NAFUMUA MSHONO: Simu za iPhone ni mdebwedo, wanaozitumia ni watu wa kufuata mkumbo bila reasoning. Simu za Android ndio mpango mzima!

Hiyo ni feature tu ya app logic behind ni kwamba video unaitazama ukitoka kwenye app ya kutazama inajipause mpaka urudi.

Feature ya app gani, youtube ?

Youtube kwenye android inaweza kuwaka wakati unafanya vitu vingine. Kwa hiyo, hiyo ya kufanya jambo moja kwa wakati sio feature ya app, bali ni feature ya Iphone! Feature ya hiyo A15 BIONIC

Processor kali kuliko zote duniani lakini ukiwasha kitu lazima uzime kitu, then what’s the point of being “most powerful”?
 
Feature ya app gani, youtube ?

Youtube kwenye android inaweza kuwaka wakati unafanya vitu vingine. Kwa hiyo, hiyo ya kufanya jambo moja kwa wakati sio feature ya app, bali ni feature ya Iphone! Feature ya hiyo A15 BIONIC

Processor kali kuliko zote duniani lakini ukiwasha kitu lazima uzime kitu, then what’s the point of being “most powerful”?
Ni feature ya Youtube app ya iPhone. Ufanyaji kazi wa app za iPhone na android ni tofauti wana approach tofauti kuanzia graphics mpaka utendaji kazi.
Unatumia iPhone gani wewe maana unalalamika vitu ambavyo havipo. Yes, bionic A15 ni powerful processor imeirithi bionic A14.
Mengine ni implimentation, ndio maana mpaka leo Apple hajawahi ruhusu tablet zipige simu na alipoona watu wanazihack zinapiga simu kwenye tablet zake za zamani, akaacha tumia same chip ambazo zinasupport simu akaanza weka chip ambazo hazisupporr calls.
Video kazi ni kutazama sio kusikiliza ukiondoka kwenye app ya video inabidi ijipause.
 
siongei sana, wacha tunyoke moja kwa moja kwenye hizi points 20+

Android inaweza kufanya mambo mengi kwa mpigo kirahisi (multi tasking)
View attachment 2167558

Kufanya shughuli zaidi ya moja kwa urahisi ni kitu muhimu ambacho kimebanwa sana kwenye iphone, mfano ukitaka kuhamia app nyingine wakati upo kwenye video call basi video call itakata ili uweze kutumia app nyingine, Android unaweza kutumia hata apps hata 10 kwa mpigo na ndio maana kuna kitufe maalum katika vile vitatu ambacho ni maalum kwajili ya multi tasking, kwenye android pia kuna split screen ambayo inafanya screen igawanyike katika vyumba kadhaa kwa shughuli unazotaka kufanya kwa mpigo.

Kwenye iphone hakuna tundu la kuchomeka earphones
View attachment 2166337

Kitu walichofanya iphone ni kulitoa tundu ili kuwakamua pesa watumiaji wao kwa kuwalazimisha wanunue earphone zao zisizo na waya zinazouzwa kuanzia laki 2 na inabidi uzichaji kila siku, wabongo wengi hata iphone wanazonunua ni za mchongo zilizotumika (refurbished) kwasababu za kiuchumi kwahio huwa wananunua earphone wireless za mchina za bei chee, hakika maji hufata mkondo wake. Kwa android uchaguzi ni wako, unaweza uamue kutumia earphone za waya za elf 5 au waweza nunua wireless za laki 4, ni wewe tu. Earphone za waya zina umuhimu wake huwa hazihitaji kuchajiwa kila mara, huwa zinasaidia simu ikianguka isigonge sakafu na pia mtu akitaka kuchomoa simu yako basi unastuka.

