Mwenge-Tegeta Road: Poorly designed, poorly constructed! Nani awajibike?

Mwenge-Tegeta Road: Poorly designed, poorly constructed! Nani awajibike?

Morogoro road ndio usiseme. Matuta mataa kila baada ya hatua 10.
Nini faida ya matuta?? Kipindi inajengwa au kwenye mchoro matuta yalkuwepo??

Usjiangalie wewe tu na kigari chako. Tazama maisha ya watu wako
 
U-turn barabara kubwa kama hio sio salama. Inabidi utoke nje ya barabara ndio urudi ulipotoka.
Ni kweli, but kiuhalisia uturn zafanyika as we type na zitaendelea,Je usalama upoje,au nini kifanyike?
Kuna Lane Ile sijui inaitwaje huwa inaongezwa pembeni hivi mtu anaekata kona aingie bila kuathiri wanaondelea mbele..
 
road designer , consultant ndio wenye matatizo, contractor anafanya kama anavyoelekezwa kwenye mchoro.
 
Kama unataka kwenda NBC, unapaswa kuingia njia ya kwenda rainbow, geuza petrol station ya Puma (zamani Bp) alafu rudi tena barabara ya kuelekea mwenge.
Mmekatazwa kupiga u turn sababu barabara ni ndogo sana...gari ikiwa kubwa kidogo inaweza kushindwa ku negotiate ile kona
Ni kweli,ila mind you tunazungumzia sehemu zingine pia,Je ziko convenient kama hapo Petrol station?
Mfano ukitokea mwenge unataka kuingia makonde upande wa mbezi beach unafanyajr kama sio ku uturn? For convenience purposes ipi njia salama
 
Ile barabara ni kaburi la pamoja kama kwenye vita/mauaji ya kimbari
 
Yote yaliyosemwa yana ukweli mtupu. Na wahandisi wetu ndio wa kulaumiwa kwa sababu walikuwa wanahudhuria vikao na waliona udhaifu wa upembuzi yakinifu wa barabara hii. Hasa kutokuwa na njia za kuchepukia pamoja na barabara za pembeni (service road). Vilevile ukisema uweke taa za kuongoza magari itakuwa kichekesho kwani ambao hawachepuki watakaa kwenye foleni muda mrefu. Barabara za pembeni zinatakiwa mwanzo mwisho na sio kisehemu kimoja tu! Upana wa hizo service road uongezwe magari yapishane kwa usalama. Makalavati yapanuliwe sehemu zote maji yanapopita juu ya barabara. Taa za barabarani nazo ni muhimu sio kuweka mabomba ya mabango!
Mkuu umenena.
Waangalizi wa usanifu sijui walikuwa wapi katika kupitia mradi huu.
Sasa ni wazi kuwa kuna watu hasa wahandisi hawafanyi kazi yao.
 
Kuna ile audio clip ya Halima Mdee, Mbunge wa Kawe aliyoitoa majuzi Bungeni wakati akichangia katika bajeti ya wizara ya ujenzi alizungumza mambo ya msingi sana kuhusu ufisafdi na changamoto za hii barabara ya Tegeta - Mwenge- Morocco.
Mwenye nayo msaada aiweke hapa tafadhali.
 
Yaan we shukuru tu imejengwa na haijabanduka bado.., Tabata lami hazichukuagi mwezi, courtesyof Del monte
 
Ni kweli, but kiuhalisia uturn zafanyika as we type na zitaendelea,Je usalama upoje,au nini kifanyike?
Kuna Lane Ile sijui inaitwaje huwa inaongezwa pembeni hivi mtu anaekata kona aingie bila kuathiri wanaondelea mbele..

Inaitwa "Acceleration lane". Kwenye hii barabara ya Mwenge -Tegeta nadhani nimeziona mbili tu, pale junction ya Africana na inapoishia barabara kule Tegeta.
 
We'll said mkuu hii Barabara ina u turn 2 tu, ndo mana mkulu wa wakati ule alisema ukitaka kula lazima uliwe kidogo. Ndo tushaliwa hi yo, tuitumie kwa uangalifu tu
 
Kwa kweli inasikitisha sana kuhusu mtaalamu aliye chora na kupitisha ramani ya barabara inayoanzia mwenge mpaka Tegeta. Wengi wa watumiaji tunapata taabu sana tunapotaka kuingia barabara za pembezoni.

