Naionya China, isijaribu

Naionya China, isijaribu

🤣🤣🤣🤣 umenichekesha na kunikumbusha mbali. Mpiganaji anarusha ngumi bila kuangalia mbele, yani anavurumisha tu utafikiri anarusha kota.
Hahahaha na risasi zao za "Tyu...Tyu..Tyuu!" Ngumi za uwongo sana
 
Kwa upande wa Russia

1. Alivyomega Crimea sio mabeberu walifurahia, waliruhusu aimege kisha wakalaani kinafki, media zikafunguliwa kumsifia Putin ni mbabe. Asichokijua ni kwamba, walikuwa wanamjaza ili baadae aingie na Ukraine. Hatimae kajaa kweli Ukraine, anatamani kutoka ila akitazama anaona ni aibu nzito kwake.

2. Leo watu wanasifia Russia kuchukua majimbo, wanasahau kuwa mwezi wa 3 au wa 4 nchi za Magharibi zimepanga kutoa bajeti ya vita hii kwa muda wa miaka 5.

3. US akasema kuwa nia yake kule Ukraine ni kutaka Russia atumie muda mwingi ktk hii Vita. Tumesahau hii kauli ya Biden?

HITIMISHO

Russia atachukua miji na vijiji lakini baada ya muda Ukraine itavikomboa tena. Rejea Ukraine alivyoikomboa Kharkiv, Snake Island na sasa Kherson inakaribia kukombolewa.

Hii yote ni kumchosha Russia. Hata hizi kelele Ulaya wanazopiga mfumuko wa bei, kwao wanajua ni kipindi cha muda tu, tayari walishajipanga kukabiliana na Russia.

CHINA V TAIWAN.

Moja ya vitu nisivyovifikiria ni China kuingia Vitani, China ana majirani ambao akiingia Taiwan na akadhoofika kwa namna yoyote ile, basi muda huohuo India na Japan wanaweza nao wakawasha moto hapo China.

India na Japan hawa wana uwezo kabisa wa kuikalisha serikali ya China totally. Hizi nchi mbili teknolojia zao ktk silaha zao za kivita ni nzuri kuliko mchina.

Mziki wa India na Japan sio wa kitoto.
Mkuu

Unaijua sana situation ya China

India na Japan wana long time beef na China na wanasubiri tu aingie mkenge,China atakalishwa vibaya na viutajiri vyake vyote vitabebwa!

Huku upande wa West China an ugomvi na India wa siku nyingi kwa ubabe wake wa kujimegea eneo la India...huku upande wa east kuna Japan ana beef na China la kihistoria na wanagombea visiwa..pia na Taiwan

China ana beef na majrani zake wote 32 na bahari nzima ya South China Sea....Rafiki yake ni mmoja tu pande hizo,North Korea.

Russia mwenyewe kwa upande wa Kaskazini wana beef na China la kitambo sana la eneo la Russia China alijimegea,japo ni marafiki kwa sasa,kikiwaka I doubt kama Russia atakua rafiki wa kweli maana sasa ilitegemewa China asaidie ila kauchuna kama hayupo vile.

China anatafutwa na watu kibao yaani.....na kama akibugi akadhani ni Taiwan tu,basi anafeli..maana hataweza kabiliana na vurugu pande zote za nchi kwa wakati mmoja....watamkamua akauke,we subiri tu
 
Mkuu

Unaijua sana situation ya China

India na Japan wana long time beef na China na wanasubiri tu aingie mkenge,China atakalishwa vibaya na viutajiri vyake vyote vitabebwa!

Huku upande wa West China an ugomvi na India wa siku nyingi kwa ubabe wake wa kujimegea eneo la India...huku upande wa east kuna Japan ana beef na China la kihistoria na wanagombea visiwa..pia na Taiwan

China ana beef na majrani zake wote 32 na bahari nzima ya South China Sea....Rafiki yake ni mmoja tu pande hizo,North Korea.

Russia mwenyewe kwa upande wa Kaskazini wana beef na China la kitambo sana la eneo la Russia China alijimegea,japo ni marafiki kwa sasa,kikiwaka I doubt kama Russia atakua rafiki wa kweli maana sasa ilitegemewa China asaidie ila kauchuna kama hayupo vile.

