Naionya China, isijaribu

Naionya China, isijaribu

Kwa sababu alikuwa na uthubutu na maamuzi magumu.hawa wa sasa ni waoga sana tokea utawala wa Deng Xiaoping mpaka Sasa Xi Jinping sijaona mtu mwenye uthubutu Kama Chairman Mao Zedong labda mbeleni watabadilika . Taiwan kurudi China inahitajika maamuzi magumu na uthubutu wa hali ya juu.
Ungekuwa wewe ungeweza mkuu? Unadhani wote wale waliomzunguka Rais na kumwambia awe mpole ktk hili unafikiri wamependa kuwa uoga? Kuna muda busara na upole ni silaha kubwa kuliko bunduki.

Sakata la Ukraine ni taswira nzuri kwa China juu ya kuingia Taiwan. Taiwan anaweza akamshusha China kiuchumi akarudi nyuma zaidi endapo akavamiwa. Hili wameliona vyema serikali ya China.
 
Kwa upande wa Russia

1. Alivyomega Crimea sio mabeberu walifurahia, waliruhusu aimege kisha wakalaani kinafki, media zikafunguliwa kumsifia Putin ni mbabe. Asichokijua ni kwamba, walikuwa wanamjaza ili baadae aingie na Ukraine. Hatimae kajaa kweli Ukraine, anatamani kutoka ila akitazama anaona ni aibu nzito kwake.

2. Leo watu wanasifia Russia kuchukua majimbo, wanasahau kuwa mwezi wa 3 au wa 4 nchi za Magharibi zimepanga kutoa bajeti ya vita hii kwa muda wa miaka 5.

3. US akasema kuwa nia yake kule Ukraine ni kutaka Russia atumie muda mwingi ktk hii Vita. Tumesahau hii kauli ya Biden?

HITIMISHO

Russia atachukua miji na vijiji lakini baada ya muda Ukraine itavikomboa tena. Rejea Ukraine alivyoikomboa Kharkiv, Snake Island na sasa Kherson inakaribia kukombolewa.

Hii yote ni kumchosha Russia. Hata hizi kelele Ulaya wanazopiga mfumuko wa bei, kwao wanajua ni kipindi cha muda tu, tayari walishajipanga kukabiliana na Russia.

CHINA V TAIWAN.

Moja ya vitu nisivyovifikiria ni China kuingia Vitani, China ana majirani ambao akiingia Taiwan na akadhoofika kwa namna yoyote ile, basi muda huohuo India na Japan wanaweza nao wakawasha moto hapo China.

India na Japan hawa wana uwezo kabisa wa kuikalisha serikali ya China totally. Hizi nchi mbili teknolojia zao ktk silaha zao za kivita ni nzuri kuliko mchina.

Mziki wa India na Japan sio wa kitoto.
Snake island ilikombolewa na Ukraine et, pumba kabisa.
 
Tena mobilization zenyew zimefanyika baada ya Pelosi kutoka tayari ndani ya Taiwan. Watu ambao wanaweza kufanya kile wanachomaanisha na hata marekani inajua kama haiwezi kuwafanyia mzaha kama huu ni Iran na pengine North Korea.
Hao wawili hawana impact kwenye soko la dunia. So, simply hawana cha kupoteza wakikorofishana na nchi nyingine.
 
Snake island ilikombolewa na Ukraine et, pumba kabisa.
Wewe uliitegemewa urusi wakubali kwamba wamefurushwa huko snake island???
Ni lini urusi ilikubali kuwa imeshindwa ??

