Mwigulu Nchemba: CHADEMA itakufa 2015

Mwigulu Nchemba: CHADEMA itakufa 2015

Mwigamba alitoa akapigwa matofari kwenye kikao,je hiyo ni demokrasia?

hebu elewa bwn simiyu, mwgamba alikili alifanya tukio lile na tena alisema km amekiuka katiba mbele ya media. hasa ulitaka afanye upotoshaji na ukiukwaji wa kanuni halafu chama kikae kimya, je hiyo ndo demokrasia unayotaka wewe simiyu?
 
Ukitaka kujua watu wanapuuza vipi vyama vya kisiasa hapa nchini , angalia ccm maana kina miaka zaidi ya hamsini lakini wanatumia nguvu nyingi kana kwamba chama kipya, na hii ni dalili ya kupuuzwa, Mkuu mara zote chema hakipaswi kutumia nguvu, ukiona hivyo ujue kuna jambo kubwa, kwa viwango vya kisiasa ccm ndiyo inapuuzwa kutokana na ukongwe na bado inafanya vitu kama chama kichanga, angalia hata hiyo mikakati ya kufungua na kufunga mafunzo ya vijana, usanii wa kujifanya wanashiriki katika shughuli za vijijini ni vielelezo wazi, alafu hayo yote ni mambo ambayo si endelevu. Hakika CCM imara imemalizika wakati wa kipindi cha Mzee Mwinyi!

Nashukuru kwa kumpa ukweli wake huy ritz, tena umesahau jambo la uhaba wa maji maeneo mengi ya nchi, hasa km CCM imeshndwa kuwapa wananch huduma ya maji safi na salama n.k, je iendelee kubaki madarakani kufanya nini? bwn ritz ni muda sasa wa kumshauri baba yako kuwa muda umefika afanye ya wananchi na cyo kwa shnikizo la ccm, na akina lukuvi
 
Ndugu zanguni,

Kama mjuavyo ndani ya chadema kuna mgawanyiko wa kutosha na tayari tuna team tatu ambazo zimejigawa kikanda., Hii ni moja ya dalili kuwa Chadema itasambaratika mapema kuliko wengi tulivyofikiri

Sababu kuu ya kusema haya ni hili suala la mahesabu na uchaguzi ndani ya Chadema

Tayari tunajua kuwa Chadema wameingia kambini kuchakachua mahesabu ili wayawakilishe kwenye kamati ya bunge ya mahesabu huku yule aliyewaitisha mahesabu haya akiwa tayari ana data zote za haya mahesabu hivyo hata wakichakachua vipi wataishia kuumbuka tu.

Suala la uchaguzi litaibuka upya soon kwani vijana tayari wameishaanza kuwashitukia viongozi waliopo kuwa ni matapeli.

Nawashauri makamanda wasikubali kufanywa misukule na kudanganywa kitoto bali wasimame na kudai uchaguzi ili wachague viongozi wanaowataka.

TUSUBIRI MHESHIMIWA JEMBE ARUDI KUTOKA SAFARI ......

JITAMBUE

LUKOS, katiba inaeleza wazi, na kwa mujibu wa katiba ibara ya 6.3.2 (a) uongozi bdo muda wake.
 
Ndugu zanguni,

Kama mjuavyo ndani ya chadema kuna mgawanyiko wa kutosha na tayari tuna team tatu ambazo zimejigawa kikanda., Hii ni moja ya dalili kuwa Chadema itasambaratika mapema kuliko wengi tulivyofikiri

Sababu kuu ya kusema haya ni hili suala la mahesabu na uchaguzi ndani ya Chadema

Tayari tunajua kuwa Chadema wameingia kambini kuchakachua mahesabu ili wayawakilishe kwenye kamati ya bunge ya mahesabu huku yule aliyewaitisha mahesabu haya akiwa tayari ana data zote za haya mahesabu hivyo hata wakichakachua vipi wataishia kuumbuka tu.

Suala la uchaguzi litaibuka upya soon kwani vijana tayari wameishaanza kuwashitukia viongozi waliopo kuwa ni matapeli.

Nawashauri makamanda wasikubali kufanywa misukule na kudanganywa kitoto bali wasimame na kudai uchaguzi ili wachague viongozi wanaowataka.

TUSUBIRI MHESHIMIWA JEMBE ARUDI KUTOKA SAFARI ......

