Mwenge-Tegeta Road: Poorly designed, poorly constructed! Nani awajibike?

Mwenge-Tegeta Road: Poorly designed, poorly constructed! Nani awajibike?

Wakuu hii hoja haiwezi kupita bila ya kutendewa haki.

Kabla sijaanza naomba kama Mamlaka husika hasa Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dk.Pombe Magufuli watapitia huku jukwaani tunaomba wafahamu barabara hii ni zaidi ya kero, tunaomba ifumuliwe upya na ijengwe kulingana na misingi ambayo inaeleweka n ahata Waziri wetu huyu anaifahamu.

Ni aibu kwa barabara kubwa kama hiii inayotumika na takribani vigogo wengi wa Nchi hii akiwemo Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ina kasoro ambazo hata mimi ambaye sikusomea uhandisi wa barabara ninaziona wazi:
1. Inatakiwa gari inayopinda kuelekea kulia ama kushoto iwekewe diversion angle ambayo itawezesha gari hilo kupinda kona na kuliruhusu gari la nyuma yake kuendelea na safari kama ilivyo kwa barabara za Nyerere na nyinginezo.

Kama alivyosema mtoa hoja, kwa watu wanaongia barabara za pembezoni tukianzia eneo la Kwakomba, kuna barabara ya Zawadi inayoingia Mbezi juu kwa Mheshimiwa Mbunge Shekifu. Mtu anayetoka Mbezi juu kuelekea Mwenge amenyimwa juction inayomwezesha yeye kukata kulia kwake na kuingia barabara ya kuelekea mwenge mpaka kwanza akate kushoto nakuelekea Tegeta mpaka eneo la Tanki bovu ndipo apinde tena kulia na kurudi tena mpaka KwaKomba ndipo aendelee na safari yake ya Mwenge. Kwanini wasiweke sehemu ya kuingilia hapo hapo Zawadi Road? Kwanini wasifanye kama walivyofanya pale Makonde?

2. Kitu kingine cha hatari ni hizi sehemu za kugeuzia magarikutoka barabara moja kuingia nyingine ni finyu sana kiasi kwamba magari mawili yakikutana pale kuna uwezekano mkubwa wa kugongana hasa kwa kuwa kwanza hakuna ile diversion angle ambayo inamuelekeza mtumiaji kwamba sasa unaingia zone ya kupinda kulia au kushoto. Na ikitokea gari zimepigana pini tayari nyuma inakuwa foleni ndefu tayari imezaliwa.

3. Barabara ni finyu sana bila shaka watakuwa wametumia vipimo vya bajaji maana ukiangalia gari mbili kubwa zinapoeleka sehemu moja utaona uwazi unaoachwa katikati ni mdogo sana.

4. Barabara hata kukamilika haijakamilika tayari kutokea tanki bovu mpaka Tegeta tayari imetengeneza matuta utafikiri mkulima ameandaa shamba kwa ajili ya kupanda viazi.

Barabara hii ni majanga, mheshimiwa Magufuli tunaomba utumie na huku rungu lilelile ulilotumia barabara ya Kilwa kuponda wote waliozembea.

Na kwa kuongezea hapo mtu anayetoka tegeta kwenda interchick inamlazimu aende mpaka makonde then arudi nyuma tena via samaki samaki ndipo afike interchick. hii barabara ni ya ajabu sana
 
Inasikitisha kweli......ndo maana mimi kazini kwangu saa nyingine akija mhandisi au injia naona wajinga tu....ni vitu vidogo sana lakini wanashidwa...hiyo bara bara imejegwa typical kam kilwa road hata hii ya kwenda kwa kasi ni upumbavu mtupu mtaiona...
 
Wakuu hii hoja haiwezi kupita bila ya kutendewa haki.

Kabla sijaanza naomba kama Mamlaka husika hasa Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dk.Pombe Magufuli watapitia huku jukwaani tunaomba wafahamu barabara hii ni zaidi ya kero, tunaomba ifumuliwe upya na ijengwe kulingana na misingi ambayo inaeleweka n ahata Waziri wetu huyu anaifahamu.

Ni aibu kwa barabara kubwa kama hiii inayotumika na takribani vigogo wengi wa Nchi hii akiwemo Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ina kasoro ambazo hata mimi ambaye sikusomea uhandisi wa barabara ninaziona wazi:
1. Inatakiwa gari inayopinda kuelekea kulia ama kushoto iwekewe diversion angle ambayo itawezesha gari hilo kupinda kona na kuliruhusu gari la nyuma yake kuendelea na safari kama ilivyo kwa barabara za Nyerere na nyinginezo.