Android kuna apps nyingi kuliko Iphone
View attachment 2166329

Sio siri wala kitu cha kubishana kwamba Playstore ya Android kuna apps nyingi kuliko Appstore ya Iphone, Sababu kuu ni kwamba, ili mtengenezaji wa app aiweke app yake kwenye playstore ya android atalipia elf 55 (55,000) mara moja tu lakini kwa upande wa iphone kuweka app kwenye appstore ni lazima ulipie laki 2 na elf 30 (230,000) “kila mwaka”, hapa ndipo watengenezaji wengi wa app wanakimbilia kutengeneza apps za android sababu ni bei rahisi na pia watumiaji wa android ni wengi kuzidi iphone.

Simu ya android yaweza kutumika na mtu zaidi ya moja (multi user)
View attachment 2166326

Hii inaitwa multi user, simu inaweza kutumika na zaidi ya mtu moja bila kuingiliana mambo, mfano unaweza kumtengenezea account mtoto wako awe anachezea game bila yeye kuona message zako, picha / video zako, apps zako, mawasiliano yako, n.k. utampa simu aitumie bila wasi wasi, wewe unakuwa kama admin flani hivi. Ni nzuri pia kwa mtu anapenda kuazima simu yako ila anapenda kupekua pekua visivyomuhusu.

Iphone inanunua vifaa kutoka makampuni ya simu za android
View attachment 2172257

Samsung huwa wanatengeneza simu za android lakini pia wanawauzia iphone vifaa kama vioo, processor, nano flash, n.k. hii ni kutokana na uimara wa vifaa vya samsung ambavyo vilimvutia iphone...

Android utatumia internet bure bila bando
View attachment 2166352

Mtu wa iphone atajibana bana anunue kifurushi cha GB 2 kwa wiki, lakini hayo mambo ya kujibana hayapo android maana kuna apps kama ha tunnel, your freedom, n.k. zinafanikisha utumie internet bure. unaweza kutumia GB 100 kwa wiki na wala isiwe habari, Nikiri kusema kwamba hili si tatizo kwa wale wanaonunuaga iphone za milioni 3 matoleo mapya pale mlimani city, shida inakuja kwa hawa wa kununua iphones za kimchongo zilizotumika (refurbished) tena matoleo yaliyochuja na kila muda simu kaishika mkononi ili watu waione, hawa wengi wao wana changamoto za kiuchumi kwa hio hata mabando ni ya kutumia kwa machale.

Iphone haina memory card
View attachment 2166333

Iphone inaweza kuwa na gb 64 na ikajaa ukasindwa kuongeza nafasi ya ziada maana hakuna tundu la memory card, Lakini pia iphone inaweza kuwa na gb 200 lakini haiondoi umuhimu wa Memory card, simu yako inaweza kudondoka, kuungua, kupata hitilafu, n.k ikashindwa hata kuwaka ila kama ilikuwa na memory card basi utaichomoa kadi yako na ukayakuta mafaili yako yakiwa salama. hata ukiwa katika mazingira ya kuchukuliwa simu yako unaweza kutoa memory kadi yako chap chap ukaiacha simu iende, pia unaweza kuwa na memory card unayohamishia mafaili na kuitunza sehemu salama ili hata simu ukiibiwa isiwe shida.

Bei
View attachment 2172222

Kwenye swala zima la bei Iphone wanatumia mbinu inaitwa “prestige pricing” mfano mwepesi ni kwenda duka la nguo ukakuta mkanda imara wa ngozi unauzwa elf 20 lakini mkanda wa manyoya unauzwa laki, ukiuliza kwanini unaambiwa mkanda wa manyoya una nembo ya Nike, Gucci, n.k. hii prestige pricing inacheza na saikolojia ya mtu ajione yupo juu matawi ya juu endapo akinunua bidhaa hio, Ila sasa ill kuendana na hizi bidhaa huwa inafaa ununue bidhaa dukani na pia toleo liwe jipya, Kwa hapa bongo watu wachache sana wananunua iphones matoleo mapya dukani, wengi huwa wananunua iphones za mchongo zilizotumika (refurbished) na hupendelea kununua matoleo ya nyuma kidogo ili kupunguza makali ya bei (ukilipenda boga kwanini ulichukie ua lake ? ), Kwa upande wa Android huku unaenda kuchukua mzigo wako mpya dukani kulingana na bajeti yako, utaamua wewe ununue daraja la juu “Flagship” mfano Samsung galaxy s22, daraja la kati “Mid range” mfano Motorola g-200, ama daraja la tatu “Budgjet” hapa kibongo bongo kampuni ya Transission holding imelikamata soko kwenye hili kundi kwa kutengeneza simu zote za Tecno, Infinix na Itel.

