Mzozo Mkali unaoendelea kati ya Marekani na Venezuela

Mzozo Mkali unaoendelea kati ya Marekani na Venezuela

subiri uone

JF-Expert Member
Joined
Sep 12, 2024
Posts
736
Reaction score
598
Screenshot_20250812-104034.png

Mnamo Agosti 2025 Serikali ya Marekani ilitangaza ongezeko la zawadi hadi dola milioni 50 kwa yeyote atakayetoa taarifa zitakazosaidia kukamatwa kwa Rais wa Venezuela Hatua hiyo ilichukuliwa kutokana na tuhuma kwamba Maduro anaongoza mtandao mkubwa wa usafirishaji wa dawa za kulevya unaojulikana kama "Cartel de los Soles," ambao unadaiwa kushirikiana na makundi ya kihalifu kama FARC na Sinaloa Cartel kuingiza kokaini iliyochanganywa na fentanyl nchini Marekani .

Mwanasheria Mkuu wa Marekani Pam Bondi alieleza kuwa chini ya uongozi wa Rais Trump Maduro hatakwepa mkono wa sheria na atawajibishwa kwa uhalifu wake .
Tangu mwaka 2020 Marekani imekamata zaidi ya tani 30 za kokaini na mali zenye thamani ya zaidi ya dola milioni 700 zinazohusishwa na mtandao wa Maduro ikiwa ni pamoja na ndege binafsi na magari ya kifahari .
Serikali ya Venezuela ilijibu kwa ukali ikikemea hatua hiyo kama ya kusikitisha na ya kipuuzi. Waziri wa Mambo ya Nje Yván Gil alieleza kuwa zawadi hiyo ni jaribio la Marekani kuingilia mambo ya ndani ya Venezuela na kujaribu kugeuza mwelekeo kutoka kwa matatizo ya ndani ya Marekani .
Kwa upande mwingine serikali ya Cuba mshirika wa karibu wa Venezuela ilikosoa vikali hatua hiyo ya Marekani. Rais wa Cuba, Miguel Díaz-Canel alishutumu Marekani kwa kujifanya hakimu wa dunia na kutumia hatua hiyo kama kisingizio cha kuchukua hatua zisizo halali na za upande mmoja dhidi ya Venezuela .

Kwa hatua ya Marekani kuongeza zawadi kwa ajili ya kukamatwa kwa Maduro imezua mvutano mkubwa wa kidiplomasia hasa kati ya Marekani Venezuela na Cuba. Hatua hii inaonyesha kuendelea kwa mvutano wa kisiasa na kiusalama katika eneo la Amerika ya Kusini.

Websites:
AP News: apnews.com/article/0e618369ca68b79b1a2143a95955344a?

New York Post: nypost.com/2025/08/07/us-news/trump-admin-announces-50m-reward-for-capture-of-venezuelas-nicolas-maduro/?

TRT Global: trt.global/world/article/678ae698f1c6?

CubaHeadlines: www.cubaheadlines.com/articles/308620?
 
Cuba ikiwa ni sehem ya mzozo ipo wazi Marekan ita poa na kuogopa!!

na lazima Cuba ijitokeza mapema mwisho wa yote ni yeye Cuba kusambalatishwa.
 
Cuba ikiwa ni sehem ya mzozo ipo wazi Marekan ita poa na kuogopa!!

na lazima Cuba ijitokeza mapema mwisho wa yote ni yeye Cuba kusambalatishwa.
Naona Cuba inafanyiakazi msemo huu "Adui wa adui wako ni Rafiki yako".
 
Cuba ikiwa ni sehem ya mzozo ipo wazi Marekan ita poa na kuogopa!!

na lazima Cuba ijitokeza mapema mwisho wa yote ni yeye Cuba kusambalatishwa.
Inaijua juju Cuba wewe......
 
Zee Trump lina tamaa na rasilimali za Venezuela
 
Cuba ikiwa ni sehem ya mzozo ipo wazi Marekan ita poa na kuogopa!!

na lazima Cuba ijitokeza mapema mwisho wa yote ni yeye Cuba kusambalatishwa.
Kumbuka kuna mkataba uliyo wekwa sahihi baina na Urusi na Merikani, kwamba Merikani haitavamia Cuba au kuifanyia hujuma yoyote, vinginevyo Urusi itaingilia kati ndio maana mpaka sasa Merikani haijawahi kujaribu kuivamia tena Cuba baada ya kushindwa kwenye uvamizi wa Bay of pigs kwenye miaka ya sitini.

Mzozo huu ulitokana na Urusi kuweka Nuclear Missiles nchini Cuba zilizo lenga Merikani, Urusi ilikataa kwamba haiwezi kuondoa nuclear missiles nchini Cuba mpaka hapo Merikani itakapo ondoa missiles zake zinazo lenga Urusi,kutokea Nchni Uturuki na Italy.

Mzozo uliisha baada ya Merikani na Urusi kukubaliana kutekeleza masharti, cha ajabu ukweli huo media za magharibi huwa hawausemi wao utoa taswira kana kwamba Urusi iliogopa Merikani ndio maana iliondoa missiles zake nchini Cuba, hiyo si kweli hata kidogo.Tangu lini Urusi ikatishwa na Taifa kama Merikani??
 
Hawa marekani itafikia hatua nchi zote kuungana kumchapa.
Na atakosa wa kumtetea maana hta ulaya kwenyewe washaanza kumchoka
 
Hapo issue ni mafuta tu wala hakuna kingine,
Kabla ya Maduro alikuwepo Hugo Chavez,nae pia US walikua hawapatani nae.
 
Dikteta Maduro inafaa kabisa akamatwe kwa kufadhili magenge yanayofanya biashara haramu ya mihadarati.
 
Back
Top Bottom