JITAMBUE

Mnanjibu huyu muosha vyoo UK ambaye hata kwao akienda anakaa hotelini ? Mnamuona ana la maana la kuongea hapa tofauti na kuwashambulia Slaa , Lema na Mbowe ? Okoeni muda wenu huyu tunamjua huku UK ni mnazi au Mchicha mwiba .
 
kwanza kabisa napenda kutoa rai mimi ni mtanzania ambaye naitaji mabadiliko kwa ajili ya maendeleo ya nchi hii. mabadiliko ambayo ccm imeshindwa kuyafanya hivyo basi niliamini kuwa vyama vya upinzani vitakuwa chachu ya mabadiliko hayo lakini ni tofauti. kwan mwaka 1995 niliamini kuwa Nccr mageuzi chini ya Mhe Mlema nilijua ndio kitaleta mabadiliko lakini hali aikuwa hivyo na hatimae waliingia kwenye malumbana baina ya viongozi wenyewe kati ya Mhe Mlema na Mhe Marandu mwisho wa siku nccr mageuzi imekuwa ni sawa na bustani nzuri iliyopanda mawe badala ya nafaka.

Nikirejea mada yangu kwa mwenendo wa chadema kwa sasa ni sawa na nccr mageuzi kwani ndanj ya chadema awatakiwi watu ambao watahoji mwenendo wa chama pia awatakiwi kusema ukweli wala kukosoa chochote ndani ya chama kwa maslahi ya chama kwani viongozi waliopo wapo kwa maslahi binafsi na sio kwa wananchi wanyonge wa nchi hii. mfano mzuri mwaka 2006 kabla ya kifo cha Marehemu Chcha Wangwe kutokea alikuwa anaonekana msaliti kwa kuwa tu alikuwa anapinga mwenendo mbovu wa chama kwa kuwa wengi wenu humu ni wadau wazuri wa siasa za nchi hii mnajua nn kililmtokea Wangwe sina haja sana ya kuwarudisha huko, huyu ni mfano wa kwanza ila mwaka 2012's tumeshuudia tena vijana makini ndani ya chama wakifukuzwa kwa kuwa tu walisema ukweli wa mambo ndani ya chama na wengi wenu ni mashahidi juu ya hili vijana hao ni Mtela mwampamba na Jiluana Shonza ambao leo hii ni mwiba kwa chama chetu kwani wanatumia muda wao mwingi kutoa maovu ya chama na wana siri nyingi kwa kuwa wamefanya kazi makao makuu kwa muda usiopungua miaka minne ila kinachonishangaza mm kila anaye sema ukweli ndani ya chama anaonekana ni upande wa Zitto, hivi ni kwa nn? au Zitto pekee ndan ya chama ndio msema ukweli?

kwa upeo wangu nikajua ni porojo tu za Mtela na Shonza juu ya ukilitimba uliopo ndani ya chadema ila mwaka huu wiki tatu zilizopita tumeshuhudia Mwigamba akisimamishwa kwa kuwa alisema uhalisia ndani ya chadema ila kwa mhe Lema kumpiga kiongozi wake kwa kuwa ajagusa maslahi ya Katibu na Mwenyekit hakuna hatua ambayo imechukuliwa kwake. kwamba hiyo aitoshi lema amekuwa kuwa hakitoa tuhuma za kejeli zisizokuwa na ushahidi zidi ya Zitto ambaye ni kiongozi wake wa chama kitaifa hakuna chochote anachoongea katibu wala Mwenyekit wa chadema taifa hii ni kwa maana kwamba awajasema ukweli na kwa kuwa Zitto amekuwa akisema ukweli ndani ya chama ni sawa kuchafuriwa. kwa mwenendo huu wa kutotaka viongozi wa juu kuambiwa ukweli na kukoserewa na kila anayesema ukweli anaonekana ni msaliti wa chama huku ni kujichimbia kaburi mwenyewe na mwisho kuja kulia kilio cha samaki.

Taifa kwanza maslahi binafsi baadae.
 
ukiona moshi unafuka ujue kuna moto. Hiki kinachoendelea hivi sasa ndani ya chadema ni ishara kuu kwamba anguko rasmi la chama hiki haliko mbali. juzi arusha viongozi wake wa kitaifa wamepigana mbele za wanachama mbele ya mwenyekiti wa chama hicho taifa. hatujakaa sawa, wabunge wake kule dodoma wanaparuana kuhusu posho za vikao, wanakula matapishi yao, jana mbunge wake ambaye pia ni mjumbe wa vikao vya chadema taifa ametimuliwa kwenye kikao huko kanda ya ziwa, hatujakaa sawa naibu katibu mkuu amejibu kuwa yeye yuko sahihi kwani maamuzi ya kukataa posho ni yake binafsi huku mbunge mwenzake wa chama hicho akikazana kuwa ni usaliti kuchukua baadhi ya posho na kuacha zingine, kwamba bora uchukue zote...
huku haya yakiendelea kutokea, uongozi wa taifa wa chadema upo kimya kama umemwagiwa maji,...hapo ndipo wadadavuzi wa mambo wanaposema kuwa huu ndio mwanzo wa mwisho wa chadema...hapo uchaguzi wenyewe ndani ya chama bado haujafanyika..tutayaona mengi.
.........................
user-offline.png
Godbless J Lema

Yesterday 14:15
#1
icon1.png
Unafiki wa Zitto Kabwe na suala la Posho - Lema


Niliposema Mh Zitto ni mnafiki kuhusu suala hili , nilikuwa na maana ifuatavyo :

Kwamba ,
sio kweli kuwa kukataa posho ni uzalendo na hata ingekuwa ni uzalendo Zitto sio mzalendo katika suala hili la fedha na maisha yake . Aliposema hatachukua posho Wananchi wengi walimuona ni shujaa , ushujaa ambao hana katika jambo hili . Nasema hivi kwa sababu , Wakati Zitto anakataa posho ya kikao ya shilingi sabini elfu ( 70,000 /=) kwa siku ambayo ni sawa na shilingi takribani milioni kumi na mbili kwa vikao vyote vya Bunge kwa Mwaka , Zitto huyo huyo , anapokea posho ya kikao kati ya shilingi laki saba hadi milioni moja kwa kikao kimoja katika vikao vinvyofanywa na mashirika mbali mbali hususani Mashirika ya hifadhi za Jamii . Maana yake ni kwamba kama anapokea laki saba kwa siku na mashirika haya kwa ujumla wake yakafanya vikao ishirini tu kwa mwaka na mara nyingi Zitto kama Mwenyekiti wa PAC huwa anapata mwaliko wa kuhudhuria vikao hivi , basi atakuwa akipata posho ya kikao takribani ya shilingi milioni kumi na nne mpaka milioni ishirini kwa vikao visivyozidi ishirini , wakati kule juu amekataa posho ya shilingi milioni takribani kumi na mbili kwa vikao vya siku takribani mia moja na themanini ambayo ni miezi sita .


Ikiwa vikao hivyo vya mashirika anayohudhuria Zitto kama Mwenyekiti wa PAC ni vya siku mia moja themanini kama ilivyo kwa vikao vya Bunge basi Zitto atakuwa anapokea posho kati ya ya shilingi milioni mia moja na ishirini na sita elfu na laki sita
( 126,600,000) na
milioni mia moja na themanini
( 180,000,000) .
Na hapa naomba kutaja masilahi yangu katika hili kwani Wabunge wa kawaida ikiwa wakialikwa katika vikao hivyo huwa wanalipwa shilingi laki tano kwa kikao kwa siku . Mimi nimewahi kuhudhuria vikao hivyo mara mbili na nikalipwa hivyo pamoja na chai na chakula cha mchana . Tofauti na Mwenyekiti wa Kamati ya PAC yeye pamoja na posho anayochukua ( 700,000 - 1,000,000) hupewa mafuta ya gari au tiketi ya ndege yamkutoa alipo na kumrudisha na kukodiwa Hoteli yenye hadhi ya nyota nne mpaka tano ambayo kwa siku . Hotel hiyo hulipiwa kati ya dola za Marekani mia moja mpaka dola mia sita kwa siku .
...............................


quote_icon.png
By Zitto

Habari/tuhuma hizi sio za kweli. PAC ni marufuku kupokea posho kutoka Taasisi au Mashirika. Ni marufuku kabisa. Namtaka Lema, atoe ushahidi kuwa kamati ya PAC wajumbe wake wanalipwa posho yeyote ile.

Toka nimekuwa mwenyekiti wa POAC sio tu nilipiga marufuku posho bali pia niliwashitaki PCCB wabunge wanaochukua posho kutoka kwa taasisi za Serikali. Wabunge walihojiwa na PCCB kuhusu jambo hili mpaka Sitta alipoingilia kati kuwatetea. Hiyo ilikuwa mwaka 2009 kabla yeye (Lema) hajawa mbunge.-

Wabunge wajumbe wa kamati ya PAC wanalipwa posho za vikao kama wabunge wengine lakini mimi sichukui posho hizo za vikao.

Sio tu PAC hata kwenye Baraza la madiwani na Baraza la Mashauriano la mkoa wa Kigoma na popote kule. Hata NGO zikinialika kwenye vikao vyao sichukui posho za vikao. Nafasi yoyote ninayoalikwa kama mbunge sichukui posho za vikao.-

Yeyote mwenye ushahidi wa mimi kuchukua posho za vikao popote pale auweke hadharani na nitawajibika. Sio kuandika uzushi au maneno ambayo mtu yeyote anaweza kuandika.-

Mimi siwezi kubishana na Lema maana ni kiongozi wake katika chama. Natumaini kadiri anavyokaa kwenye uwanja huu wa siasa atabadilika na kukomaa zaidi.
.....................................


Na hili pia.

icon1.png
Shibuda atimuliwa kikaoni CHADEMA; Apigiwa kura ya kutokuwa na Imani naye!


..............................................



TUESDAY, OCTOBER 29, 2013

SAMSON MWIGAMBA AMWAGA VIELELEZO KUTHIBITISHA MADAI YAKE .... MBOWE, LEMA NA MNYIKA WAMESHIKWA PABAYA ... RIPOTI KAMILI HII HAPA..

hayo ni machache kati ya mengi ndani ya chadema/kadima...yangu macho.














 
CHADEMA ni matapeli wa kisasa.

Nawasifu kwa kutumia matatizo ya wananchi kama mtaji, na wanavuna mihela kweli!


mbona inaonyesha wewe na slaa mlikuwa mabest kinyama? alikutapeli nini mpaka uwaite matapeli? ama ile tender yako nini?
 
MAONI YANGU KWA KILE KINACHOENDELEA KATI YA LEMA NA ZITTO NI DALILI MBAYA KWA CDM KWA SABABU ZIFUATAZO
1. Kama suala la posho wameshindwa kukaa chini na kulimaliza kimya kimya ndani ya chama, je wakipewa nchi si watauana hawa, wataweza kuwa wamoja?? wataweza kutatua matatizo kwa vikao
2. Je hawana viongozi?? DR SLAA YUPO WAPI SASA maana kwenye suala kama hili angewaita mara moja na kuwaonya kama katibu wa chama
3. CCM itazidi kuongoza nchi hii miaka na miaka kwa sababu wapinzani hawana umoja, muda mwingi wanagombana kwa mambo ambayo wangekaa na kuyatatua kama wasomi. Pili hata kama ZITTO anamatatizo kwa nini wasimuite kama chama wakae naye na kuyazungumza matatizo yake yote na mwisho wa siku wawe kitu kimoja
4. Wakosefu wapo kila sehemu hata CCM wapo lakini kama mmekomaa, Ni kufanya kama Nyerere enzi zake ukikosea anakuita ofisini kwake mnazungumza na kukuonya kwa makosa uliyoyafanya kwa misingi ya kutatua matatizo
5. Niliamini CDM wamekomaa, kwa hili ilivyo kati ya ZITTO na LEMA ni mtaji mkubwa kwa CCM
6. Ugomvi wa LEMA na M|kiti wa mkoa wa arusha pia ni dalili mbaya kwa chama. Kwa nini wasingekaa naye kwenye vikao ili kutatua matatizo aliyonayo badala ya kufanya vurugu na timua timua
7. Kama kweli WAPINZANI wanania ya kuongoza nchi hii wajitafakari na kuwa wamoja
8. ZITTO naye kama kiongozi wa PAC badala ya kuita vyombo vya habari angeongea na MKAGUZI MKUU WA SERIKALI na kumuuliza kuhusu hesabu za vyama badala ya kuanza kulipuana. Hapo naye nilimuondolea maksi kwa maana kama kiongozi hutakiwi kukimbilia kwenye vyombo vya habari kwa kila jambo, msingi mkuu ni kutatua tatizo kwa kuzungumza na kupeana hitimisho ili hapo baadae sasa ndo unaweza kutoa kwenye vyombo vya habari yaliyojiri. Maana yangu hapa ni kwamba yeye zitto anatoka chadema na nikiongozi kwenye chama je hakujuwa status ya kukaguliwa?? Pili je akiwa kiongozi wa nchi ataweza kuhilimili mikimiki ya matatizo hapo ndo ninapoona JK anaweza ingawa anaangushwa na watz wenyewe.
 
MAONI YANGU KWA KILE KINACHOENDELEA KATI YA LEMA NA ZITTO NI DALILI MBAYA KWA CDM KWA SABABU ZIFUATAZO
1. Kama suala la posho wameshindwa kukaa chini na kulimaliza kimya kimya ndani ya chama, je wakipewa nchi si watauana hawa, wataweza kuwa wamoja?? wataweza kutatua matatizo kwa vikao
2. Je hawana viongozi?? DR SLAA YUPO WAPI SASA maana kwenye suala kama hili angewaita mara moja na kuwaonya kama katibu wa chama
3. CCM itazidi kuongoza nchi hii miaka na miaka kwa sababu wapinzani hawana umoja, muda mwingi wanagombana kwa mambo ambayo wangekaa na kuyatatua kama wasomi. Pili hata kama ZITTO anamatatizo kwa nini wasimuite kama chama wakae naye na kuyazungumza matatizo yake yote na mwisho wa siku wawe kitu kimoja
4. Wakosefu wapo kila sehemu hata CCM wapo lakini kama mmekomaa, Ni kufanya kama Nyerere enzi zake ukikosea anakuita ofisini kwake mnazungumza na kukuonya kwa makosa uliyoyafanya kwa misingi ya kutatua matatizo
5. Niliamini CDM wamekomaa, kwa hili ilivyo kati ya ZITTO na LEMA ni mtaji mkubwa kwa CCM
6. Ugomvi wa LEMA na M|kiti wa mkoa wa arusha pia ni dalili mbaya kwa chama. Kwa nini wasingekaa naye kwenye vikao ili kutatua matatizo aliyonayo badala ya kufanya vurugu na timua timua
7. Kama kweli WAPINZANI wanania ya kuongoza nchi hii wajitafakari na kuwa wamoja
8. ZITTO naye kama kiongozi wa PAC badala ya kuita vyombo vya habari angeongea na MKAGUZI MKUU WA SERIKALI na kumuuliza kuhusu hesabu za vyama badala ya kuanza kulipuana. Hapo naye nilimuondolea maksi kwa maana kama kiongozi hutakiwi kukimbilia kwenye vyombo vya habari kwa kila jambo, msingi mkuu ni kutatua tatizo kwa kuzungumza na kupeana hitimisho ili hapo baadae sasa ndo unaweza kutoa kwenye vyombo vya habari yaliyojiri. Maana yangu hapa ni kwamba yeye zitto anatoka chadema na nikiongozi kwenye chama je hakujuwa status ya kukaguliwa?? Pili je akiwa kiongozi wa nchi ataweza kuhilimili mikimiki ya matatizo hapo ndo ninapoona JK anaweza ingawa anaangushwa na watz wenyewe.

cc: Dr.W.Slaa
 
Last edited by a moderator:
Watoto wa familia moja wakigombana haina maana undugu utavunjika! Binadamu kwa hulka yake wameumbwa kwa ufahamu wa kujua mema na mabaya! Tangu enzi watu wamekuwa wakigombana na kupatana!

Hivyo kutofautiana kwa Lema na Zitto ni sehemu ya ubinadamu lakini haina maana kudhoofika kwa namna yo yote ile cha CHADEMA!
 
Chadema kushika nchi hii sio leo wala kesho labda mpaka CHAUSTA au SAU vitakaposhika nchi ndipo chadema ifate...
 
CHADEMA ni matapeli wa kisasa.

Nawasifu kwa kutumia matatizo ya wananchi kama mtaji, na wanavuna mihela kweli!

nashukuru kwa kuliona hilo ..... hiyo ni mbinu ya mwanasiasa yyte.
lakini watu wanataka kuamshwa ktk usingizi mzito wa kutojua mambo na haki zao, pia watahitaji watu imara wasio na waoga kudai haki na mali zao za msingi na sio kuburuzwa kama sasa.

chadema sio kama TLP, au NCCR wana wa mageuzi ambao bado ni mamluki hadi leo.
 
Yanayoendelea CHADEMA na CCM ni yale yale , huku Zitto na Lema, kule Kingwangallah na Anna Makinda na Deo Filikunjombe pia inamhusisha Kangi Lugola. Kwa mtu anayeijua siasa vizuri haya mambo ni ya kawaida sana, yanatokea ni kwa sababu ya wakati muafaka kuelekea 2014 na 2015

Sio busara kuhukumu kwa haya yanayotokea bali kwa muelevu ni kukaa na kutulia kufuatilia kwa makini kiongozi sahihi ni yupi kati ya hao watu

Sikubaliani na suala la kuitana na kuyamaliza mambo kisirisiri, ni vyema mambo yakawa wazi kama hivi tunavyo yaona , kutatua mambo kisirisiri huo nao ni unafiki mkubwa
 
Back
Top Bottom