Notch ya iphone inaziba vitu kwenye screen
View attachment 2172218

.Notch ni kile kisehemu cheusi juu kwenye screen chenye camera na sensor, kwenye iphone huwa ni kipana sana na huwa kinakuziba usione video nzima, pia kuna apps nyingine natumia unakuta zimejaa kwenye screen ila kule kwenye notch unashindwa kuona ama kuminya,

Ni shughuli pevu kuperuzi / kuhamisha mafaili ya iphone
View attachment 2166322

huku android tunatumia file manager tunaona mafaili yote kirahisi lakini system ya iphones kwa kuwa haishirikiani vema kwenye kushare storage na apps huwa inakuwa kazi ngumu kuperuzi mafaili, shughuli inakuwa pevu zaidi unapotaka kuhamisha mafaili kwenye iphone kwa computer / laptop, yani inabidi uwe na program ya itunes kwenye pc ili ufanikishe hili zoezi. unaweza kuwa na pdf file kwenye simu ya android ukifika stationary unachomeka waya wa usb kwenye computer unaprint kazi haraka, kwa upande wa mwenye iphone inabidi ambembeleze mwenye stationary aingize program ya itunes na hapo inabidi anunue bando ili kudownload itunes, yani hadi amalize hii shughuli anakuwa ametumia muda mwingi na kagharamika kununua bando.

Iphone haina radio
View attachment 2166334


Simu za Iphone hazina radio, hapa labda uwe unatumia bando kusikiliza radio za online. ukiwa na android hata kikifika kipindi cha uchaguzi, internet ikikatwa na tcra bado unaweza kuendelea kusikiliza radio.

Mipangilio ya muonekano imebanwa sana iphone
View attachment 2166317

Kwenye iphone kwenye swala la mipangilio ya muonekano (User inteferace customization) wamepigwa kanzu na android kwasababu kwenye android wanaruhusu kubadili launcher, hii launcher itakuruhusu kupangilia muonekano mzima wa simu yako kuanzia muonekano na upangiliaji wa icons, kubadili styles za miandiko, kuficha apps kirahisi kwenye home screen, kuseti mitindo ya app drawer, kuseti gestures, kucheza na swipe actions, scrolling effects, lock screen customization, widgets, n.k. kuna vitu vichache kama widgets za homescreen viliongezewa kwenye iphone mwaka 2020 lakini haya mambo yalikuwepo android toka kitambo.


Iphone haina always on diplay
View attachment 2166345
Kwenye simu za android utaweza kuzima screen ya simu yako ila itaendelea kuonyesha vitu muhimu kama saa, notifications, n.k. Hutakuwa na haja ya kuwasha screen ya simu kila muda ukitaka kuangalia muda. Huna haja ya kuhofia matumizi ya battery kwa sababu hii feature inatumika kwenye vioo vya kisasa vya Amoled ambavyo vinatumia charge kidogo sana, Kuna tetesi matoleo yajayo ya iphones huenda wataweka hii ishu.