China anatafutwa na watu kibao yaani.....na kama akibugi akadhani ni Taiwan tu,basi anafeli..maana hataweza kabiliana na vurugu pande zote za nchi kwa wakati mmoja....watamkamua akauke,we subiri tu
Angalau umeleta historia inayofikirisha mkuu. Mchina kwa sasa amekalia kuti kavu.
Akilikata ataanguka mwenyew.
 
Una hoja nzuri.

Wengi wanaona US akiingia vitani na washirika wanahisi US ni weak. Wanashindwa kutambua jamaa anatazama unafuu wa kupambana ktk vita.

Ni mjinga pekee anayedhani Uchumi wa Russia bado uko imara kutokana na vikwazo alivyowekewa. Kila siku nasemaga humu ndani, laiti vyombo vya habari huko Russia vingefunguliwa na kuwa huru kama Ulaya, basi tungesikia mengi zaidi huko Urusi.
Warejee vita yetu na Uganda badala ya kufunga mkanda miezi.18 hadi sasa mwamgwi upo
 
Wewe uliitegemewa urusi wakubali kwamba wamefurushwa huko snake island???
Ni lini urusi ilikubali kuwa imeshindwa ??

Waliposhindwa kuiteka Kyiv baada ya kupewa kipigo kikali,walikimbilia Huko Donbass huku wakidai kuwa wamejiondoa Kyiv baada ya makubaliano maalum

Hata ikitokea wakafurushwa huko Donbass watakwambia wamejiondoa baada ya kukamilisha operation maalum ya kijeshi, Russia hajawahi kukosa sababu yule
Sasa nikuulize, ingekua Ukraine walikomboa snake Island, kwanini kupitisha meli za nafaka ni ruhusa ya Urusi, fatilia vizuri, kijana, Russia ilitoka snake Island ili kuruhusu meli zianze kupitisha ngano
 
Aliyeanzisha vita vya Ukraine ni Putin na Urusi yake sio Marekani, asilimia 70 uliyoandika ni kweli, 30 zilizobaki ni porojo na propaganda tu.
 
Kumpinga dikteta ni hatari sana, wengi waliojaribu kumpinga Putin wameishia kunywa chai zenye polonium, kupigwa risasi, ajali zisizoekewaka, vifungo vya muda mrefu gerezani au kukimbilia uhamishoni West
Kabisa mkuu, nchi za kidikteta mara nyingi maamuzi yao huwa ni ya mtu mmoja alie mbele ya mstari. Hata kama kuna athari mbele yao wao wataenda tu ili mradi watekeleze matakwa ya dikteta wao.
 
Dikteta Stalin wa USSR alijaribu kuimaliza Ukraine kwa mauaji ya kimbari ya Holodomor mwaka 1932-1933 akashindwa kuimaliza japo aliua mamilioni ya Wa Ukraine. Ukraine ni wagumu na wapambanaji haswa sio rojo rojo kama nyie.
Kwa hiyo una uhakika kwamba Ukraine itakuwepo hadi kufikia hiyo miaka mi 5.
 
Russia haifanyi maamuzi kutokana na think tanks au strategists bali kutokana na anavyojisikia dikteta Putin.
Yaani wewe kwa akili yako na upeo wako unahisi umewazidi think tank na strategist wa Russia?? Kwamba wewe umeona mtego halafu wao hawajaona??? Msipende kuleta ujuaji kwa vitu ambavyo ukweli halisi hatutakuja kuufahamu kwa sasa!!!!
Nb: Dunia inaongozwa kwa siri sana.Mimi na wewe hatuzifahamu.
 
Hakuna kiongozi kama Mao atakayeiongoza China tena, Mao alipotea na ujamaa wake kabisa na haitajirudia hiyo historia mbovu ya China ya zamani baada ya kuonja utamu wa kibepari.
Mimi kwa maoni yangu naona China kwa Sasa inamuhitaji Rais mwenye kaliba ya Chairman Mao Zedong ili kukamilisha mission ya Taiwan Unification.
 
Kumbuka America ilivyochapwa na Vietcong wakakimbia Saigon miaka ya 70's, na mwaka jana 2021 wakafukuzwa Afghanistan na Taliban kwa aibu kubwa! Waamerika wanataka kuogopwa na watu kama were mleta uzi huu, ili waitawale DUNIA, na kusambaza sera za unyonyaji, ushoga, kuruhusu mihadarati n.k.
 
Back
Top Bottom