Kaka Kwa mm navyoona Mchina ameogopa VIKWAZO ili gap kati yake na USA isiongezeke.
Ngojea nkutajie baadhi ya sancs ambazo USA alijaribu kuweka Kwa China na akashindwa;
1)kuiwekea vikwazo Huawei isitumie google lengo ni kuua soko la simu la China ila China alizi improve Oppo,Xiaomi na vivo na alikua na mpango wa kuanzisha OS yake USA wakamuondolea vikwazo,pia alizuia cheap skilled labors wa China kutengeneza iphone na soko la iphone China likawa doomed.
2)Kuweka ushuru mkubwa katika bidhaa za China ziingiazo USA,China nae aliongeza ushuru maradufu Kwa USA mnamo 2018 USA ikapunguza ushuru.
Pia alitishiwa kuwekewa vikwazo km atai contain south china sea kijeshi ila alifanya na USA wakashindwa kumuwekea vikwazo.
Kiufupi kaka China yenyewe Ina soko kubwa maana Ina raia takriban bilioni mbili.
Pili China soko lake kubwa ni maeneo ambayo population ya Dunia ndio imeelemea (Africa,Asia,South America) tukubali tukatae huko ndio population ya Dunia ilipoelemea na China ndio kakamata soko.
mwaka Jana walitoa ripoti bank ya China imekopesha takriban mataifa 128 km sijakosea ulimwenguni kote na pia ameyasamehe mataifa 38 madeni bro unapoweka vikwazo lazima na wa pembeni waitikie vikwazo.
China ni taifa muhimu sana ulimwenguni hakuna taifa au bara litakalokubali vikwazo dhidi ya China.
Mfano wa mwisho Von derleyen mwenyekiti wa EU alitoa wito alisema mzozo kati ya USA na China kuhusu Taiwan utatuliwe kidiplomasia maana hao watu wakiingizana kimabavu Dunia itaumia.
Hususan Asia na Afrika.
Unayoongea mengi nakubaliana nayo kaka, ndio maana ukisoma mwanzo wa thread yangu nilizungumzia hiki hiki ambacho kinafanya China wasiingie vitani.
I mean niliishauri China isiingie mtegoni kwa kuivamia Taiwan kijeshi, maana itakuwa imefanya kosa kubwa katika maisha yake yote.
Najua China ni Super Power wa tatu kidunia baada ya US na Russia. Pia ni ya pili kiuchumi duniani baada ya US,
lakini halingani ushawishi na Marekani kwahiyo hilo litam cost sana.
Nakupa mfano wa nchi zilizowekewa vikwazo vikubwa na vidogo vya kiuchumi na marekani jinsi zinavyohangaika kuinua upya chumi zao lkn inashindikana. Angalia baadhi ya nchi kama Venezuela, Cuba, Iran, North Korea nk zilivyo na hali mbaya kiuchumi, mpaka zinajaribu kutafuta njia bora ya kuifanya Marekani iondoe au pengine ipunguze vikwazo hivyo vinavyoathiri kwa kiwango kikubwa chumi zao.
Marekani imekuwa ikitoa mamilioni ya dola kuzisaidia baadhi ya nchi za ulaya ktk maswala ya kijeshi, kiuchumi nk, moja ya nchi hizo ni Ujerumani ambapo wakati Trump anaingia madarakani alipunguza msaada huo kwa madai kwamba Ujeruman kwa sasa ni miongoni mwa nchi zinazojiweza kiuchumi.
Hapo sijazungumzia nchi za Afrika, baadhi ya nchi za Asia na mabara mengine.
So suluhisho zuri ktk hili ni kuacha vita tu kaka maana italeta athari kubwa kwa kila mmoja wetu. Na sio China, Taiwan au USA peke yake.