Iphone ni lazima utumie bando kuingiza app/game

View attachment 2170901


Kwenye iphone njia pekee ya kuingiza app ni kuzi download kwenye appstore kwa kutumia bando, huku android si lazima kudownload app kwenye playstore, mfano kama unahitaji app flani na huna bando, unaweza kwenda kwa mwenye hio app akakuhamishia file la app kwenye memory card au kwa usb cable, ukipata file unaingiza app bila hata bando. ukitaka ujue thamani ya hii feature chukulia kwamba app kama game ina gb 7 ambazo kifurushi cha data ni shilingi elf 10, kwenye iphone lazima wekundu wa msimbazi ukutoke ili ushushe app ila kwenye android hutalipia hata senti, lakini pia kama sehemu haina network nzuri itabidi usubirie muda mrefu mpaka app imalize kudownload na kama internet imekatwa itabidi utulie tu.

Iphone wanachelewa sana kuweka mahitaji ya wateja
View attachment 2166343

Huwezi amini kwamba iphone ya kwanza kuwa na line 2 ilitoka mwaka 2018 september na hapo bila milioni 2 huipati ila toka kitambo kulikuwa na vitochi vya elf 20 vyenye line mbili, Tukija kwenye widgets za homescreen iphone iliziweka mwaka 2020 wakati android zipo muda mrefu.

Huwezi kuseti ringtone ya muziki kwenye iphone
View attachment 2166320

Ili kuseti ringtone yoyote kwenye android ni kitu ambacho kipo tayari na ni rahisi, kwenye iphone ni mpaka uwe mtundu mtundu ufanye kudownload apps za ziada., hii ndio sababu watumiaji wengi wa Iphones simu zikiita huwa zina mlio kama wa vingoma vya watoto, tulu tutu tu tu tu tu tu, ndi ndi ndi ndi.

Camera
View attachment 2166341

kamera zimeboreshwa sana kwa pande zote, hiki kigezo kwa sasa hakina uzito sana kama zamani picha zilipokuwa na ubora mdogo, Nimetoka kucheki simu zenye kamera kali nimeona inayokimbiza ni android pixel 6 pro, ila nimecheki ubora wa picha za iphone 13 pro max nimeona nayo inatoa picha kali, nadhani hizi ishu za kamera kwa sasa tuzichukulie kawaida, hata simu za laki 2 siku hizi mtu anakutumia picha safi tu ambayo ina ubora standard si haba, kadri miaka inavyoenda tutarajie hata simu za elf 80 zikitoa picha kali mno.

Ulinzi
View attachment 2166338

Hakuna system ambayo haipenyeki, ndio maana hata iphone wanao jibrand kwamba wana simu yenye ulinzi kamili kuna kipindi walikataa kutoa ushirikiano kwenye kuifungue simu ya gaidi ila wataalam wakaichokonoa chapchap ikafunguka bila msaada wa kiwanda cha iphone, hata I-cloud nayo ilidukuliwa zikavuja picha tupu kibao za mastaa, pia iphone hadi leo watu wanai jailbreak, n.k.. kwa iphone naweza kusema ulinzi wake umezidi ulinzi wa android kwa asilimia kadhaa ila sio kwamba ni ulinzi kamilifu. nawakumbusha kwamba sehemu dhaifu kwenye ulinzi wa kifaa huwa ni mtumiaji, iwe ni iphone au android haiwezi kukuzuia kutuma hela kwa namba ile, ukiingia ukurasa feki wa facebook ukaingiza password zako utaibiwa akaunti yako, n.k.