Kama alivyosema mtoa hoja, kwa watu wanaongia barabara za pembezoni tukianzia eneo la Kwakomba, kuna barabara ya Zawadi inayoingia Mbezi juu kwa Mheshimiwa Mbunge Shekifu. Mtu anayetoka Mbezi juu kuelekea Mwenge amenyimwa juction inayomwezesha yeye kukata kulia kwake na kuingia barabara ya kuelekea mwenge mpaka kwanza akate kushoto nakuelekea Tegeta mpaka eneo la Tanki bovu ndipo apinde tena kulia na kurudi tena mpaka KwaKomba ndipo aendelee na safari yake ya Mwenge. Kwanini wasiweke sehemu ya kuingilia hapo hapo Zawadi Road? Kwanini wasifanye kama walivyofanya pale Makonde?

2. Kitu kingine cha hatari ni hizi sehemu za kugeuzia magarikutoka barabara moja kuingia nyingine ni finyu sana kiasi kwamba magari mawili yakikutana pale kuna uwezekano mkubwa wa kugongana hasa kwa kuwa kwanza hakuna ile diversion angle ambayo inamuelekeza mtumiaji kwamba sasa unaingia zone ya kupinda kulia au kushoto. Na ikitokea gari zimepigana pini tayari nyuma inakuwa foleni ndefu tayari imezaliwa.

3. Barabara ni finyu sana bila shaka watakuwa wametumia vipimo vya bajaji maana ukiangalia gari mbili kubwa zinapoeleka sehemu moja utaona uwazi unaoachwa katikati ni mdogo sana.

4. Barabara hata kukamilika haijakamilika tayari kutokea tanki bovu mpaka Tegeta tayari imetengeneza matuta utafikiri mkulima ameandaa shamba kwa ajili ya kupanda viazi.

Barabara hii ni majanga, mheshimiwa Magufuli tunaomba utumie na huku rungu lilelile ulilotumia barabara ya Kilwa kuponda wote waliozembea.
Kweli mdau umelonga,hii barabara mimi mwenyewe huwa najiuliza hawa wakandarasi wako field kama wanafunzi au ni wakandarasi weledi.Mfano mwingine wa udhaifu wa hii barabara ni kuanzia maeneo ya mbuyuni unapopandisha kwenda stendi tayari lami inatitia,achilia ilo njoo tegeta darajani foleni kubwa ni balaa.Mimi namshauri waziri kituo cha Tegeta kwa ndevu kipanuliwe kwa kuondoa maduka ya upande wa kushoto(walipwe fidia) ili daladala ziweze kuingia ndani ya kituo kama Ubungo tanesco pale,hii itasaidia kupunguza foleni ya Tegeta darajani.Na pia ushauri kwa watu wanaoishi kuanzia maeneo ya basihaya mpaka Bunju,hakuna ulazima wowote wa kupitia tegeta kwa ndevu,wapitie maeneo ya bahari Beach kuelekea ununio mpaka CCM then waunganishe mpaka Bunju kwa kuchepukia Mbuyuni ili kupisha watu wanaoelekea Wazo,Tegeta kibaoni n.k.
 
Kweli mdau umelonga,hii barabara mimi mwenyewe huwa najiuliza hawa wakandarasi wako field kama wanafunzi au ni wakandarasi weledi.Mfano mwingine wa udhaifu wa hii barabara ni kuanzia maeneo ya mbuyuni unapopandisha kwenda stendi tayari lami inatitia,achilia ilo njoo tegeta darajani foleni kubwa ni balaa.Mimi namshauri waziri kituo cha Tegeta kwa ndevu kipanuliwe kwa kuondoa maduka ya upande wa kushoto(walipwe fidia) ili daladala ziweze kuingia ndani ya kituo kama Ubungo tanesco pale,hii itasaidia kupunguza foleni ya Tegeta darajani.Na pia ushauri kwa watu wanaoishi kuanzia maeneo ya basihaya mpaka Bunju,hakuna ulazima wowote wa kupitia tegeta kwa ndevu,wapitie maeneo ya bahari Beach kuelekea ununio mpaka CCM then waunganishe mpaka Bunju kwa kuchepukia Mbuyuni ili kupisha watu wanaoelekea Wazo,Tegeta kibaoni n.k.

Mkuu hapo kwenye rangi nyekundu umenikumbusha jambo muhimu sana ambalo nililisahau, sehemu hiyo inakera mpaka basi. Daladala wakati mwingine zinapakia abiria zikiwa barabarani bila kujali watumiaji wengine kwa kuwa kituo hakitoshi.

Labda wahusika wanasubiri mpaka maafa yatokee waunde tume ndiyo jawabu lipatikane.
 
