UFASHE MLIBHONA
Senior Member
- Nov 28, 2012
- 177
- 51
Kwani Jk ni nani? si unajua alivyo dhaifu, hata angeagiza chochote na mtu asitekeleze hawezi kuwawajibisha.
Suala ili usitake kuligeuza kisiasa na kuwa mtaji kwa Chadema hakuna mtu anayeshabikia polisi kuuwa raia... Unataka kutuambia mama Jay na mama Juma pamoja ni wafuasi wa Chadema.
If journalists are Tanzanians, and journalists are not safe, then Tanzanians are not safe!.
Kama jukumu kuu la polisi ni kulinda raia na mali zao, lakini jukumu la polisi wetu badala ya kulinda rais wao ndio wauaji number one, tuki waorganise raia nao walipize kisasi kwa kuwaua polisi wauaji, jee huu utakuwa ni uchochezi?.
Kwani Tahrir squire ilianzaje?, kama ni kweli nguvu ya umma ni nguvu ya Mungu, kama wao waliweza, kwa nini sisi tushindwe?.
Pasco!.
Big No Pasco !!!!unayoyasema naona ni kama naona siamini wewe na kiberiti kwenye kituo cha Petrol station!!nakutambua kama shabiki mkubwa sana wa aina fulani ya kada.Unapochange na kusimama upande mwingine unanitia hofu sana manake asiye amini siku akiamini uwa na IMANI KALI SANA.Ebu tuombe tusifike kwenye stage ya hamasa ya baadhi kuorganize raia walipe kisasi,huko ni kwenda kituo cha mafuta ya Petrol na kiberiti cha gesi.
Nazani kama ili limetokea ni matumaini jukumu la waandishi wa habari nao kujijua wako kwenye hali gani kwa sasa,ni wakati mwafaka wafanye investigative journalism juu ya swala la mwandishi mwenzao huyo,imani yangu ni kuwa sio kila POLISI ni adui wa umma,si vyema kujumuisha.Ebu waandishi wa TANZANIA wafike sehemu nao wabobee!!!ni matumaini yao watakaa kimya na si kupayuka na kisha wataingia mzigoni kupiga kazi nzito ya INVESTIGATIVE JOURNALISM kujua ni nani yuko nyuma ya hili.Kwa umoja wao wataweza wasisimame upande wa kulijaza jesshi hasira na kulifanya nalo lighafilike kujiona liko pekee yake na hakuna anaetambua mchango wao.
KAMA KWELI WANA UJUZI WA KUPATA HABARI NYETI,ZA UFISADI BASI WATUONYESHE KUWA WANAUJUZI WA KUJUA NANI YUKO NYUMA YA ISSUE NZIMA HIYO.Ila wasikurupuke kulitwisha Jeshi lawama za jumla nao ni binadamu tunapowasakama wote hawafai basi wanavunjika moyo na walio wabovu wanapata nafas ya kuongeza makovu ya ufa huo.
Ni kweli sio polisi wote wenye kufanya mabaya ninakubaliana na wewe ila kwa sasa imezidi,imekuwa ni kama kawaida au ndio utaratibu police kutumia risasi za moto ktk miili ya binaadamu hata ktk mazingira yasiofaa.Hivi wangemuua unafikiri wangesema nini?
Ni matukio mengi yameshatokea nchini kwetu ya police kuuwa raia bila sababu au mazingira yanayoruhusiwa kumdhibiti raia.Hivi unafikiri sisi tunapenda kuona ndugu zetu wakiuwawa kinyama na kutuachia majonzi pia tukakaa kimya kama wananchi?Ni bora na sisi tu-dill nao huku mtaani tunapoishi nao ili na wao wauonje walau ule uchungu tunaoupata pale police wanapotushindilia risasi ktl miili yetu.Ktk matukio yooote polisi walioua raia hakuna hatua kali walizochukuliwa sana wanalindwa tu utafikiri wao ndio binaadam sisi ni mafisi
Hatupendi kuyafanya haya lakini vitendo vya kinyama wanavyotufanyia polisi vinatufanya tulazimike kuyafanya haya sababu sisi ni binaadamu,tunao uvumilivu lakini pia tuna kipimo cha uvumilivu.Wajue sisi pia ni binaadam kutuua kwa kutupiga risasi kunaongeza chuki kati yetu na wao.
U cant dragg me out of point Ritz. Pole sana. What is politcs? Kwenye hiyo hoja yangu tena mistari miwili where is CHADEMA. Unashabikia polisi kuua, ndiyo maana unauliza maswali yenye mantiki zilizopinda. I dont care kama ni wafuasi wa chama chochote au hawana chama kabisa, lakini hatuwezi kukubali nchi hii muigeuze police state. Haya ni maisha ya watu, huu ni uhai. Come on. Mambo haya yanafanywa na yataendelea kufanywa kwa sababu polisi wamepewa amri vibarazani kufanya wanayoyafanya. Ndiyo maana wanaua wala hakuna anayewajibika au kuwajibishwa.
Siku hizi kuna amri ya shoot to kill questions later? yaani this is getting out of hand, kama huyu Amiri Jeshi wetu atashindwa kuchukua hatua na kama ana condone such actions things are bound to get even worse kuelekea 2015....................haya ni mambo yasiyokubalika kabisa na wala wasidhani jinsi yanavyotokea kwasababu hawaoni madhara kwao sababu ya ukimya wa wananchi wakatulia na kujiona wako in control, mambo kubadilika ni dakika chache tu hata kwa wale usiowadhania
IGP Mwema na wenzako nadhani muda umewadia kujihudhuru, this is too much