Mhaya
JF-Expert Member
- Aug 20, 2023
- 2,563
- 7,321
Katika mkutano wa CAF uliofanyika hivi karibuni, Kuna kipande cha video cha mkutano huo kimeibua maswali mengi hususani kwa watu wa Afrika Mashariki, ikiwemo wakenya ambao kwenye kurusa za mitandao yao ya kijamii video hii imekuwa ikisambaa sana.
Video hii inamhusu muandishi wa habari kutokea Ivory Coast ambaye aliuliza swali ambalo lilionekana kuwakera watu kutokea Afrika Mashariki. Alisikika akisema
View: https://youtu.be/nttda6OWiCg?si=tvkAFrxBTawORycW
Wakenya na watu wengine wa Afrika Mashariki wamekasirishwa na kitendo cha Mwanahabari huyo ambacho limetafsiriwa kama ni kuchongea au kutoa habari ya uongo kuharibu taswira nzima ya Afrika Mashariki. Watu imebidi waende kwenye ukurasa wake wa Instagram na kumzonga kwa maneno mbalimbali. Ukurasa wake ni huu
Video hii inamhusu muandishi wa habari kutokea Ivory Coast ambaye aliuliza swali ambalo lilionekana kuwakera watu kutokea Afrika Mashariki. Alisikika akisema
Sasa lingine linaenda katika nchi tatu za Afrika mashariki ambako tayari nilishafika. Hakuna barabara ndani ya nchi hizo. Baadhi ya wenzangu kutoka Afrika Mashariki waliniambia kutoka nchi moja hadi nyingine itakuchukua siku mbili kuendesha gari. Alafu wasiwasi wangu mkubwa na wasiwasi wa wengi wanahangaika kujua kama hatutashusha kiwango kwa kupeleka mashindano Afrika Mashariki au suluhu ni nini? maana tumeona sasa tuko Morocco, lakini AFCON ilitakiwa iwe Guinea Republic kwa sababu hawakuwa tayari ikahamishiwa Morocco na hii ni AFCON yenye kuhusisha nchi 24. fikiria katika Afrika labda ni nchi nne au tano zenye miundombinu isiyofaa ya kuikaribisha michuano. Je, kuna uwezekano wowote kwamba itaondolewa katika nchi hizo tatu au kuahirishwa tena? Hilo ni swali langu.
View: https://youtu.be/nttda6OWiCg?si=tvkAFrxBTawORycW
Wakenya na watu wengine wa Afrika Mashariki wamekasirishwa na kitendo cha Mwanahabari huyo ambacho limetafsiriwa kama ni kuchongea au kutoa habari ya uongo kuharibu taswira nzima ya Afrika Mashariki. Watu imebidi waende kwenye ukurasa wake wa Instagram na kumzonga kwa maneno mbalimbali. Ukurasa wake ni huu