Komeo Lachuma
JF-Expert Member
- Oct 31, 2014
- 5,360
- 11,507
Huwa namfuatilia mbunge wa Mbeya Mjini Dr. Tulia huyu pamoja na Ubunge ni Naibu Spika ni msomi mzuri wa Sheria. Lakini kiukweli akili ya kisiasa hana kabisa toka anajindaa kuwa Mbunge mpaka anakuwa Mbunge hakuna mambo ya maendeleo ya maana anayoyafanya. unamwona anaangaika na petty issues za kusaidia vijitimu vya mpira, ngoma, utamaduni na mambo madogo madogo yasiyo na tija kwa Mkoa wa Mbeya.
Inahuzunisha sana kuwa anakosa kushughulikia suala la Msingi la kujengwa Tawi la Chuo Kikuu Mbeya kwa kufanikisha na viongozi na wakazi wa Jiji kutoa Uwanja wa Kutosha kwa ajili hiyo ila unamwona anacheza cheza tu kwenye matamasha na sherehe mbalimbali. yaani mambo madogo anayafanya makubwa na mambo makubwa anayafanya madogo.
Ni aibu sana kwa mtu msomi kama yeye na exposure aliyo nayo kushindwa kujua mahitaji ya msingi kwa Mkoa wa Mbeya ni nini. Kila mara utamwona akicheza cheza kwenye matamasha na sehemu mbali mbali na kutoa vimichango mbuzi vya jersey, vifaa vya michezo n.k akisahau mambo muhimu ya msingi kwa ajili ya maendeleo akama shule, hospitali, zahanati, vyuo, barabara au miundo mbinu, mipango mji n.k anazunguka zunguka tu kula bata haonekani akifanya jambo la msingi JIJINI MBEYA. yaani huyu Mbunge ni Gunzi Kabisa.
Inahuzunisha sana kuwa anakosa kushughulikia suala la Msingi la kujengwa Tawi la Chuo Kikuu Mbeya kwa kufanikisha na viongozi na wakazi wa Jiji kutoa Uwanja wa Kutosha kwa ajili hiyo ila unamwona anacheza cheza tu kwenye matamasha na sherehe mbalimbali. yaani mambo madogo anayafanya makubwa na mambo makubwa anayafanya madogo.
Ni aibu sana kwa mtu msomi kama yeye na exposure aliyo nayo kushindwa kujua mahitaji ya msingi kwa Mkoa wa Mbeya ni nini. Kila mara utamwona akicheza cheza kwenye matamasha na sehemu mbali mbali na kutoa vimichango mbuzi vya jersey, vifaa vya michezo n.k akisahau mambo muhimu ya msingi kwa ajili ya maendeleo akama shule, hospitali, zahanati, vyuo, barabara au miundo mbinu, mipango mji n.k anazunguka zunguka tu kula bata haonekani akifanya jambo la msingi JIJINI MBEYA. yaani huyu Mbunge ni Gunzi Kabisa.