Nahisi nimetapeliwa sijui nifanye nini?

Nahisi nimetapeliwa sijui nifanye nini?

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Hatari mimi jamaa angu alikuta sony tv nch 55 akauziwa laki 5 mpaka leo ile tv haiwashi maana akiwasha tu lazima umeme wa 10000 uishe kwa siku na akati umeme wa 10000 anatumia siku sita
 
Mpambanie atoke, pesa mtatafuta nyingine tu
Matapeli hawaishi na wajinga pia hawaishi.
Jana wife kapigwa 760,000 kwenye laini za miamala na wale jamaa wanaoipigaga simu.
Yaani licha ya kumpa elimu yote huko nyuma kuwa asije akajaribu kuelekezwa kitu na akafanya kwenye simu za miamala bado alinasa tu.
Hv kalazwa yuko hospitali yaan hasara mara 2.
Damn Dunia ni chungu hii wakat mwingine
 
Yaani kwa kujua hilo niliwaambia hata kwa namna yoyote ile asije mtu akakwambia sijui bonyeza namba flani kwenye simu usikubali.Nikawaambia na namba ni 100 tu zingine ni utapeli.
Tena niliwaasa kama kunatakiwa marekebisho yoyote msifanye chochote mpaka mnitaarifu.
Ila ajabu hata moja hakukumbuka. Kapigiwa simu kwenye namba za miamala baadae wakamwambia kuna marekebisho ya mtandao tunafanya kwa mawakala,wakaomba na namba yake kawapa.
Wakampigia kwa namba yake huku wanamwamuru abonyeze anachoelekezwa kwenye namba ya wakala.Yaan watu ni wa tigo wakampitisha tigopesa kawatumia wakaja voda napo kawatumia halotel katuma mpaka kumaliza hela damn!
Iliwahi kutokea kwa shemeji yangu vivyo hivyo uliyosimulia tena biashara ya brother alikua na ofisi mbili kipindi hicho nikawa namsaidia saidia siku kaingia pale yani anaulizwa tigo una kiasi gani? tuma...same kwa laini zote,watoto wa kike wakati mwingine kipengele sana
 
Habar za humu wanajamvi? Ilikuwa siku ya jumamosi natoka kwenye harakati za vikao na clients wangu basi nikapita pale mwenge mpakani kulikuwa na mnada wavitu wakidai muuza duka alichukua mkopo kashindwa rejesha so vitu vya dukani vikawa vinapigwa mnada.
Basi pale nikaona simu aina ya IPhone 11 Pro max ambayo bei zake huwa ni 1.7m dukani,basi nikaikagua ile simu nikaona kama ipo poa basi nikatamka offer yangu 500,000tsh nikachukua baadae nafika home nakuta sio IPhone kabisa bali wameweka os inayoendana na iPhone isee nilichoka. Sasa je ninaweza kwenda kwenye mamlaka gani inisaidie nipate hela yangu maana hapo nimetapeliwa. Nina risiti ya efd na ya kawaida
Nenda Mombasa central police station.
 
Iliwahi kutokea kwa shemeji yangu vivyo hivyo uliyosimulia tena biashara ya brother alikua na ofisi mbili kipindi hicho nikawa namsaidia saidia siku kaingia pale yani anaulizwa tigo una kiasi gani? tuma...same kwa laini zote,watoto wa kike wakati mwingine kipengele sana
Yaani sijui wanawaza nini.Kuanzia sasa nitakuwa msiri sana na mambo ya pesa zangu.Hawa watu ukiwaamini ndani ya siku moja wanakufilisi unarudi kulima town.
 
Dah mwaka 2008 nilikaribishwa mjini.. Kipindi hicho ndo naanza chuo, nikapita pale ubungo nikakuta wananadi simu na shati kwa elf 8 [emoji3][emoji3]
Visimu hivi vya batani, masharti ni utatestia kwenu.. Nikajisemea sio mbaya hata kama simu mbovu basi nitapata shati, shati lenyewe liko sealed.

Dah nafika hostel, kutest simu hamna kitu.. Shati nalo sio shati linaishia kifuani.. Ikabidi nibaki nalo moyoni tu ila tamaa ziliniponza, sijawah msimulia mtu ule ujinga wangu ndo kwa mara ya kwanza naandika hapa!
 
Dah mwaka 2008 nilikaribishwa mjini.. Kipindi hicho ndo naanza chuo, nikapita pale ubungo nikakuta wananadi simu na shati kwa elf 8 [emoji3][emoji3]
Visimu hivi vya batani, masharti ni utatestia kwenu.. Nikajisemea sio mbaya hata kama simu mbovu basi nitapata shati, shatg lenyewe liko sealed.

Dah nafika hostel, kutest simu hamna kitu.. Shati nalo sio shati linaishia kifuani.. Ikabidi nibaki nalo moyoni tu ila tamaa ziliniponza, sijawah msimulia mtu ule ujinga wangu ndo kwa mara ya kwanza naandika hapa!
Hahahahhahaha...we kiboko..shati ununue ubungo🤣🤣! Dah..mimi sinaga tamaa kbs yaani...hata kuwasikiliza huwa sina huo muda...dah..maduka ya simu yapo ajabu mtu ananunua simu kitaa🤣🤣🥺🥺
 
Yaani sijui wanawaza nini.Kuanzia sasa nitakuwa msiri sana na mambo ya pesa zangu.Hawa watu ukiwaamini ndani ya siku moja wanakufilisi unarudi kulima town.
Halafu akanipa mm jukumu la kufuatilia kesi,siku ya kwanza tu kdg nimzibue vibao nkamchana braza...,hz mambo zipo kifamilia fuatilia mwnyw maana kwangu suspect namba moja hyu hyu shemeji nisije kuharibu mambo bure,for sure mi nltaka akabananishwe na wapelelezi kwanza maana mambo zingine haziingii akilini.
 
Back
Top Bottom