Mara nyingi tumejikuta tukiwa katika hatari ya kugongwa kwa nyuma ya magari yetu kwa ukosefu wa maeneo ya kuwapisha wenzetu wanaotakiwa kwenda moja kwa moja.

Mfano mzuri ni pale Tangi Bovu kama unatoka mjini na unataka kuingia upande wa kulia yaani Ally Sykes road au anayetoka barabara hiyo na kutaka kuelekea Tegeta wote hao wanakuwa katika hatari ya kupata ajali.

Tunaomba mamlaka husika kabla ya kuipokea barabara hii watoe ushauri na maagizo ya kufanyiwa marekebisho sehemu zote hizo ili ionekane tuna wataalamu wanaojenga barabara za karne hii.

Panahitaji taa za kuongoza magari
 
Barabara imekosewa sana na sijui kama tuna hela ya kuongeza barabara za kuchepuka pembeni
 
Wa kulaumiwa ni aliyekuwa waziri wakati huo
 
Ah
Kwa kweli inasikitisha sana kuhusu mtaalamu aliye chora na kupitisha ramani ya barabara inayoanzia mwenge mpaka Tegeta. Wengi wa watumiaji tunapata taabu sana tunapotaka kuingia barabara za pembezoni.

Mara nyingi tumejikuta tukiwa katika hatari ya kugongwa kwa nyuma ya magari yetu kwa ukosefu wa maeneo ya kuwapisha wenzetu wanaotakiwa kwenda moja kwa moja.

Mfano mzuri ni pale Tangi Bovu kama unatoka mjini na unataka kuingia upande wa kulia yaani Ally Sykes road au anayetoka barabara hiyo na kutaka kuelekea Tegeta wote hao wanakuwa katika hatari ya kupata ajali.

Tunaomba mamlaka husika kabla ya kuipokea barabara hii watoe ushauri na maagizo ya kufanyiwa marekebisho sehemu zote hizo ili ionekane tuna wataalamu wanaojenga barabara za karne hii.
Mkalifya umenikumbusha mbali I'd yako imetulia
 
Kupe umesema kweli. Wa TZ wamezoea sana kufanya mambo kiholela. wanataka kila baada ya hatua chache wakatishe barabara. Hata watembea kwa miguu hawatumii zebra crossings wanavuka kila sehemu kiholela. Hata vitu vidogo vya watu binafsi kutimiza wajibu wao wanalalamikia serikali.

Nimekuelewa sana ndugu. Na Sio kilometa 3 tu unaweza kwenda hadi kilometa tano na kwako unapaona pale lakini lazima uzunguke ndio uweze kuingia mtaa wako. Sasa wa tz Kila kona mtu anataka aingie apendavyo yeye. Watu wanashindwa kutofautishga high ways na barabara za mitaani. Serikali itilie mkazo watu wakasome udereva na sheria za barabarani
 
Tatizo si la watalam ni njaa yetu. Tuliomba msaada ya kujengewa barabara kwa Wajapan. Wao wakatoa masharti moja wapo ni kutojenga njia za mikato na taa za barabarani. Tulikubali masharti na ndicho kilichotokea. So issue si wataalam wetu ni njaa yetu
 
Mbona ya kutoka mwenge kuja morocco hamuijadili? Au zile pesa za sherehe ya uhuru ndio hazikutosha? Barabara ile inajaa maji kupita kiasi. Na ina mawimbi kushinda ya baharini. Hata sielewi hawa wajenzi walitumia akili ya wapi kufanya kazi chini ya kiwango vile. Au mnamkomoa aliyeagiza kupanuliwa kwa barabara hiyo? Waziri mhusika zuia malipo ya upanuzi wa barabara hiyo na eafungulie mashtaka wahandisi wanaojenga barabara chini ya viwango mlivyokubaliana. Nawasilisha japo sina gari wala pikipiki!
 
Kila kitu wanafanya JICA kuanzia michoro mpaka kukabidhi barabara na wana wahandisi wao na kila kitu chao.Shida yetu ni umaskini wetu ndo mana tunapokea kazi zenye makosa kama ile ya Kilwa road
 
Inaitwa "Acceleration lane". Kwenye hii barabara ya Mwenge -Tegeta nadhani nimeziona mbili tu, pale junction ya Africana na inapoishia barabara kule Tegeta.
Kama unatoka mjini, ukifika Africana huo mchepuo unaokuwezesha kufanya right turn unaitwa "deceleration lane" sio acc***
 
Back
Top Bottom