Mwandishi APIGWA risasi na Polisi

Mwandishi APIGWA risasi na Polisi

Police in actions.wamekula milungi na Bangi wanaenda kufanya arrest,upuuzi mwingine huu wa jeshi la polisi!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Nachelea kusema hili tatizo liko CCP, sipati jibu kuwa askari anaamriwa na boss wake kuwa nenda kwa fulani ukikutana naye piga risasi. Mathalani angefungua mlango mtu tofauti bado wangetwanga au wangeingia kupekua?
Pole sana mwandishi!
maagizo yanatoka kwa wakuu wao wa kazi umesahau ya kamanda baro alivyomuambia yule afisa uhamiaji kuwa ana bahati, ukiingia kwenye anga zao wao ni risasi tu hawana Mswalie mtume !
 
DSN,umeeleza vizuri kupoza hasira za Pasco na wengine,Lakini umeharibu kuleta siasa ktk suala la maisha mwanadamu.Unaposema wana ujuzi wa kufanya Investigation za kifisadi"wafanye na Journal Investigation una maana lifanyiwe kazi kisiasa?je mwandishi huyo angekuwa wa gazeti la uhuru ungesema hivyo?!!au kwa sababu ni mwandishi wa Tz daima?!!!.Think Twice"

Mkuu REMSA hoja yangu mi binafsi si muumini wa kisasi [Revenge] na amini kwenye katika TIBa ya kuondoa na kutatua tatizo kama si kulimaluiza kwa ujumla wake kwa njia za mazungumzo na namna ambazo hazi athili wasio husika.Tufike sehemu wanaJF tutambue Nchi yetu nayo inapita katika KIPINDI cha mkanganyiko, kama vile binadamu yoyote anavyopita katika maisha yake.Kuinuka kwa mwanadamu yoyote aliye kwenye CRISiS inategemeana ustahimilivu wake dhdi ya hiyo misukosuko inayomwandama na akishapona kutoka kwenye misukosuko hiyo, binadamu huyo ugeuka kuwa imara na mwenye mafanikio ya aina yake ikiwemo faida kubwa kuwa alishapata kuanguka na atimae alisimama na kufanikiwa.Na hata matajiri wenye mafanikio duniani au hapa nchini ambao hawakupata fedha zao kwa ufisadi ukipewa historia yao walikopita kama unakichwa kidogo utazilai na kuogopa kuwa yeye alifanyaje kupita na kufika hapo.

Tufike sehemu tukubaliane kuwa Taifa nalo liko kwenye migongano mingi yenye interest za magroup ya kijami tofauti tofauti hivyo misuguano hiyo imezaa aina fulani ya tabia na mifumo,mojawapo ikiwa hii ya baadhi ya polisi, ambao ni baadhi na sio wote.Na waandishi ambao kupitia SIRAHA YAO AMBAYO NI karamu na karatasi basi wanaweza kutoa mchango wa mapinduzi ya kifkra tofauti na kada nyingine yoyote.

Vyombo vya habari ambavyo waandishi wa habari wanavitumikia ni muhimili mwingine wa dola usio lasmi [The Fourth Pillar].Hivyo kupitia risasi karamu yenye nguvu ya uchunguzi kwenye taarifa za kina kuhusu nguvu ya nani ilitumika kutenda tukio husika wakiwemo kutambua watendaji wa tukio, hivyo kupatikana kwa taarifa hizo kutaleta mapinduzi ambayo licha ya kuisadia jamii kuvuka katika mtafaruku ho wa kimigongano ya kitabaka na maslahi itaibua ufahamu na werevu mwingine kwenye sekta ya habari.

Mpaka sasa investigation Journalism kwa watanzania tulio wengi ni ndoto,na hatjui ni nini? wakati kwa mataifa ya wenzetu uchunguzi wa aina hiyo ulishasababisha Rais akatolewa madarakani.

Tutafute majibu kwa njia mbali mbali lakin si kwa njia ya jino kwa jino., ama revange!!!
 
This is getting serious guys...!!
JK nchi imemshinda for sure.

.
Nyerere alipokikataa katu katu hiki kichwa kuwa head of state watu hawakumwelewa. Sasa sii kwa hiari tena bali kwa genge hatari la wanamtandao tumelazimishwa kumwelewa Nyerere.
.
 
This is crime...there is no any defense on this, whether they were searching for an armed robber-er or not, it can not justify shooting on an empty hands man. The Culprit should be prosecuted promptly regardless of his/her status.
 