Waliposhindwa kuiteka Kyiv baada ya kupewa kipigo kikali,walikimbilia Huko Donbass huku wakidai kuwa wamejiondoa Kyiv baada ya makubaliano maalum

Hata ikitokea wakafurushwa huko Donbass watakwambia wamejiondoa baada ya kukamilisha operation maalum ya kijeshi, Russia hajawahi kukosa sababu yule
 
Screenshot_20220806-131237.jpg
 
Ungepasa kujua wakati wa Mao Zedong China ilikuwa ni tishio kwa kiasi gani kwa marekani kwa maeneo ya Asia ya mbali. Bila ya Mao Zedong Korea kaskazini isingekuwepo mpaka Sasa.
Mkuu nakubaliana na ww kwa namna fulani, lkn pia ujue kwamb Marekani nayo imekuwa na uzoefu wa miaka mingi wa ku deal na watu wa aina hiyo. Tuliona kilichotokea kwa akina Fidel Castor, Sadam Hussein nk.

Kifupi USA na washirika wake walijiandaa muda mrefu kukabiliana na nchi au viongozi wenye mitazamo tofauti na yao. Na mwisho huwa mbaya kwa hizo nchi afu viongozi wao. Korea Kaskazin leo hii milo mitatu kwa siku inaliwa na maofisa wa Ikulu tu peke yake, huku wananchi wa kawaida wakishindia mlo mmoja kwa siku, Iraq tuliona walivyo deal na Sadam baada ya kumlia taiming muda fulan, Cuba hadi ilifika kipindi wenyew wakaomba poo ili angalau waweze kuwaondolea robo ya vikwazo ili wapate pesa za kuwalipa watumishi wa serikali baada ya serikali yao kufilisika.

So hawa watu wakiamua lao, kweli unaweza ku savaivu miezi au miaka kadhaa kama vile Iran, but one day utajikuta umeingia kwenye 18 zao tu. CIA huwa hawalali kwa sababu ya mission za namna hii.
 
Shida iliyopo US wanategemea bidhaa za china, kuanzia chupi hadi mitambo,, sababu viwanda vilihamia china kukwepa gharama za uzalishaji marekani,
Yani hadi sasa US alichobakiwa nacho kijeuri ni noti za hela tu. Ila ana shortage ya resources na bidhaa zitaenda kuwa adimu hasa anazozalisha china.
 
Sasa hao watu wengi ikawaje wakashindwa jua Pelosi anaenda Taiwan hadi waliposikia kwenye vyombo vya habari, ndo wakaanza mobilization ya vifaa?
Vikwazo Kwa warusi SII jambo geni na ndio maana wapo tayari kupambana na mabeberu na kutafuta ushawishi duniani Kwa gharama yeyote,mwanajeshi kufa vitani ni sehemu ya kazi kama ilivyo kazi zingine na porojo za beberu wala hazimtishi kwani adui hukuombea njaa siku zote🤔
Mzee baba ameshasema operation lazima ifanikiwe kwa namna yeyote ile hata kama itaendelea hadi kiama😂😂😂
 
Vita urusi imepata faida hasa kuyachukua maeneo muhimu kama kinu kikubwa kabisa cha nuclear hapo ulaya na sehemu zenyewe migodi mingi na viwanda vingi hapo urusi imechukua karibu asilimia 95 la eneo lote la kulima ngano hapo Ukraine

Upande WA vikwazo kila mtu ni shahidi vikwazo vimewapiga wao kuliko hata urusi na kupelekea regime change

Ukweli mchungu hii vita West wameishiwa mbinu hata himars zimeshindwa kufua dafu kwa urusi ha ha ha ha ha ha ha ha ha Putin aliletwa kuwashughulia hawa wapuuzi WA West
Hahahaha halafu kuna Kenge wanasema urusi kala hasara 😂😂😂
 
Nakupongeza mkuu. Maana Ni Kama upo ndani ya fikra na akili zangu . Kwa 100% Umeiongelea mawazo yangu pia kuanzia mwanzo mpaka Mwisho ulipo hitimisha.

