msoma akimzungumza kwa jema, na yote ni kutokana na kununuliwa na hilo kundi. Huyu hana tofauti na kina Balile pale Mtanzania.

Tatizo ambalo Kibanda anashindwa kufahamu ni uwezo wake mdogo wa kujificha kuonyesha mapenzi yake yalipo pale anapochambua hoja.

Sielewi nini kilitokea lakini ilikuwa naye ajiunge Rai.
 
Mkuu Ubarikiwe, umemaliza yote!

Kama nilivyochangia kule kwenye thread ya hoja kwenda kwa Balile wa Mtanzania, mathinkers wengi humu tunaelekea kuwa mediocres-hatusomi.Mwandishi anafanya kitu ambacho watanzania wengi na hata wachambuzi makini wameshindwa kukifanya. Kibanda amekuwa akindika kila wiki kwa takribani mwezi sasa katika Tanzania Daima la Jumatano kumkashifu Sitta na akionekana kuchekelea zigo la mabilioni wanayotakiwa kulipwa Dowans. Kibanda amekuwa akichekelea lakini kwa ujanja ambao si wake, amekuwa akisukuma zigo hilo eti ni lawama kwa Sitta na Bunge lake lililozikataa Richmond na Dowans.

Balile amekuwa akiandika upuuzi huo na hakuna wa kumjibu, mathinker wanapotumia jukwaa hili kujibu kwa hoja sadifu, mathinker wanaotakiwa kusoma wanaishi aya ya kwanza na kuanza kulaumu, kama si ujinga wa kweli, basi nadhani kuna watu wanahujumu hili jukwaa kwa kuanzisha mada za kupuuza michango yenye nguvu matokeo yake jukwaa hili litakosa maana.
 
Back
Top Bottom