Naliona anguko la Kibanda

Naliona anguko la Kibanda

Naamini Jamiiforums ni Home of Great Thinkers sasa hawa ndugu zangu akina informer na wengine ni kwa nini wanashusha tuhuma nyingi wasizo na uhakika nazo. Mimi ndiye Absalom Kibanda. Nimekuwa Mhariri wa Tanzania Daima huu ni mwaka wa nne na ninaelekea wa tano. Msimamo wangu kuhusu mambo kadha wa kadha haujabadilika.

Kila mtu ana uhuru wa kufikiri anavyotaka. Niweke kumbukumbu sawasawa. Sina sababu hata moja ya kununuliwa na mtu yeyote. Rostam Aziz amekuwa mkurugenzi wangu Mwananchi na nikaacha kazi kinyume cha matakwa yake. Ninaamini katika mabadiliko. Nimeanza kumpinga Sitta kila anapofanya mambo ambayo sikubaliani nayo tangu akiwa spika na hata kabla Lowassa hajajiuzulu.

Nikiwa mhariri Mtendaji wa Tanzania Daima ninatoa uhuru kwa viongozi wote pasipo kujali misimamo yao kutoa maoni yao. Nimeruhusu mijadala ya kina kupitia Tanzania Daima kutoka pande zote mbili. Kwangu mimi Rostam, Sitta, Lowassa, Chenge, Mwakyembe na wengine wote ni vyanzo muhimu vya habari na kwa Tanzania Daima wana nafasi sawa kihabari. Msimamo wangu huo uko bayana na kimsingi hili ndilo gazeti linalokimbiliwa na kila mtu, hatufungamani na upande wowote zaidi ya kupigania mabadiliko. Ninapata furaha nisikiapo nikituhumiwa kuwa wakala wa Chadema, mara wakala wa CUF, mara wakala wa mafisadi, mara wakala wa Kikwete kwa sababu ya msimamo huru wa mawazo.

Nilikataa tangu mapema kujiingiza katika vita ya ufisadi inayopiganwa na akina Sitta na akina Mwakyembe kwa sababu nimejiridhidhs kwamba ni vita ya kitapeli na yenye malengo ya kisiasa zaidi kuliko kihalisia. Naamini na hili nimekuwa nikiliandika katika safu yangu ya Tuendako kuwa ufisadi uliopo nchini unakigusa Chama Cha Mapinduzi moja kwa moja. Kwa hiyo hakuna anayeweza kumnyoshea mwenzake kidole. Viongozi wote wa juu wa chama hicho tawala wakianzia na mwenyekiti wao wa taifa hawana ubavu wa kukwepa tuhuma halisi za chama chao kuhusika katika ufisadi.

Hiyo ndiyo dhambi yangu iliyonikosanisha na wengi katika taaluma. Nimekataa kuingia katika mkumbo wa kujifanya mwanaharakati na jemedari wa ufisadi kwa kuwa naamini ni unafiki. Ni jambo la kheri kwamba wamiliki wa Tanzania Daima wanathamini mchango wangu, wanaufahamu na kuuamini msimamo wangu, wanaujua uzushi wa kila siku wa akina informer ambao wao wanalipwa mamilioni ya fedha kuwachafua akina Lowassa kwa sababu ambazo mimi ninazijua na ushahidi upo.

Acha nihukumiwe kwa haki huku nikiwa na uhakika kuwa ipo siku historia itanitetea
 
Mnaweza kutuwekea Article Nzima ili Tuijadili Hiyo Article? Maana msipoiweka watu wataanza Kumjadili Mtu badala ya Article yenyewe

Mkuu kuwa na uhakika wa asilimia 100% na uchambuzi huu, nimesoma kwa makini habari zote mbili ya Kibanda na ya Mwananchi na hapa nilipo nina nakala ya magazeti yote mawili.
 
Nashukuru kwa bwana Kipanda,kujitokeza na kutoa msimamo wake,ila hata mimi ckubaliani nae kwa lugha aliyoitumia,ni lugha kali na ya kufedhesha hasa kwa mtu mzima kama 6(acha suala la vyeo),ungeweza tumia lugha nzuri na ya staha,yenye hoja na ujumbe ungefika tena vizuri,kumbuka 6,ni mume wa m2 na pia ana watoto,.chondechonde waandishi kalamu zenu ni kali kuliko risasi,so msitumie vibaya hizo kurasa zenu,na wala ninyi sio watu special sana,ni mgawanyiko wa kikazi,naomba kuwasilisha
 
Kama hajachakachuliwa, mbona siku hizi yuko busy kutuandikia habari za Lowasa?? hata gazeti la uhuru halimpi coverage yoyote Lowasa lakini Kibanda siku hizi imekuwa bandika bandua Lowasa hakosi kwenye front page.