Jail breaking (iphone) v/s Rooting (android)
View attachment 2166335

Jail breaking kwenye iphones itakuruhusu kufanya mambo mengi ambayo tayari yapo kwenye android kwa mfano customization, kwa upande wa rooting inayofanyika android unapata full controll ya kucheza na system kadri unavyotaka.

iphone hazina support nzuri ya Emulators za game

View attachment 2172113

Emulators ni app zinazorugusu kucheza games za playstation, psp, n.k. iphone hazina support nzuri ya Emulators. Kama una simu ya Android ya kisasa kuanzia 2018 kupanda unaweza ukacheza games za Nintendo switch, gamecube, Wii, Playstation 2, psp, Sega dreamcast na console kibao za zamani. Iphone kuna emulators chache sana na hizo zilizopo ni uibie uibie ku install. (point kutoka kwa chief - mkwawa)

………………………………………

Jamanni nawaombeni tu niishie hapa maana nimechoka kuandika, mambo ni mengi ila muda umenibana, yani huwezi amini mpaka leo kuna vitu kama kile kitaa cha rangi cha notification hakipo kwenye iphone, Hivi kweli jamani?.., mdebwedo ni mdebwedo tu hata uuzwe milioni 3😂😂


Tutafute hela tu mjomba..Eti kwamba ubora wa camera ya Iphone 13 Pro ni sawa na simu ya laki 2??
 
Ukiwa na SD Card option huna ulazima wa kwenda Icloud kununua storage wala computer wala itunes wala app yeyote ile.

Kwa nini ulipie ku access data zako kwenye server Marekani wakati naweza kuwa na back up zangu hapa hapa Makete Stendi ???

Keep data local.
Ila kitu kikiwa kwenye icloud sometime hata nikisahau flash nakivuta tu kwenye simu na simu ikiwa imezima nakivuta tena kupitia kwenye PC kwa kuwa ninakuwa doc zangu nimezifanyia arrangement flan hivi

Nimependa "keep data local" ila usiwe local ukapitiliza maana hata mwenye iPhone anaweza akaweka kwenye SD Card kumbuka 5gb free storage ya icloud na nilisema hapo juu kwamba kuna option ya ku-share doc kwa iPhone na PC kwa sekunde chache tu hivyo ukiona hutaki kununua unakuwa unazi-save document zako kwenye PC kwa utaratibu wa kawaida huku kwenye icloud unaacha space ya kutosha kwenye 5GB zako za kitonga.
 
Ukiwa na SD Card option huna ulazima wa kwenda Icloud kununua storage wala computer wala itunes wala app yeyote ile.

Kwa nini ulipie ku access data zako kwenye server Marekani wakati naweza kuwa na back up zangu hapa hapa Makete Stendi ???

Keep data local.
hii ni point kubwa sana, wacha niingize
 
Feature ya app gani, youtube ?

Youtube kwenye android inaweza kuwaka wakati unafanya vitu vingine. Kwa hiyo, hiyo ya kufanya jambo moja kwa wakati sio feature ya app, bali ni feature ya Iphone! Feature ya hiyo A15 BIONIC

Processor kali kuliko zote duniani lakini ukiwasha kitu lazima uzime kitu, then what’s the point of being “most powerful”?
upele umepata mkunaji hapa
 
Maji

Maji ya Kilimanjaro mara nyingi utayakuta bungeni, mahotel makubwa na sehemu zingine za heshima. Maji ya uhai hata muuza ukwaju anayo anapotembeza ukwaju wake. Itoshe kusema Ni sawa uliyoyaongea na watu wanayafahamu ila ukiona kitu kinatumiwa na wachache jua Kuna Cha ziada. Huwezi kuwa Bora duniani Kama ujafanya kitu Cha ziada. Tununue tu simu zetu hizi hizi za Tecno.
maji ya kilimajaro tunayoyapenda ni buku, maji ya dew drop ni buku, maji ya mkwawa ni buku, maji ya dasani ni buku....

-hustuki hapo kwamba kuna ushindani tofauti na iphone asietaka ushindani kwa kuibania os yake?

-nitaftie maji yanayouzwa buku 3 bei juu kama iphone yanayoizidi kilimanjaro tunayolipia thamani yake kama android ?

-cha kukushauri nenda hata kwa mwanafunzi wa form 5 anaesomea hge akufundishe masoko kabla hujakurupuka kuandika usivyovijua.
 
