Naishi naye ndio, Lakini...

Habari wana jamvi...

Natamani sana kupata msaada, uwe wa kimawazo, kisheria ama hata kiuzoefu tu katika hili ninalolipitia. Miaka mitatu iliyopita, nilikutana na mwanamke fulani ghafla tu, [ingawa badae niligundua kuwa tulikuwa tukiishi mtaa mmoja] na pasipo hata makubaliano yoyote ya kimaisha, tulikubaliana kulala pamoja siku ile. Nakiri wazi kuwa, nilikuwa nimepata kinywaji kidogo, hivyo sikuwa na uwezo wa kuamua ni nini kilikuwa sahihi kwa wakati ule. Siku iliyofuatia, niliondoka mapema na kuelekea kazini nikiamini kuwa naye angejiandaa upesi na kurudi nyumbani kwao. Wakati huu akawa amenieleza kuwa, palikuwa ni pale pale mtaani.

Ajabu ni kuwa, jioni ya siku hiyo nilimkuta akiwa bado nyumbani kwangu na alikuwa amenisaidia kufanya kazi nyingi ambazo sikuwa nimezifanya kwa muda mrefu. Nyumba ilikuwa na mwonekano wa tofauti kidogo. Hasira ikayeyuka na kwa mara nyingine akalala nami. Siku ya tatu akaridhia kurudi kwao, lakini mazoea ya kuja kwangu mara kwa mara hayakuisha.

Baada ya kipindi fulani, nilihisi kuwa alikuwa mjamzito na nilipomuuliza, alikiri na kuniambia wazi kuwa, alikuwa anaogopa sana kuniambia kuhusu hilo. Najua mtashangaa kidogo, lakini mwanamke huyu hatukuwa na mazoea ya kuongea mara kwa mara, hata tukiwa nyumbani. Kitabia, yeye ni mkimya kupitiliza nami ni muongeaji, hivyo hili halikuwa gumu kwetu.

Mimba ililelewa yeye akiwa kwao, lakini kutokana na ugumu wa mazingira ya pale kwao, tulikubaliana kuwa wakati wa kujifungua aende akajifungulie kwa dada yangu anayeishi Morogoro. Alijifungua mtoto wa kike ambaye hakuna shaka yoyote kuwa, ni wangu!! Tumefanana zaidi ya ninavyoweza kuelezea, na hili linathibitika zaidi kadiri alivyoendelea kukua.

Baada ya kula uzazi kwa miezi sita, alirudi nyumbani, na ile hofu yangu juu ya mazingira ya kwao [sina haja ya kuuelezea sana ugumu wake], nikapata wazo la kumwacha aishi pale nyumbani kwangu mpaka walau mtoto akue ndipo nijue nafanya nini. Sikuwahi kumwambia kuwa nna mchumba ambaye tuna malengo makubwa, lakini mchumba wangu yule nilimweleza kila kitu na amenisamehe na tunaendelea na mipango yetu, tena anajua wazi kuwa naishi na mwanamke huyu. Nadhani, huenda ananipa nafasi ya kufanya maamuzi magumu. Kiajabu, yeye pia anampenda sana mtoto na amekuwa akimtumia zawadi mara kwa mara.

Sasa ninaishi naye ndani kama SURIA, yani mtu ambaye sina ndoa naye.. Mtoto ana miaka mitatu sasa, na ninampenda sana mwanangu. Nieleweni nisemapo kuwa, sikuwahi kuwa na hisia na mwanamke huyu, ingawa yeye anaonekana wazi kuwa ananipenda sana. Jitihada zote zimefanyika ili kuhakikisha kuwa hatupati tena mtoto mwingine, lakini bado nashindwa kujua kuwa, nawezaje sasa kumweleza kuwa, inabidi aendelee na maisha yake na mimi pia nifanye hivyo. Namtazama mtoto wangu, namwonea yeye pia kama mama wa mtoto huruma, lakini nna malengo yangu makubwa SANA na mchumba wangu ambaye pamoja na makosa makubwa niliyotenda, ameamua kunisamehe na kuwa mtu wa karibu mno kwangu.

Tafadhali wajuzi wa mambo, naombeni sana msaada wa mawazo yenu...
Ifupishe maana sisi ma manager hatuna muda sana wa kusoma paragraph zote
 
Afadhali unisaidie maana watu humu Mmmmh
Hapana mkuuu,hatujui moyo wa huyo mwanamke ila kwa experince zangu Huyo mchumba ake kampenda sana tu mana ingekua ni kumuacha angeweza kumuacha hata saivi,yawezekana hata mchumba wake ana makosa alishayafanya so anaona yeye ni nanai hadi Ahukumu wakati yeye alisamehewa?
 