- Ni kweli kabisa mkuu utofauti wa itikadi usitufanye tusipeane nafasi za kusikilizana kwa ajili ya manufaa ya taifa hili ndio maana hata Mimi Ni mpenzi wa falsafa za kijamaa lakini katu siwezi kutokumsikiliza na kumtilia maanani mtu eti kisa yeye ni mpenzi wa falsafa za kibepari la hasha sipo hivyo ndio maana napenda kuona taifa letu lisijengwe katika misingi ya kwamba ni taifa la kijamaa 100% au taifa la kibepari 100% hapana tunapaswa kufungua mlango kwa yote yenye faida tu yapatikanayo ndani ya ujamaa kuingia nchini kwetu na kujenga nchi yetu vivo hivyo tunapaswa kufungua mlango kwa yote yenye faida yaliyo ya kipebari kuingia nchini kwetu na kujenga nchi yetu . Kwa kuwa kiukweli kabisa sisi Kama TANZANIA tumechelewa tena tumechelewa Sana tupo nyuma kweli kweli kimaendeleo wakati matifa ya Asia ya mbali na mataifa ya magharibi yapo mbali kimaendeleo sisi bado tupo nyuma ni Kama wao tayari Ni watu wazima katika maendeleo Ila sisi ndio kwanza tumezaliwa kimaendeleo hata hatua za kuanza kutambaa kimaendeleo hatujaanza hivyo yatupasa kuwakimbilia wao walipo kadili tuwezavyo . Tunahitaji kuwa na kizazi Cha vijana shupavu na wenye kujitambua na sio mradi tuna vijana , vijana shupavu na wenye kujitambua ni mtaji tosha wa kufufua uchumi wetu na kuukuza na pia ndio kichocheo cha mabadiliko nchini.

- Taifa letu lina vijana wengi Sana hilo halipingiki lakini je tujiulize je hao vijana Ni vijana wenye faida kwa taifa ? Ni vijana wenye kujitambua na kujua jukumu lao kwa TANZANIA Ni lipi? Au ndio tunavijana wengi lakini Ni wajinga, wapumbavu, washenzi, wahitimu badala ya wasomi , wanaowaza umbea kuliko Mambo ya msingi , walioendekeza ngono, wasiojikita na kujishughulisha na Mambo ya msingi Ila ni watu wanaopenda kufuatilia na kuyapa nafasi Mambo ya kijinga na ya kipumbavu yanayo tokea katika Taifa letu Ila mambo ya msingi wao kujishughulisha nayo ni ukoma, vijana waliojikatia tamaa kimaisha.

- Taifa letu linahitaji vijana walio na afya ya akili wenye kujitambua na kujua Tanzania inahitaji nini kufanyiwa na sio kuiacha inaendelea kuzama hivi hivi taratibu kuliko kuinuka na kukimbizana na waasia ya mbali na wamagharibi.
Kabla hujafikia kwa vijana hao hio safu ya viongozi na mifumo ambayo inaakisi unachofikiria je wapo?
 
Kabla hujafikia kwa vijana hao hio safu ya viongozi na mifumo ambayo inaakisi unachofikiria je wapo?
Ni kweli Kama taifa tuna matatizo chungu mzima kuhusu mfumo wa kiutawala na kisiasa . Jambo ambalo ni Kikwazo kwa zaidi ya 60% wa upigaji hatua wetu kwenye safu ya maendeleo. Yatupasa kwanza kabla ya yote tubadili mfumo mzima wa kiutawala na kiuongozi katika taifa letu na tuweke mazingira Safi na yaliyobora kwenye tawala na siasa za nchi ili tuweze kuvuna mavuno yaliyo bora ya vijana waliomo nchini . Kwa kuwa utawala bora na siasa safi zitashiriki kwa kiwango kikubwa katika upandaji wa mbengu bora za vijana shupavu na waliobora na mazao hayo ya vijana yatalilisha taifa letu maendeleo makubwa sana.
 
India nao wana mtei anaitwa Amitah Bachan au Dharmenda mzee wa kishipa, unafikiri hao wakiungana hawawezi kumdhibiti tai chii na genge lake 🤣🤣🤣🤣
Hahahah Amita Batchan na San Deo wazee wa ngumi za "Dushwaa"
 
Back
Top Bottom