Ni dhahiri kwamba kibanda ameshachakachuliwa, na siku zake zinahesabika, yuko njiani kuelekea kwa bosi wake muya fisadi papa

si umeona kuna mhariri mmoja tayari ameshachoropoka na kuingia zizini?


Mbona hatuwaulizi viongozi wa dini ambao siku zote wanamualika Lowassa kwenye shughuli zao? Nao wamechakachuliwa? Mbona hatushangai iweje CCM impitishe kuwa mgombea ubunge Monduli, nako huko chama chake kimechakachuliwa? Kwa nini akiandikwa gazetini iwe nongwa? Msimamo wangu ni thabiti LOwassa akizungumza mambo ya msingi habari zake zitaandikwa Tanzania Daima, akifanya mambo yasiyostahili ataandikwa pia kwa uzito ule ule. Hakuna aliye salama Tanzania Daima hususan kama ni kiongozi wa kitaifa.
 
Nashukuru kwa bwana Kibanda,kujitokeza na kutoa msimamo wake,ila hata mimi ckubaliani nae kwa lugha aliyoitumia,ni lugha kali na ya kufedhesha hasa kwa mtu mzima kama 6(acha suala la vyeo),ungeweza tumia lugha nzuri na ya staha,yenye hoja na ujumbe ungefika tena vizuri,kumbuka 6,ni mume wa m2 na pia ana watoto,.chondechonde waandishi kalamu zenu ni kali kuliko risasi,so msitumie vibaya hizo kurasa zenu,na wala ninyi sio watu special sana,ni mgawanyiko wa kikazi,naomba kuwasilisha

Kesho Jumatano katika Tanzania Daima nimeandika sehemu ya pili ya makala hiyo. Kwanza nimemuomba radhi Sitta na Watanzania kwa lugha kali niliyotumia dhidi yake na dhidi ya Watanzania wenzangu. Naamini katika kukosoana. Nimekiri mapungufu katika maandishi yangu. Hata hivyo nimesisitiza msimamo wangu kuhusu Sitta uko pale pale. Nimejaribu kutumia lugha ya staha kueleza kile ninachoamini kuhusu sakata la Dowans na vitanzi tulivyojifunga
 
Pole poor Kibanda! Wana jf njaa ni mbaya inaweza kumfanya mtu akahemewa kichogoni hv hv! Huyu bwana Kesha hemewa! Pole Poor Kibanda
 
tutahakikishaje km mikono yako ni safi kwani kuna cku ulijadiliwa juu ya suala km hili lkn haubadiliki
 
Mhariri Mtendaji wa Tanzania Daima, Absalom Kibanda, anafanya kazi part-time kwenye magazine inayomilikiwa na Edward Lowassa inaitwa UMOJA. Pia Kibanda amekuwa anatoa habari za kumbeba Lowassa, Rostam Aziz na Andrew Chenge kwenye Tanzania Daima mara nyingi. Kwa kupokea maagizo na malipo kutoka kwa Lowassa na Rostam Aziz, Kibanda pia amekuwa akiandika habari na makala nyingi za kuwakashifu Samuel Sitta, Harisson Mwakyembe, Bernard Membe na John Magufuli.

Tanzania Daima ni moja ya magazeti yanayotumiwa na fisadi Rostam Aziz kutetea ufisadi mbalimbali, ikiwemo malipo kwa Dowans kwa nguvu zote. Wanaitumia Tanzania Daima kwa kuwa gazeti linaaminika kuwa ni huru na ni rahisi ku-brain wash watu kuliko kutumia Mtanzania/Rai ambayo Watanzania hawayasomi tena sasa baada ya kugundua kuwa yanamilikiwa na Rostam.

Cha kushangaza ni kuwa mmiliki wa Tanzania Daima, Freeman Mbowe, anaachia tu gazeti lake litumiwe na mafisadi kupitia kwa Kibanda kuangamiza nchi.

