Dkt. Mwigulu asema Nchi haiwezi kupigwa Tsh. 30 Trilioni wakati Bajeti yetu haivuki Tsh. Trilioni 50, Mpina asema Waziri hajui lolote

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
84,010
142,043
Mbunge Mpina asema hii nchi inapigwa kila kona na zaidi ya Tsh. 30 Trilioni zimepigwa na nyingine zimesafirishwa/ kutoroshwa nje ya nchi.

Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba PhD amesema anachosema Mpina hakiwezekani kwa sababu Bajeti ya nchi haizidi tsh 50 trilioni.

Mpina ameomba Waziri Dr Mwigullu PhD na Prof. Mbarawa Wakamatwe na kufungwa kwa Uhujumu Uchumi.

----
Hivi ndivyo ilivyokuwa ndani ya Bunge, leo Novemba 3, 2023 wakati Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina alipokuwa akichangia hoja kisha kujibiwa na Mbunge na Waziri wa Fedha, Mwigulu Lameck Nchemba kuhusu upigaji wa zaidi ya Tsh. Trilioni 30.


 
Mwigulu amekuwa akihenyeshwa na Mpina karibia miezi sita mfululizo, hana hamu kabisa na huyo jamaa.

Huyo Mbarawa ni sawa na mdoli tu wa Samia, hata yeye binafsi naamini anajua kabisa hastahili kuendelea kuwepo kwenye hiyo nafasi, amshukuru dada yake anayemlinda.
 
Mbona wanatuletea mazingaombwe,wizi gani Tena jamani?
 

Attachments

  • 20231102_114349.jpg
    20231102_114349.jpg
    98.3 KB · Views: 5
Mh Mpina asema hii nchi inapigwa kila kona na zaidi ya tsh 30 trillion zimepigwa na nyingine zimesafirishwa/ kutoroshwa nje ya nchi.

Waziri wa Fedha Dr Mwigullu PhD amesema anachosema Mpina hakiwezekani kwa sababu Bajeti ya nchi haizidi tsh 50 trilioni.

Mpina ameomba Waziri Dr Mwigullu PhD na Prof. Mbarawa Wakamatwe na kufungwa kwa Uhujumu Uchumi.

Source: TBC
Mpina ana akili sn, Mwigulu na majangili wenzake lazima walindane bahati mbaya bunge halina hata Spika lina dalali wa Ikulu ana subiri maelekezo pekee
 
Mh Mpina asema hii nchi inapigwa kila kona na zaidi ya tsh 30 trillion zimepigwa na nyingine zimesafirishwa/ kutoroshwa nje ya nchi....
Hakuna jitu jinga kama Mpina, lenyewe ndio halijui kitu. Namfahamu tangia kaiwa Mzumbe huwezi kwa namna yoyte kumlimganisha hata kwa tone na Mwigulu.

Huwa linaongeaga kwa jazba kukosa uwaziri, shida ni kwamba halina impact ktk nchi hii. Amesharudisha yale mashamba alowadhulumu wananchi kule Morogoro?
 
Mwigulu amekuwa akihenyeshwa na Mpina karibia miezi sita mfululizo, hana hamu kabisa na huyo jamaa.

Huyo Mbarawa ni sawa na mdoli tu wa Samia, hata yeye binafsi naamini anajua kabisa hastahili kuendelea kuwepo kwenye hiyo nafasi, amshukuru dada yake anayemlinda.
Mbarawa, Makamba, Mwigulu, Aweso, Nape, Ummy, Bashe, Kijachu, Jafo na Masauni hawafai kuwa kwenye ofisi za umma wanatakiwa magereza haraka sn
 
Mh Mpina asema hii nchi inapigwa kila kona na zaidi ya tsh 30 trillion zimepigwa na nyingine zimesafirishwa/ kutoroshwa nje ya nchi.

Waziri wa Fedha Dr Mwigullu PhD amesema anachosema Mpina hakiwezekani kwa sababu Bajeti ya nchi haizidi tsh 50 trilioni.

Mpina ameomba Waziri Dr Mwigullu PhD na Prof. Mbarawa Wakamatwe na kufungwa kwa Uhujumu Uchumi.

Source: TBC
Mpina anaishi na machungu sana awamu ya sita. Angalau biashara zilizokuwa zinakufa awamu ya tano kwa sasa zinafunguka na mzunguko upo vizuri huku mtaani.
 
Hakuna jitu jinga km Mpina, lenyewe ndio halijui kitu. Namfahamu tangia kaiwa Mzumbe huwezi kwa namna yoyte kumlimganisha hata kwa tone na Mwigulu. Huwa linaongeaga kwa jazba kukosa uwaziri, shida ni kwamba halina impact ktk nchi hii. Amesharudisha yale mashamba alowadhulumu wananchi kule Morogoro?
Hayo Mashamba Komredi Makonda atafuatilia
 
Mh Mpina asema hii nchi inapigwa kila kona na zaidi ya tsh 30 trillion zimepigwa na nyingine zimesafirishwa/ kutoroshwa nje ya nchi.

Waziri wa Fedha Dr Mwigullu PhD amesema anachosema Mpina hakiwezekani kwa sababu Bajeti ya nchi haizidi tsh 50 trilioni.

Mpina ameomba Waziri Dr Mwigullu PhD na Prof. Mbarawa Wakamatwe na kufungwa kwa Uhujumu Uchumi.

Source: TBC
Ok. Tukubaliane na Mwigulu kuwa nchi haiajapigwa trilioni 30, basi Mwigulu aseme, yeye na wenzake wameipiga nchi kwa trilioni ngapi?

Maana hajakanusha kuwa nchi haijapigwa bali anachokataa ni kiasi walichokipiga.
 
Hakuna jitu jinga km Mpina, lenyewe ndio halijui kitu. Namfahamu tangia kaiwa Mzumbe huwezi kwa namna yoyte kumlimganisha hata kwa tone na Mwigulu. Huwa linaongeaga kwa jazba kukosa uwaziri, shida ni kwamba halina impact ktk nchi hii. Amesharudisha yale mashamba alowadhulumu wananchi kule Morogoro?
Nyie ndio madalali, una bifu na Mpina wewe sio bure, hivi kwa uelewa wako Mwigulu ni wa kumlinganisha Mpina!!??
 
Back
Top Bottom