Tetesi: Mwigulu Nchemba na Januari Makamba wakutana kikao cha dharura baada ya Bunge kutoa mwongozo wa Luhaga Mpina

Stuka

JF-Expert Member
Jul 19, 2022
214
686
KUNA tetesi kuwa baada ya Spika wa Bunge leo 28/6/2023 kumtangaza bungeni Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina kuwa alikuwa sahihi kuhusu kutotekelezwa kwa maagizo ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa. Mawaziri Mwigulu Nchemba na Januari Makamba wamekutana kwa kikao cha dharura kujadili uamuzi huo wa Spika.

Inasemekana kuwa wawili hao kwa muda mrefu walitumia nafasi zao kuzihadaa mamlaka za Chama na Serikali kuwa Mpina amekuwa akisema uongo kwa lengo la kuichafua Serikali ya Rais Samia jambo ambalo Spika wa Bunge Dk. Tulia Ackson amekata mzizi wa fitna kwa kuweka wazi.

Hivyo kwa sasa wanahaha watakwenda kusema nini kuhusu Mpina ilihali walishaziaminisha mamlaka kuwa Mpina ni mpingaji wa Serikali ya Rais Samia.





 
KUNA tetesi kuwa baada ya Spika wa Bunge leo 28/6/2023 kumtangaza bungeni Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina kuwa alikuwa sahihi kuhusu kutotekelezwa kwa maagizo ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa. Mawaziri Mwigulu Nchemba na Januari Makamba wamekutana kwa kikao cha dharura kujadili uamuzi huo wa Spika.

Inasemekana kuwa wawili hao kwa muda mrefu walitumia nafasi zao kuzihadaa mamlaka za Chama na Serikali kuwa Mpina amekuwa akisema uongo kwa lengo la kuichafua Serikali ya Rais Samia jambo ambalo Spika wa Bunge Dk. Tulia Ackson amekata mzizi wa fitna kwa kuweka wazi.

Hivyo kwa sasa wanahaha watakwenda kusema nini kuhusu Mpina ilihali walishaziaminisha mamlaka kuwa Mpina ni mpingaji wa Serikali ya Rais Samia.






Majizi hayo
 
Kuna watu wapumbavu, yaani mtu smart makamba na mwamba jasiri mwigulu wakae kumjadili mpina?!!!!!! Acheni siasa zenu za kijinga hizo......kibongobongo hao wameshatoboa na hamuwafikii hata muwachafue vp
 
Luhaga Mpina alikuwa sahihi ktk suala lipi? Umeandika kana kwamba kila mtu anajua kilichosemwa na Mpina hapo awali.

Mpina kaongea mengi sana pale bungeni. Sasa ni suala lipi lililoombewa ufafanuzi wa spika??
 
Back
Top Bottom