Nahisi nimetapeliwa sijui nifanye nini?

Nahisi nimetapeliwa sijui nifanye nini?

Mi nlipigwa smart tv imewashwa kabisa naiona 42inch. Nafika home nkakuta imekata mistari. Na flash Gb64 kuweka kwa computer haisomi. Jumla nlipigwa 310K.

Nlipowarudishia tulizinguana lkn nkawa nmepigwa.

Nlikuja kumuuzia fundi sh 10000/=[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Umepigwa mzeee

Usipende vitu cheap kabisa[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Duuh nimecheka sana
 
Wanavyodai wanasema. Huwa mara nyingi wanaojua mali zao zina enda Taifishwa basi hufanya mbinu ya kubadilisha bidhaa zao na watu wengine alafu wanachua copy ili walizo nazo wasiinge Hasara kubwa. Hivyo uchukuao kitu kuwa makini kwenye hiyo minada.
 
Habar za humu wanajamvi? Ilikuwa siku ya jumamosi natoka kwenye harakati za vikao na clients wangu basi nikapita pale mwenge mpakani kulikuwa na mnada wavitu wakidai muuza duka alichukua mkopo kashindwa rejesha so vitu vya dukani vikawa vinapigwa mnada.
Basi pale nikaona simu aina ya IPhone 11 Pro max ambayo bei zake huwa ni 1.7m dukani,basi nikaikagua ile simu nikaona kama ipo poa basi nikatamka offer yangu 500,000tsh nikachukua baadae nafika home nakuta sio IPhone kabisa bali wameweka os inayoendana na iPhone isee nilichoka. Sasa je ninaweza kwenda kwenye mamlaka gani inisaidie nipate hela yangu maana hapo nimetapeliwa. Nina risiti ya efd na ya kawaida
Pole sana, chukulia kama funzo kisha songa mbele na maisha.
 
Simu zipo madukani, huko mitaani ulikuwa unatafuta mteremko? Hapo sasa umeupata bara bara! Simu ya bei ghali namba hiyo eti mtu akuuzie kwa laki tano! Lazima liwe kopo! Kwani Dar una muda gani tangu utoke mikoani?
Kaenda mnadani jamanii,mpeni pole lol,.
 
bongo ukisikia kitu bei chee,epuka sana kukisogelea.

maana haya vitu used tu kama ni kizima huwa bei bado imesimamisha mlingoti.

picha linaanza unaambiwa mtu kafilisiwa,kuna pasi za ya umeme,mzani digital,cherehani ya umeme,laptop 6,simu mixer kama 38 hivi,tv 6 zote kampuni tofauti,vyombo vya ndani na printer,saaa swali la kujiuliza huyo mtu alikuwa anafanya bisahara ya aina gani??[emoji23][emoji23]

pole mkuu.
 
Habar za humu wanajamvi? Ilikuwa siku ya jumamosi natoka kwenye harakati za vikao na clients wangu basi nikapita pale mwenge mpakani kulikuwa na mnada wavitu wakidai muuza duka alichukua mkopo kashindwa rejesha so vitu vya dukani vikawa vinapigwa mnada.
Basi pale nikaona simu aina ya IPhone 11 Pro max ambayo bei zake huwa ni 1.7m dukani,basi nikaikagua ile simu nikaona kama ipo poa basi nikatamka offer yangu 500,000tsh nikachukua baadae nafika home nakuta sio IPhone kabisa bali wameweka os inayoendana na iPhone isee nilichoka. Sasa je ninaweza kwenda kwenye mamlaka gani inisaidie nipate hela yangu maana hapo nimetapeliwa. Nina risiti ya efd na ya kawaida


Mnadani mnunuzi anajipangia bei mwenyewe.pia kuna siku utengwa kwa ajili ya wanunuzi kuona vitu vinavyouzwa kabla ya siku yenyewe ya mnada. Mnadani wazoefu hawakurupuki.
 
Jamaa yangu mwaka juzi aliagiza atafutiwe mke kijijini, akatumiwa picha watsapp wakampanga dem mmoja akawa anaongea na jamaa, jamaa akaanza kutuma hadi matumizi watu wanakula, akaambiwa atume mahali jamaa wataifikisha lahaula alikuja kwenda kujionea maajabu mchumba ana mimba ya mshenga
 
Matapeli hawaishi na wajinga pia hawaishi.
Jana wife kapigwa 760,000 kwenye laini za miamala na wale jamaa wanaoipigaga simu.
Yaani licha ya kumpa elimu yote huko nyuma kuwa asije akajaribu kuelekezwa kitu na akafanya kwenye simu za miamala bado alinasa tu.
Hv kalazwa yuko hospitali yaan hasara mara 2.
Damn Dunia ni chungu hii wakat mwingine
 
Back
Top Bottom