Hilo ni kosa la kiufundi tu na maamuzi yako yanatakiwa yaangalie utu kwani maisha ni mafupi sana(kufika miaka 100 ni bahati).Kama uko vizuri kiuchumi mjengee nyumba ndogo tu ikiwezekana mpatie biashara itakayomuwezesha kujikimu;baada ya hapo endelea na mtu wako unayemtaka
 
Mkuu historia yako kama yangu, mm nliona mschana enzi hizo yupk form six nikaona ameumbia vizuri. Baada ya miaka 2 nikatafta namba yake, mm nikiwa udsm yy akiwa chuo mkoani. Nikawa naongea naye nikaomba gem akatiki na kuniletea mzigo mabibo hostel. Badae nikagundua alishagegedwa na dogo, basi nikaamua kumpiga chini, ila nikawa nimecheleww maana alikuwa ashabeba mimba alipoona dalili za kibuti. Akazaa mtoto ila kibuti kilimhusu. Nikamove on ila akaja kuniletea mtoto akiwa na 8months kwamba nilee mwanangu. Ilibidi nitangaze ndoa bila kupenda, mpaka leo ni mke wangu. So dogo oa huyo usie mpenda ila yeye anakupenda, utaishi kwa amani sana kuliko kuoa mwanamke unayempenda afu yeye anakuchukulia poa
Yaani kwamba mdogo nae alimla??
 
Mimi nakushauri oa uyo uliyezaa nae uyo ndio mke wa ndoa uyo mwingine ambae mna malengo hewa achana nae
 
Women...
Wachache sana tena Mno kuwaamini, anaweza kwambia yameisha ila.! Siku likilipuka hutakuwa na pakutokea, Mkuu.
 
Hayo malengo makubwa hamishia kwa huyo uliyezaa nae

malengo makubwa hayachagui mtu wa kupanga nae

najua unamdharau kwa kua hana kipato
 
Mmh,yaani nikusamehe ,hapohapo najua bado upo na huyo uliyezaa nae?haiwezekani aiseee!
No,huyo hajakupenda,tusidanganyane!

Oa uliyezaa nae ukimuacha utajuta!
 
Mmmh
Unatujua wanawake vzr wewe?
Be carefully
Mkuu... Huyu ambaye ndiye yuko kwenye plan alivunjika sana moyo pindi alipoujua ukweli. Sikujua kuwa angeweza kunielewa. Lakini amekuwa nami katika kipindi chote. Yeye pia, baada ya kumweleza mazingira ambapo mtoto anaweza kukulia kama nikiachana na mama yake, amekuwa msikivu na mpango uliokuwa awali ukarudi upya.. Hakika sio rahohisi kulielezea hili...
 
Me makushauri mtie kwanza mimba huyo.mvhumba mwengine ile kwanza ujiwekee uwakika kama hyo mwengine ukishamtia mimba ndo anza kufanya nae mipango ya kukaa nae la sivyo nae atakufanyia kitu hutokuja kuamini kama yeye kakufanyia hivyo
Huu sio ushauri mzuri!
Unafikiri kua na watt mama tofauti nayo ni sifa?
Km imetokea kukosea inatakiwa kujifunza sio kufanya kwa nakusudi
 
Sikiliza wewe kijana. Acha kuchezea wanawake utakuja kujuta. Nitakupa kisa fulani kidogo tu. Kuna rafiki yangu fulani aliajiriwa huko kanda ya ziwa. Baada ya kuona maisha ya kupika ni taabu akajipatia house girl wa kisukuma tena mkubwa tu na wakati huo alikuwa na mchumba wake aliyekuwa akija kumtembelea. House girl naye hakuwa mjinga kwani kwa ushawishi wa wapambe aliweza kumtega jamaa mpaka akawa anagonga vitu. Zoezi hilo liliendelea kwa muda mrefu tu. Shida ilikuja pale alipomwambia arudi kwao kwani kipindi cha kufunga ndoa na mchumba wake kimekaribia. Ndani ya wiki hiyohiyo jamaa aliugua kwikwi mfululizo ambayo ilimuondoa duniani. Hakuna mwenye uhakika kama binti yule alihusika au la. Hivyo chukua tahadhali kijana. Acha kucheza na hisia za wanawake.
duh
 
Ouky Kama hauna hisia nae mtengenezee mama yake (mzazi mwenzio ) maisha ili aweze kumuhudumia mtoto pale utakapo muacha.... Huwezi kulazimishwa kumpenda mtuu ila jali damu yako mgungulie biashara au mtafutie kazi then muachie nyumba mnayokaa uondoke na nguo zako tuu uende kwa uyo mchumba ako wa zamani
Huyu muongo Bwana, anazo hisia,asingekua Nazo asingeweza kuishi nae zaidi ya miaka 3!
 
Kuzaa na mwanamke mwingine kusamehewa inawezekana. Lakini kumruhusu baada ya kumzalisha waendelee kuishi nyumba moja na yeye hayupo... I can't buy that.. Kamwe.
Yaani nashangaa!
Basi huyo mdada sio wa kawaida
 
Habari wana jamvi...

