1 .Miujiza ya Mungu, hutusogeza katika kumtumikia Yesu Kristo na kushika maagizo yake, na kutufanya kuwa watakatifu kama yeye alivyo mtakatifu. Miujiza yoyote inayoambatana na maagizo yoyote yaliyo kinyume na Neno la Mungu, kama kutumia sanamu za watakatifu, kufukiza uvumba, kutumia rozari au maji ya Baraka, kuzuru makaburi, kuwaomba wafu tuwaombee n.k; haitokani na Mungu (KUMBUKUMBU 13:1-4).Mafundisho ya mtu anayetumiwa kufanya miujiza ya Mungu, hutufundisha kuwa watakatifu, na kuwa mbali na mapenzi ya Mataifa. Wote waliotumiwa sana na Mungu kufanya miujiza kama Paulo, Petro, Yakobo na Yohana, walifundisha hivyo (WARUMI 12:1-2; 1YOHANA 2:15-17; 1 PETRO 1:14-16; 2:12; 4:2-3; YAKOBO 4:4; 1 WAKORINTHO 4:3-4).
2. Miujiza ya Mungu hutolewa bure, hainunuliwi (MATHAYO 10:8; 2 WAFALME 5:14-16; DANIELI 5:16-17; 1 WAFALME 13:6-8; MATENDO 8:18-20). Namna yoyote ya kuomba hela ili kununua muujiza ni kinyume na mpango wa Mungu .Hata kama tutaona wakiuza vitambaa,leso na sabuni zilizoombewa ili zitusaidie, hatuna budi kujua mapanzi ya Mungu kwa watumishi wake ni kutoa huduma ya maombezi bure. Huduma yoyote inayochangisha mchango au kiingilio kwa ajili ya semina ya Neno la Mungu hiyo siyo huduma ya kimungu, ni huduma ya Shetani. Mungu anataka injili iwafikie watu wote.Mfano 1 wa huduma ya shetani ni huduma ya babu wa Loliondo. Bila kutoa sh: 500 usingeweza kupata msaada.Pia miujiza ya Mungu inatokana na Neno la Mungu kama tulivyoona hapo juu. Miujiza ya Mungu inakuwa na lengo la kuwaleta watu kwa Yesu.Watu wanaokuja kutafuta msaada kwa Yesu sharti waongozwe kutubu dhambi zao
kwanza ili kuwapatanisha na Mungu kwa ajili ya kufungua mlangio wa Miujiza yao.
3. Miujiza ya Mungu humtukuza mwana wa , Yesu kristo (YOHANA 11:4), wale wanaotumiwa na Mungu kufanya miujiza ya Mungu hubaki wanadamu na wao kukiri hivyo, na kumpa Mungu utukufu(MATENDO 14:8-18). Tunapomuona mtu akichukua utukufu kana kwa mba yeye ndiye anayetenda miujiza ndipo tunatambua kuwa huyo si mtumishi wa Mungu.
Maisha ya mtu anyetumiwa na Mungu kufanya miujiza yanapaswa kuwa sawasawa na Neno la Mungu. Watu wanaotumiwa na Shetani kufanya miujiza, huambatana na dhambi NNE zinazoonekana upesi-uzinzi au uasherati (1 WAKORINTHO 6:15-17), maneno ya kihuni (YAKOBO 3:10-12), maisha yaliyo sawa na mataifa katika kuvaa na kutenda (WARUMI 12:2; 1 PETRO 2:12; YAKOBO 4:4), maisha yasiyo na uaminifu katika masuala ya fedha na kusema uongo (NEHEMIA 7:2)
HUKUMU YA WATUMISHI WA SHETANI
Watumishi wanaotumiwa kufanya miujiza ya mashetani, mahali pao ni katika ziwa la moto (UFUNUO 19:20; KUMBUKUMBU 13:1-5; MATHAYO 7:22-23. Baada ya kuwa tumefahamu; ni wajibu wetu kujihadhari nao na kuwa mbali na mafundisho yao (MATHAYO 7:15-17; WARUMI 16:17).Mungu akuongoze kufanya maamuzi mazuri katika kuchagua mahali pa kuabudia (dhehebu au kanisa), maana kufanya makosav katika kuchagua mahali pa kulishwa NENO LA MUNGU kunaweza kukugharimu milele. Tafuta mahali ambapo utaelezwa kweli yote bila kufarijiwa kunyume na maandiko.