Na kwa kuongezea hapo mtu anayetoka tegeta kwenda interchick inamlazimu aende mpaka makonde then arudi nyuma tena via samaki samaki ndipo afike interchick. hii barabara ni ya ajabu sana
Dada yangu nashukuru kwa kuliona hilo, ahsante kwa kunikumbusha, hapo napo nikero mpaka wakati mwingine huwa najiuliza hivi hii nchi watu wanaitumia kufanyia majaribio wahandishi wanafunzi wao nini!!!
 
kweli hiyo barabara ina mitihani mingi, ni adhabu ukitaka kuingia kushoto au kulia uingie ndani, eti mpaka ugeuze urudi tena ukaikute njia yako nyuma ulikotoka, entrance hazikutengwa kadri ya mahitaji! sasa sijui ni kumkomoa mwenye gari amalize mafuta akizunguka? na pili ni kweli kama unaindicate kuingia kushoto au kulia ukajisahau au akaindicate lakini wa nyuma yako akaoverlook asipunguze spid anakuvaa, kwa sababu unasubiria kuingia hapohapo hakuna provision yakuingia upande unaoelekea, hasa ukikuta kuna mwenzio kakutangulia na anasubiri magari yanayokuja kutoka upande huo yapite.
kama kuna uwezo wa kurekebisha wafanye hivyo wahusika la sivyo tutakuwa na vilio visivyoisha mbele yetu
 
hamjagusia service road ya hii barabara, yani ni kituko service road hata toroli haliwezi pita, hata watu wawili kupishana kazi!
 
Kwa kweli inasikitisha sana kuhusu mtaalamu aliye chora na kupitisha ramani ya barabara inayoanzia mwenge mpaka Tegeta. Wengi wa watumiaji tunapata taabu sana tunapotaka kuingia barabara za pembezoni.

Mara nyingi tumejikuta tukiwa katika hatari ya kugongwa kwa nyuma ya magari yetu kwa ukosefu wa maeneo ya kuwapisha wenzetu wanaotakiwa kwenda moja kwa moja.

Mfano mzuri ni pale Tangi Bovu kama unatoka mjini na unataka kuingia upande wa kulia yaani Ally Sykes road au anayetoka barabara hiyo na kutaka kuelekea Tegeta wote hao wanakuwa katika hatari ya kupata ajali.

Tunaomba mamlaka husika kabla ya kuipokea barabara hii watoe ushauri na maagizo ya kufanyiwa marekebisho sehemu zote hizo ili ionekane tuna wataalamu wanaojenga barabara za karne hii.

Nakubaliana na wewe mkuu kwa asilimia mia moja.

Usanifu wa barabara hii NI BOMU.
Msanifu ambaye ni mjapani nasikia anaitwa INGEROSEC, ndiye yule yule aliyesikmamia Kilwa Rodi.
TANROADS ndio wa kulaumiwa hapa kwa kukubali kuuziwa mbuzi ndani ya kiroba.siyo siri, usanifu ni bomu, na msanifu hafai.

Katuingiza mjini Kilwa rodi na sasa anatuingiza mjini Bagamoyo rodi.

Usanifu wa barabara ya Bagaomyo kwa kweli uko chini ya viwango kwa sababu zifuatazo
  • Pale eneo la GOIG kuna mto mkubwa tu unaomwaga maji yanayopita juu ya barabara, msanifu hakufanya uchunguzi?
  • Eneo la kuelekea Salasala/Africana vile vile kuna mto mkubwa tu ambao mvua ikizidi mitaro iliyowekwa vile vile ni finyu
  • Pale Interchick tulijionea wenyewe jinsi kale kamto Ndumbwi kanavyoichachafya barabara, hadi mvua za hivi karibuni kukaribia kuibeba barabara
  • Barabara zote kubwa za kitaifa huwa zina kitu inaitwa acceleration & deceleration lane,(Nyerere Rd zipo) kwa ajili ya magari yanayopunguza mwendo na kuingia barabara ndogo za vitongoji, hasa sehemu za Mbezi,Tegeta na hata Jeshini.Hizi lanes hazihjawa provided.
  • Barabara kubwa kama Bagamoyo rd haina service road, barabara za kuunganisha barabara kuu na za vitongoji
  • Kama alivyobainisha mkuu ayoub mkalifya hapo juu, maungio na intersection za barabara yenyewe ni utata mtupu, utafikiri usanifu ulikuwa unafanywa na mtu anayejifunza kazi.
Swali langu ni hili, TANROADS kweli hamuyaoni haya?
Au mnasubiri tu mpaka Magufuli aanze kumwaga razi??
 