Natamani sana kupata msaada, uwe wa kimawazo, kisheria ama hata kiuzoefu tu katika hili ninalolipitia. Miaka mitatu iliyopita, nilikutana na mwanamke fulani ghafla tu, [ingawa badae niligundua kuwa tulikuwa tukiishi mtaa mmoja] na pasipo hata makubaliano yoyote ya kimaisha, tulikubaliana kulala pamoja siku ile. Nakiri wazi kuwa, nilikuwa nimepata kinywaji kidogo, hivyo sikuwa na uwezo wa kuamua ni nini kilikuwa sahihi kwa wakati ule. Siku iliyofuatia, niliondoka mapema na kuelekea kazini nikiamini kuwa naye angejiandaa upesi na kurudi nyumbani kwao. Wakati huu akawa amenieleza kuwa, palikuwa ni pale pale mtaani.

Ajabu ni kuwa, jioni ya siku hiyo nilimkuta akiwa bado nyumbani kwangu na alikuwa amenisaidia kufanya kazi nyingi ambazo sikuwa nimezifanya kwa muda mrefu. Nyumba ilikuwa na mwonekano wa tofauti kidogo. Hasira ikayeyuka na kwa mara nyingine akalala nami. Siku ya tatu akaridhia kurudi kwao, lakini mazoea ya kuja kwangu mara kwa mara hayakuisha.

Baada ya kipindi fulani, nilihisi kuwa alikuwa mjamzito na nilipomuuliza, alikiri na kuniambia wazi kuwa, alikuwa anaogopa sana kuniambia kuhusu hilo. Najua mtashangaa kidogo, lakini mwanamke huyu hatukuwa na mazoea ya kuongea mara kwa mara, hata tukiwa nyumbani. Kitabia, yeye ni mkimya kupitiliza nami ni muongeaji, hivyo hili halikuwa gumu kwetu.

Mimba ililelewa yeye akiwa kwao, lakini kutokana na ugumu wa mazingira ya pale kwao, tulikubaliana kuwa wakati wa kujifungua aende akajifungulie kwa dada yangu anayeishi Morogoro. Alijifungua mtoto wa kike ambaye hakuna shaka yoyote kuwa, ni wangu!! Tumefanana zaidi ya ninavyoweza kuelezea, na hili linathibitika zaidi kadiri alivyoendelea kukua.

Baada ya kula uzazi kwa miezi sita, alirudi nyumbani, na ile hofu yangu juu ya mazingira ya kwao [sina haja ya kuuelezea sana ugumu wake], nikapata wazo la kumwacha aishi pale nyumbani kwangu mpaka walau mtoto akue ndipo nijue nafanya nini. Sikuwahi kumwambia kuwa nna mchumba ambaye tuna malengo makubwa, lakini mchumba wangu yule nilimweleza kila kitu na amenisamehe na tunaendelea na mipango yetu, tena anajua wazi kuwa naishi na mwanamke huyu. Nadhani, huenda ananipa nafasi ya kufanya maamuzi magumu. Kiajabu, yeye pia anampenda sana mtoto na amekuwa akimtumia zawadi mara kwa mara.

Sasa ninaishi naye ndani kama SURIA, yani mtu ambaye sina ndoa naye.. Mtoto ana miaka mitatu sasa, na ninampenda sana mwanangu. Nieleweni nisemapo kuwa, sikuwahi kuwa na hisia na mwanamke huyu, ingawa yeye anaonekana wazi kuwa ananipenda sana. Jitihada zote zimefanyika ili kuhakikisha kuwa hatupati tena mtoto mwingine, lakini bado nashindwa kujua kuwa, nawezaje sasa kumweleza kuwa, inabidi aendelee na maisha yake na mimi pia nifanye hivyo. Namtazama mtoto wangu, namwonea yeye pia kama mama wa mtoto huruma, lakini nna malengo yangu makubwa SANA na mchumba wangu ambaye pamoja na makosa makubwa niliyotenda, ameamua kunisamehe na kuwa mtu wa karibu mno kwangu.

Tafadhali wajuzi wa mambo, naombeni sana msaada wa mawazo yenu...
Braza kitu unachotaka kukosea sana ni kuzaa mtoto alaf na kumtelekeza mamayake kwa kumuoa mwanamke mwingine, hakika unatengeneza bomu kuubwa ambalo haujui athari zake katika maisha ya familia yako na maisha ya mtoto wako na mke utakae muoa,

nduguyangu nikushauri kwamba yule usiye mpenda wewe ndiye mwanamke wa ukweli ambaye kaja kwenye maisha yako ili kukupa mabadiliko chanya, mjenzi wa familia na maisha kiuchumi kwa ujumla na ndiye yeye anae kupenda na anajua nin maana ya upendo kwako,,,

Na huyo unaye mtaka wewe baada ya kumuoa na kumfukuza huyu uliye kwisha kuzaa nae, atakuatu consumer na asiye jari, atakua mwiba wa mti wa mkenge,

hebu jitahidi basi uwe na upendo kwa mwanao, jitahidi kuvaa viatu vya mwanamke huyu imagine ungalikua niwewe ingekua vipi!!!


Mtoto huyo katika maisha ya uzee wako huenda ndo atakaye kua malaika wako!! Jitahid kumpenda mtoto na mama wa mtoto pia, mjari, ila pia muoe.

"We don't recognize the value of water in the pond until it get dry"
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom