Nafikiria kuhama Catholic

Hapo juu umeandika vizuri sana but usiupotoshe umma hapo nilipo-bold,Imani Katoliki inamjali yeyote ikiwa tu alijijali yeye mwenyewe alipokuwa hai kwa kufanya yale yanayompasa.

Kuwa muumini hai kwa kuhudhuria jumuiya ndogo ndogo,(hata kama hatoi hata cent moja) na kutoa zaka hata mara moja kwa mwaka,zaka ni msingi wa imani kwa sababu unaonyesha shukrani kwa Mungu unayeamini ndiye amekupa mafanikio so acha kudanganya watu kuna kuwekeza hela Kanisani ili upewe heshima hata uwe nani hutekelezi imani utazikwa kama walevi wengine tu
 
Yeye anataka akitoa sadaka aitwe madhabahuni ili waamini wote wamjue yeye ndiye ametoa nyingi zaidi!

Shida kubwa sana hii Kanisa linaonekana limejaa lakini wengi hatujui tumeenda kusali au kujionyesha uwezo wetu.
Hasomagi biblia huyu, hajui kilichomo kwenye Mathayo 6:3-4!
Asituchoshe
 
Leo ndio unafahamu kuwa Catholic ni na hawapo kiroho hata siki moja

Proud to be Muslim
Funny,very funny!!!

Ndiyo maana kumbe upo bega kwa bega na sa100 japo katuulia ndugu zetu Watanganyika 10K+tena baadhi waliokuwa majumbani mwao wala hujisikii aibu kwa sababu mna-share dini?β€œproud to be” ni kichekesho cha karne,niamini mimi mdau.
 
Mada iliyopo mezani haihusu hayo uliyoandika
 
Utaenda wapi ambako hakuna michango?
 
Mi wanapo nikwaza Wakatoriki ni Ibada ya
Kuisujudia Sanamu ya Kike tu:
Kwakweli wananikwaza sana hata Sina hamu:
Hii na Karne ya Kizazi kipya:
Siwezi kuisujudia Sanamu ya Kike ya SIMENTI kamwe
Mimi mkatoliki lakini sijawahi kuabudu sanamu
 
The right choice , watu tulihama huko miaka Mingi sana. baada ya kulijua hilo .

no spiritual awekening anymore
 
Akitaka sifa aende Jumuiya 🀣
Ila Kanisani Padri akishasema salini ndugu ili sadaka yenu na yangu ikubaliwe na Mungu Baba Mwenyezi imeisha hiyo
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
Au anataka pia akifanya usafi Kanisani atangazwe pale mbele na Padre kwamba Vinci ndiye alipamba Kanisa.

Ila akienda Pentecoste huko
Hasa kwenye huduma changachanga atapata hiki anachokitaka...japo baada ya muda pia atachoka tu maana michango haiishagi.
 
Anataka hadi itajwe kabisa ya kwake specifically πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ’”πŸ™Œ
 
Yeye anataka akitoa sadaka aitwe madhabahuni ili waamini wote wamjue yeye ndiye ametoa nyingi zaidi!

Shida kubwa sana hii Kanisa linaonekana limejaa lakini wengi hatujui tumeenda kusali au kujionyesha uwezo wetu.
Na hiyo siyo Kanuni ya sadaka
Akishajua namna ya utoaji wa sadaka kibiblia, hataangaika na haya mambo ya kutaka kutangazwa na kusifiwa sana.

MUNGU mwenyewe Mbinguni ndiye anayepokea sadaka zetu zote,,zilizoonwa na watu..hata zile zisizoonwa na watu.
 
Hama tu mkuu πŸ˜‚ sema na moyo wako tu , Me nilishaacha hata kusali kitambo tu.

Sema lile chuma limepitia mapito mengi sana mpaka leo wataendelea tu kuwepo walishajiengua watu huko ukiachana na Martin Luther , Henry VII mfalme wa uingereza alijitoa sababu kubwa ikiwa kukataliwa ruhusa ya talaka na Papa, ndo ikaanzishwa Church of England na akawa kiongozi wake mkuu na bado hao Anglican bado sana kuwafikia wakatoliki yaan bado.

Kuna kina Charles Chiniquy jamaa alikosoa sana mamlaka ya papa, Menno Simons huyu alipinga ubatizo wa watoto na Muungano wa kanisa na serikali ,
William Tyndale huyu alitafsiri biblia kwa lugha ya kiingereza bila idhini ya kanisa tena walimchoma moto kabisa πŸ˜‚
Jan Hus huyu nae alichomwa moto tena ni padre kabisa huyu alikosoa ufisadi kanisani tena huyu ni kabla ya Luther.

Wengi wao hawakuanza kwa chuki, bali kwa kukosoa mafundisho, mamlaka ya Papa, au mienendo ya Kanisa.
Wengine walitaka marekebisho ndani ya Kanisa, lakini walikataliwa au kuadhibiwa.

Kwa hiyo mkuu hautakua wa kwanza, Dubwasha litaendelea tu kuwepo mpaka kristo arudi.
 
Ellen G white mwenyewe alishakiri Hilo dude haliwezi kutetereka,miaka ya mbele sabato itasambaratika lakini Hilo dude ni mpaka ukamilifu Wa dahari!
 
Eti Katoliki halimthamini mtu mwenye roho wa Mungu na mwenye Upako ndani πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€ Nenda kwa Mzee wa Upako! Kwani umelazimishwa kusali Katoliki πŸ˜€ Kwamba ukihama kanisa litatetereka? πŸ˜€ Nenda tu kwa Mwamposa, Sisi tupo sana tunasali rozary, na kukamilisha sehemu muhimu ya Liturjia ya misa Takatifu kwa kutoa sadaka na majitoleo! Tunaungama ubatizo mmoja, Maondoleo ya dhambi na Sakramenti muhimu. Tunakutakia kila lenye heri huko uendapo!
 
 

Attachments

  • Screenshot_2026-01-03-11-06-14-77_1c337646f29875672b5a61192b9010f9.jpg
    68.3 KB · Views: 14
Anataka hadi itajwe kabisa ya kwake specifically πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ’”πŸ™Œ
Mwanzo wa mwezi uwa wanataja baada ya sadaka ya kwanza. Muda wa vipaji, mf. Leo jumuiya flani italeta vipaji au familia fulani ina sadaka ya shukrani.. asubiri hizo, mbona zinakuwepo. Ni kwamba hajui au kusudi πŸ₯Ή
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…