Wanabodi
namshauri kumuandaa mtu wa kumpokea hiyo 2025, na kwa maoni yangu, Dr. Hussein Mwinyi atatufaa sana, hivyo namuomba Rais Samia amuombe Dr. Hussein Mwinyi, kwa uchaguzi wa urais wa 2025 aje kugombea urais wa JMT, kuimalizia awamu ya pili ya Mama Samia
Unaweza kuta aliyepangiwa na YEYE kuwa rais wetu 2025 ni Mama Samia mwenyewe, baada ya kuingia by default kuwa rais wa JMT kwa awamu hii ya kwanza, sasa anajipanga kuendelea awamu ya pili, properly kwa kuchaguliwa na kura za Watanzania, ila kugombea kwake ni kupitia ule mserereko wa CCM , huku Dr. Mwinyi akiji set for his second term in Zanzibar kwa mserereko wa CCM na wala hajui kuwa kuna sauti inamtaka yeye ndiye aje awe rais wa JMT, 2025!, hivyo maono kama haya, yanasaidia sana kuwaandaa watu kisaikolojia!.
Hili la Mwinyi kuja huku, sio la sauti, hili ni langu tuu, maana usikute pia ni mpango ya YEYE, kumfanya huyu jamaa
Dr. Shein Mfute Kazi Haraka, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Kabla Hajamwaga Sumu Hii maana
wakati nikiandika hayo, Dr. Shein alikuwa hajui, hivyo hata saa hizi ninapoandika hapa, usikute huyu jamaa wala hajajijua kuwa yeye ndiye anapaswa aje awe rais ajaye wa Zanzibar!. Hii nibkufuatia dhulma kubwa iliyokuwa ikifanyika Zanzibar kwa miaka na miaka,
Elections 2015 - Imethibitishwa pasi na shaka kuwa ni kweli kabisa, Zanzibar, Maalim Seif na CUF ndio walioshinda lakini sasa kwavile Samia ni mpenda haki, msema haki na mtenda haki, for the first time in Zanzibar tangu baada ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya January 12, 1964, uchaguzi wa 2025 unaweza kuwatendea haki!.
Kuna kitu pia nimeambiwa ni kwa nini Mama amuombe Mwinyi, ila sio lazima kusema kila kitu.
Swali la Morality: Je, ni lazima kuusema kila ukweli unaousikia au tutangulize mbele maslahi ya Taifa? Hivyo mpaka umelisikia hili nimelisema, ujue lina maslahi kwa Taifa.
Paskali
(Mzee wa Sauti, "The Voices From Within)