Tutafute hela tu mjomba..Eti kwamba ubora wa camera ya Iphone 13 Pro ni sawa na simu ya laki 2??
Full stop. Nimekuelewa ndugu yangu kitu chochote kizuri au kitamu lazima kiwe na thamani tutafute ela.😂 Ni sawa na kufananisha dagaa mwanza na nyama ya ng'ombe au kuku ziwe bei sawa.
Exactly....hizi nguvu kubwa tunatumia ni umaskini tu.

Naona mmejiunga kumsifia iphone ana kamera nzuri, basi wacha niwakusanye niwape makavu.

Nataka niwajuze tu kwamba hio iphone 13 pro max, kwenye ipande wa camera inakimbizwa na simu nyingi tu za androd, mfano google pixel 6.

Android tunalipia thamani, sio bei ya monopoly anaetengeneza simu kwa laki 8 anaziuza milioni 3 na nusu 🤣
 
Naona mmejiunga kumsifia iphone ana kamera nzuri, basi wacha niwakusanye niwape makavu.

Nataka niwajuze tu kwamba hio iphone 13 pro max, kwenye ipande wa camera inakimbizwa na simu nyingi tu za androd, mfano google pixel 6.

Android tunalipia thamani, sio bei ya monopoly anaetengeneza simu kwa laki 8 anaziuza milioni 3 na nusu
Hivi Pixel 3xl ni nzuri hii...vipi kwenye upande wa chaji mkuuu....nataka ninunue hii
 
Hivi Pixel 3xl ni nzuri hii...vipi kwenye upande wa chaji mkuuu....nataka ninunue hii
Ni simu nzuri sana hizo hasa kwenye kamera wapo vizuri tangu kitambo

naona kuna uzi maalum

 
Ila kitu kikiwa kwenye icloud sometime hata nikisahau flash nakivuta tu kwenye simu na simu ikiwa imezima nakivuta tena kupitia kwenye PC kwa kuwa ninakuwa doc zangu nimezifanyia arrangement flan hivi

Nimependa "keep data local" ila usiwe local ukapitiliza maana hata mwenye iPhone anaweza akaweka kwenye SD Card kumbuka 5gb free storage ya icloud na nilisema hapo juu kwamba kuna option ya ku-share doc kwa iPhone na PC kwa sekunde chache tu hivyo ukiona hutaki kununua unakuwa unazi-save document zako kwenye PC kwa utaratibu wa kawaida huku kwenye icloud unaacha space ya kutosha kwenye 5GB zako za kitonga.
Hatutaki kupitia ICLOUD iliyopo Marekani tunapotaka ku access data zetu na kubadilishana hapa Makete. Tunatumia SD Card na flash zinazouzwa hapa stendi. That is for the vast majority of the minimalist masses of us.

Hatuna bundles za kuchezea, na hatuna minara kila tarafa, na hatuna broadband connectivity kila nyumba. Hatuwezi ku justify, hatuna hoja na haja ya status symbol Apple phones, Apple icloud and Apple stores.

Again, we keep data local, here at Makete Stendi.
 
Naona mmejiunga kumsifia iphone ana kamera nzuri, basi wacha niwakusanye niwape makavu.

Nataka niwajuze tu kwamba hio iphone 13 pro max, kwenye ipande wa camera inakimbizwa na simu nyingi tu za androd, mfano google pixel 6.

Android tunalipia thamani, sio bei ya monopoly anaetengeneza simu kwa laki 8 anaziuza milioni 3 na nusu 🤣


Nakubaliana nawe kuwa kwa benchmarks tofauti tofauti, some android phones zinaishinda Iphone kwenye baadhi ya vigezo vya ubora wa picha.

Ubora wa Iphone 13 Pro Max unapatikana kwenye consistency ya camera yake na zaidi ubora wa video. Jaribu kucheki renowned reviewers kama MKBHD, Lew (Unbox therapy), Dave2D na MrWhoistheBoss.

lastly, simu za android zinazoweza leta upinzani ni flagships only kama Samsung S22 Ultra na mwisho wa siku inategemea zaidi na personal preferences.

