Hii story haina mantiki hasa kweli kama mwandishi angekuwa mtu makini, maswali yafuatayo au mambo yafuatayo ni muhmi kujiuliza na kuyafahamu; Iwapo watu wana uwezo wa kufoji sahihi hata za viongozi wakubwa, mihuri na nyaraka mbalimbali hadi kukwapua kwenye mabenki na sehemu nyingine nyeti ( kama ilivyowahi kuripotiwa sehemu mbalimbali nchini na nje ya nchi) bila kutumia nguvu ya aina yoyote, iweje huyu atumie nguvu kama sio Uongo???
Pili, kulikuwa na umuhimu gani hasa wa kumfuata TABU badala ya kutumia mbinu kibao ambazo zipo? yaani huyo anaehitaji hiyo sahihi alikua mjinga kiasi gani hadi amfuate Katibu wa RA huku akijua fika uhusiano wa karibu kati ya Tabu na RA ( kama ilivyowahi kuripotiwa kwenye vyombo vya habari nchini).
Tatu, je ni vigumu sana kuipata sahihi ya RA hadi aende ofisini kwake? yaani hakuna nyaraka nyingine zozote ambazo RA ameweka sahhihi ni hadi ofisini kwake?
Nne, kwa nini amsubiri wakati anatoka ofisini huku akijua fika kuwa hawezi kuwa anatembea na document zenye sahihi, hapa huyu mtuhumiwa ambaye mimi naamini hayupo, ni mjinga kiasi gani amsubiri Tabu atoke ofisini ndio amfuate??
Tano, angewezaje (Mtuhumiwa hewa) kutoa pesa kidogo hivyo (5M) hali akijua nafasi ya Tabu na kipato chake, kweli Tabu angekuwa radhi kutoa sahihi ya Bosi wake kwa Million tano tu??? labda kama hawafahamu vizuri.
Mwisho, ni vyema unapotunga stori, jiulize kwanza baadhi ya maswali mwenyewe, yaani, jiweke kwenye position ya msomaji na sio kuvutiwa na hisia zako tu. Naombeni ushauri kwa haya machache. Asante