Last edited by a moderator:
Hii barabara ni majanga na aibu kubwa hao wahandisi wa TANROADS wamekalia ufisadi tu wanazunguka nchi za wezetu kuna barabara zenye design nzuri ajabu halafu wanakuja kuleta vioja yaani sehemu zote kungia upande wa pili ni majanga kuanzia hapo Tanki bovu, maenea ya karibu na engeni, kungia kunduchi na barabara inayochipukia salasala ni hatari tupu

Vipi kuingia Wazo na kuingi T/Nyuki?
Kulikua na ubaya gani kujenga kiduarisho kama cha mlimani city/kwa Kakobe ambapo watu wa Tegeta Nyuki wange zunga na kuingia service road kisha kupotelea waendako kuliko kiini macho kilichopo hapo sasa hivi.
Hivi hata kifusi ni GHALI sana kiasi barabara mpya ipo chini ya zamani ipo juu, yaani wametengeneza stairs aka vilima visivyo rasmi.
Sehemu zote zilizotajwa na wadau, zina maeneo yaliyobaki wazi kuwezesha kupata viduarisho vya maana kuliko hata vya Mbagala(Kilwa rd). Hii ingesaidia sana kuliko mawazo yao ya kuweka sijui taa au ndo mtajijua wenyewe iliyopo.
Vipinda shoto vya Tangi bovu,Massana, Engen, Afriakana, Mbuyuni(Kunduchi/Sala sala tena hapa ndo balaa,njia ya zamani ipo juu lami mpya ipo bondeniiii!!!!), kona ya Wazo na Tegeta Nyuki.
sasa kile ki Service road cha futi mbili chini ya bara bara sijui cha nini?
Wataalam tusaidieni hapa.
 
Hii barabara ni chinjachinja kabla hata haikaisha. Na magari yanavyokimbizwa uwiii



Sent from my BlackBerry 10 using JamiiForums
 
Na kwa kuongezea hapo mtu anayetoka tegeta kwenda interchick inamlazimu aende mpaka makonde then arudi nyuma tena via samaki samaki ndipo afike interchick. hii barabara ni ya ajabu sana

Sasa hapo makonde jamani tunashuhudia ajali kila wiki ajali mbili hadi tatu....watu wanadai kuna majini....kweli usilolijua ni usiku wa giza.
 
Kwa kweli inasikitisha sana kuhusu mtaalamu aliye chora na kupitisha ramani ya barabara inayoanzia mwenge mpaka Tegeta. Wengi wa watumiaji tunapata taabu sana tunapotaka kuingia barabara za pembezoni.

Mara nyingi tumejikuta tukiwa katika hatari ya kugongwa kwa nyuma ya magari yetu kwa ukosefu wa maeneo ya kuwapisha wenzetu wanaotakiwa kwenda moja kwa moja.

Mfano mzuri ni pale Tangi Bovu kama unatoka mjini na unataka kuingia upande wa kulia yaani Ally Sykes road au anayetoka barabara hiyo na kutaka kuelekea Tegeta wote hao wanakuwa katika hatari ya kupata ajali.

Tunaomba mamlaka husika kabla ya kuipokea barabara hii watoe ushauri na maagizo ya kufanyiwa marekebisho sehemu zote hizo ili ionekane tuna wataalamu wanaojenga barabara za karne hii.
Yaani ni hatari tupu, kama wao hawana ujanja basi si wangedesa hata kwenye bara ya "Sam Nujoma" ! wao ni wakosa kwa upande mmoja lakini hata monitors na mafundi wazalendo nao ni wakosa vile vile! kila anaepewa kazi anawaza "whether it pays or not" hakuna mtendaji anaewaza maslahi ya taifa...
 
Yaani hii mada imenigusa. Waziri hapa yupo kimya kabisa. Yaonekana naye kanogewa na %.
Kituo baada ya Njiapanda ya Kunduchi ukitokea town vipi. Ukitoka kwenye bus watumbikia mtaroni. Yaani wamekula wakasahau kunawa. Waziri mwenye dhamana hili kalifumbia macho. Au naye siku hizi anananii..
 
Du! Haya ni majanga, nami nilipita mitaa ya huko nikabaki nashangaa barabara yote toka mwenge hadi tegeta 'HAINA' vituo vya daladala kabisa.Vilivyopo nadhani ni vituo vya pikipiki,manake ni vidogo.Kwa vituo vilivyopo vya daladala, nadhani zitakua zinapaki ndani ya barabara.vituo ni vidogo mnooo
 
Hii barabara ni majanga ndio maana Mr. J.Pombe haizungumzii kabisa! Nakumbuka nilipita huko wakati ujenzi unaanza, katika mabango ya ujenzi waliandika ujenzi ungekamilika trh 31.8.2013.Mabango hayo kwa sasa yameondolewa! Manake zimebaki siku 23 tu na bado hakisomi! barabara bomu, madaraja Tegeta na eneo la bondeni hayajakamilika na kama vile mkandarasi hayupo site.Kiukwelii mkandarasi ni kama hayupo serious
 
Hii kitu rahisi sana solution yake..... Ila kwa Tanzania, najua itakuwa imesababisha kifo kingine.

4322813.jpg
images
traffic_signal_bird_nest.jpg
 
Pole sana,Nampango wa kutoka lakini ngoja nilale.
 
Back
Top Bottom