Buy flagship kuanzia Sony, Huawei na Samsung na camera zake zitakuwa almost the same na tofauti pekee itakuja kwenye your personal preferences only.
 
Hatutaki kupitia ICLOUD iliyopo Marekani tunapotaka ku access na kubadilishana data zetu hapa Makete. Tunatumia SD Card na flash zinazouzwa hapa stendi. That is for the vast majority of the minimalist masses of us.

Hatuna bundles za kuchezea, na hatuna minara kila tarafa, na hatuna broadband connectivity kila nyumba. Hatuwezi ku justify, hatuna hoja na haja ya status symbol Apple phones, Apple icloud and Apple stores.

Again, we keep data local, here at Makete Stendi.
Nakazia
 
Ubora wa Iphone 13 Pro Max unapatikana kwenye consistency ya camera yake na zaidi ubora wa video. Jaribu kucheki renowned reviewers kama MKBHD, Lew (Unbox therapy), Dave2D na MrWhoistheBoss.
Yote kwa yote ni kwamba Iphone 13 pro max hafui dafu wala hakaribii mbele ya mashine kama pixel 6, anakaa chini vizuri kabisa,

lastly, simu za android zinazoweza leta upinzani ni flagships only kama Samsung S22 Ultra na mwisho wa siku inategemea zaidi na personal preferences.
Post imeshaweka wazi hapo zaidi ya vitu 20 iphone kapigwa kanzu na android, hakuna upinzani hapo bali kuna kuburuzwa,
Buy flagship kuanzia Sony, Huawei na Samsung na camera zake zitakuwa almost the same na tofauti pekee itakuja kwenye your personal preferences only.
Yes, lakini nakukumbusha tu kwamba iphone sio simu yenye kamera bora kama wengi wanavyo danganyika, kuna wababe wa android wanamkalisha
 
Yote kwa yote ni kwamba Iphone 13 pro max hafui dafu wala hakaribii mbele ya mashine kama pixel 6, anakaa chini vizuri kabisa,


Post imeshaweka wazi hapo zaidi ya vitu 20 iphone kapigwa kanzu na android, hakuna upinzani hapo bali kuna kuburuzwa,

Yes, lakini nakukumbusha tu kwamba iphone sio simu yenye kamera bora kama wengi wanavyo danganyika, kuna wababe wa android wanamkalisha


Naomba twende kwa facts mkuu...nakuwekea hapa link ya DXOMark na screenshot yao kuonesha camera scores.

Naomba na wewe uweke yako twende sawa.....https://www.dxomark.com/smartphones/

Screenshot 2022-04-05 120710.png
 
Naomba twende kwa facts mkuu...nakuwekea hapa link ya DXOMark na screenshot yao kuonesha camera scores.

Naomba na wewe uweke yako twende sawa.....https://www.dxomark.com/smartphones/

View attachment 2176718
Kwahio iphone na kelele zote zile ni ya 5 😂😂.

Kwangu binafsi nmewahi cheki review, google pixel 6 ni mashine nyingine,
 
Umekazia, na mimi nakaza.

Nilikuwa kwa kinyozi akapiga miziki mikali nikadhani labda ipo Spotify, au Icloud au Amazon Music, au sijui XM Satellite. Nikamwambia nazipataje hizo ngoma Kiongozi ?

Akasema ziko kwenye flashi hapa hapa saluni. Hakuna mtu analipia ma iCLOUD na ma SPOTIFY viunga hivi. We have higher priorities on spending. Data zetu haziko kwenye servers San Fransisco mjini.

Tunatunza data zetu hapa hapa Makete Stendi.

For the overwhelming majority of us, our phones are powered by Android, the gold-standard of everything open-source.
 
Back
Top Bottom