Jarida la UMOJA halimilikiwi na Lowassa. Mimi si mtu wa kufanya kazi kwa mtu kwa kujificha hata siku moja. Wewe ni ndugu yangu kwa nini uwapotoshe Watanzania wanaosoma thread hii. Ni vyema ukiwaeleza udhaifu wangu wa kweli. Kama ningekuwa ninatawaliwa na fedha nisingekuwa Tanzania Daima leo. Kosa langu ni kuruhusu mijadala huru katika Tanzania Daima.

Nitakuwa ninakwenda kinyume cha dhamira yangu nikianza kuzuia habari zinazowahusu akina Lowassa, Rostam, Chenge na wengine kama wanavyofanya wahariri wengine. Nimekataa kuwa mnafiki kujifanya nawapiga vita watu fulani fulani na wakati huo huo nikikutana na watu hao mafichoni. Namshukuru Mungu nimekuwa mhariri katika kipindi ambacho kikundi fulani chenye nguvu katika media kilipoamua kutumia media na kututumia sisi waandishi kuwafunga midomo wengine na kuwachafua wengine.

Wakati waandishi wa habari wengi wakipiga kampeni za kumuunga mkono Kikwete mwaka 2005 hata kuliunga mkono kundi la mtandao ambalo moja ya sera zake zilikuwa ni kuwachafua akina Dk. Salim, Sumaye, Malecela etc baadhi yetu tulisimama kidete kupinga kosa hilo la kuwachafua wengine kwa sababu ya urais. Nitakuwa mpumbavu iwapo nitakubali leo hii kikundi cha watu wengine wawachafue wengine kwa sababu tu ya urais wa mwaka 2015. Kosa hilo nimelikataa.

Ni jambo jema kwamba Mbowe anazijua siasa za nchi hii, anawajua vyema ninyi akina informer na anaujua unafiki wenu. Wewe mwenyewe alikuwa akuajiri mwaka 2005 lakini kwa tamaa zako za fedha ukaenda kwa mwajiri mwenye pesa. Laiti kama familia ya Mbowe ingekuwa ni ya kusikiliza majungu na uzushi wa akina informer ingenifukuza kazi zamani. Wasomaji wa Tanzania Daima endeleeni kusoma gazeti hili na ikibidi andikeni hata makala za kupinga mitazamo yangu na ya wengine kwani huo ndiyo uhuru wa habari. Siogopi challenges za kukosolewa, kupingwa na hata kuzushiwa. Niko thabiti, namshukuru Mungu
 
For sure nimekuwa ni mpenzi wa makala za Kibanda lakini tangu nimesoma hiyo makala nimemuweka kundi chafu ka RA.Ukitaka kumjua Kibanda vizuri soma toleo la kwanza na la pili la Magazine ya Umoja utagundua jinsi anavyopamba rushwa, ufisadi na kuponda wapambanaji dhidi ya ufisadi.Ni ukweli ulio wazi kwamba,nimeweka msimamo wa kutosoma makala za huyu bwana tena.Ni uchafu mtupu na amenunuliwa.Bila shaka ana gawio kubwa kwenye dili la Dowans
 
Mbona hatuwaulizi viongozi wa dini ambao siku zote wanamualika Lowassa kwenye shughuli zao? Nao wamechakachuliwa? Mbona hatushangai iweje CCM impitishe kuwa mgombea ubunge Monduli, nako huko chama chake kimechakachuliwa? Kwa nini akiandikwa gazetini iwe nongwa? Msimamo wangu ni thabiti LOwassa akizungumza mambo ya msingi habari zake zitaandikwa Tanzania Daima, akifanya mambo yasiyostahili ataandikwa pia kwa uzito ule ule. Hakuna aliye salama Tanzania Daima hususan kama ni kiongozi wa kitaifa.

Mtumikie kafiri upate mradi wako. We know your type mate.

Kesho Jumatano katika Tanzania Daima nimeandika sehemu ya pili ya makala hiyo. Kwanza nimemuomba radhi Sitta na Watanzania kwa lugha kali niliyotumia dhidi yake na dhidi ya Watanzania wenzangu. Naamini katika kukosoana. Nimekiri mapungufu katika maandishi yangu. Hata hivyo nimesisitiza msimamo wangu kuhusu Sitta uko pale pale. Nimejaribu kutumia lugha ya staha kueleza kile ninachoamini kuhusu sakata la Dowans na vitanzi tulivyojifunga

Waandishi kama wewe ndio mmekuwa makuwadi wa kina RA, EL et al. Tanzania ya leo sio ile ya jana ya kulala lala ... ... No retreat no surrender haiingii akilini kuona vimburu kama wewe mnanakuja hapa kutaka ku-justfy utumbo ambao unaandika.
 
tutahakikishaje km mikono yako ni safi kwani kuna cku ulijadiliwa juu ya suala km hili lkn haubadiliki


Jambo la msingi dhamira yangu safi. Naipenda nchi yangu. Siwezi kubadilika kwa kuwa huo ndiyo msimamo wangu. Siku watu watakapoacha kunijadili basi nitakuwa nimekufa kiuandishi. Jambo moja liko wazi nikiwa ni mwandishi wa habari na mhariri nimejipa uhuru wa kukutana na kuzungumza na yeyote na mmoja wa watu ninaozungumza nao kama mwanahabari ni huyo wanayemuita Rostam Aziz. Hata katika makala ambayo ndiyo chanzo cha mjadala huu nimemtaja Rostam tena si kwa uzuri bali kwa dhambi yake ya mtandao. Mimi ndiye mwandishi wa kwanza wa habari kumtaja kwa jina Rostam Aziz na kumkosoa kwa sera zao mbovu za mtandao. Ni Tanzania Daima lililoandika kwa undani habari kuhusu Richmond kabla ya Kamati ya Mwakyembe. Najivunia rekodi yangu
 
Mtumikie kafiri upate mradi wako. We know your type mate.



Waandishi kama wewe ndio mmekuwa makuwadi wa kina RA, EL et al. Tanzania ya leo sio ile ya jana ya kulala lala ... ... No retreat no surrender haiingii akilini kuona vimburu kama wewe mnanakuja hapa kutaka ku-justfy utumbo ambao unaandika.


Naamini katika nguvu ya hoja siyo hoja za nguvu kama zako. Umeandika jambo gani la maana katika jamvi hili. Umechoka kufikiri wewe, huu si uwanja wako fungua majarida na magazeti ya udaku usome.
 
Kesho Jumatano katika Tanzania Daima nimeandika sehemu ya pili ya makala hiyo. Kwanza nimemuomba radhi Sitta na Watanzania kwa lugha kali niliyotumia dhidi yake na dhidi ya Watanzania wenzangu. Naamini katika kukosoana. Nimekiri mapungufu katika maandishi yangu. Hata hivyo nimesisitiza msimamo wangu kuhusu Sitta uko pale pale. Nimejaribu kutumia lugha ya staha kueleza kile ninachoamini kuhusu sakata la Dowans na vitanzi tulivyojifunga

Leo sitochangia hadi nihisome makala hiyo ya pili, Cha msingi KIBANDA simamia msimamo wako na wadau mnao amini kuwa KIBANDA kanunuliwa na mafisadi tunaomba ushahidi. KIBANDA ni member humu JF hivyo mkitoa ushahidi tutasubiri utetezi wake na kisha tutachambua mchele ni hupi na chuya ni zipi.
 
For sure nimekuwa ni mpenzi wa makala za Kibanda lakini tangu nimesoma hiyo makala nimemuweka kundi chafu ka RA.Ukitaka kumjua Kibanda vizuri soma toleo la kwanza na la pili la Magazine ya Umoja utagundua jinsi anavyopamba rushwa, ufisadi na kuponda wapambanaji dhidi ya ufisadi.Ni ukweli ulio wazi kwamba,nimeweka msimamo wa kutosoma makala za huyu bwana tena.Ni uchafu mtupu na amenunuliwa.Bila shaka ana gawio kubwa kwenye dili la Dowans

Kwa hiyo umesoma issue ya kwanza na ya pili ya UMOJA halafu unaandika uongo hapa kwamba kwenye jarida hilo kuna utetezi kwa mafisadi. Ama kweli tunajenga taifa la hatari la watu wasomi wazushi. Hebu waandikie wasomaji humu ukitoa ushahidi wa hilo ulilosema.
 
Kilichobaki ni nguvu ya umma kufanya kazi yake,mwaka huu watakoma mpaka kieleweke,paka amelala jikoni,maji yamezidi ugali unga,n.k ongezeeni
 
Naamini katika nguvu ya hoja siyo hoja za nguvu kama zako. Umeandika jambo gani la maana katika jamvi hili. Umechoka kufikiri wewe, huu si uwanja wako fungua majarida na magazeti ya udaku usome.

Do you think you really know me? If at all you were smart you wouldn't write in that Udaku paper of yours and come to justfy your ignorance.
 
Back
Top Bottom