Huwa haya mavituko hayaishi bongo yaani kama muvie hivi
 
kazi kweli kweli Mungu tunusuru najanga hili la polisi maana hata shetani anawashangaa kuona mnavyo ua wenzenu angali ni ndugu zenu
 
Mwandishi wa habari wa gazeti la Tanzania Daima, Shaban Matutu amepigwa risasi na Polisi, ambao wanadaiwa walikuwa wanamtafuta mhalifu na kwenda kugonga chumbani kwa Mwandishi huyo.

Baada ya kufunguliwa wakamfyatulia risasi na kisha wamesema suala hilo ni la bahati mbaya.

Hhivi sasa wamemchukua na wanampeleka hospitali ya Mwananyamala

Mimi bado sijafika popote katika kutafakari hili, najiuliza kwani kama angekuwa muarifu mwenyewe angestahili kupigwa risasi? Isitoshe alikuwa hakimbii ili kutaka kuwatoroka. Kweli hapa lazima pana jambo nyuma ya pazia.

Roho inaniuma lakini nashindwa jinsi ya kuwasaidieni waandishi wa habari wangu.
 
Wanasema kirahisi kuwa walikuwa wanasaka majambazi, walitonywa kuna majambazi wakavamia nyumba ya Mwandishi eti katika kusukumana ndio bastola ikafyatuka risasi ikampata Mwandishi, polisi hawasemi majambazi yapo wapi waliyokuwa wanayasaka, hawakupita kwa mwenyekiti wa mtaa, walivamia nyumbani kwa mwandishi. wanasema Mwandishi alijilinda kwa panga akamjeruhi Askari, hawaonyeshi Askari huyo yuko wapi? amejeruhiwa vipi? Jamani Maswali kibao mimi nimechoshwa na Ujinga wa Polisi na Ujambazi wanaofanya.
 
Yaani hata kuongopa kwa ajili ya kulinda heshima zao wenyewe hawawezi!!! Hopeless imbeciles ndio 'wanaolinda wananchi na mali zetu'!!!!!! hopeless!!!!!

Wakubali tu kuwa wamekosea na wawajibishwe kwa lawsuit kuuuuuuuubwa! wamlipe like 500million hivi ili wapate adabu
 
Ni safari wameanza. Ngoja niwaambie ukweli kidigo kuhusu hawa Polisi, Fuatilia historia zao za maendeleo ya darasani wakiwa shuleni kwa wale waliopata kusoma japo mpaka form four tu. Ni wale ambao walikuwa hawawezi kupata swali kwa mara ya kwanza mpaka masahihisho. Au la, lazima waibie kwa mjuaji mmoja. sasa leo wako wao kwa wao wataibia wapi kama si mwendo wa makosa tu? Ukweli huu haufutiki kirahisi, ni historia imeshaandikwa.
 
[h=3]HIVI NDIVYO MWANDISHI WA HABARI WA GAZETI LA TANZANIA DAIMA ALIVYO AJERUHIWA NA RISASI JANA. [/h]






DSCF3005.JPG

Shabaan Matutu akionesha sehemu ya mkono wake wa kulia ambao ulipata
majeraha wakati polisi walipotumia nguvu kuingia chumbani kwake na
kumtwanga risasi iliyompiga upange wa kushoto wa kifua chake.

DSCF3010.JPG

Mwandishi wa habari wa Kampuni ya Free Media inayochapisha magazeti ya
Tanzania Daima na Sayari, Shaaban Matutu akionesha jeraha lililotokana
na kupigwa risasi na Polisi katika tukio lililotokea usiku wa kuamkia
leo - baada ya polisi kuvamia nyumbani kwake Tegeta jijini Dar es Salaam
kwa madai ya kumtafuta mtuhumiwa waliyekuwa wakimsaka. Matutu kwa sasa
amelazwa Hospitali ya Muhimbili katika Kitengo cha Mifupa (MOI) kwa
ajili ya matibabu zaidi.

DSCF3007.JPG

Shabaan Matutu akionesha sehemu ya mkono wake wa kulia ambao ulipata
majeraha wakati polisi walipotumia nguvu kuingia chumbani kwake na
kumtwanga risasi iliyompiga upange wa kushoto wa kifua chake.

DSCF3012.JPG

Daktari aliyekuwa zamu katika Hospitali ya Mwananyamala akiangali picha
ya X-Ray ya Matutu mara baada ya kufikishwa katika hospitali hiyo na
kufanyiwa kipimo hicho, kabla ya kuhamishiwa katika Hospitali ya Taifa
Muhimbili kwa matibabu zaidi.

DSCF3020.JPG

Wafanyakazi wa Free Media, Khadija Kalili kushoto na Maria Kayala
(kulia) ambao walifika Hospitali ya Mwananyamala baada ya kupata taarifa
za tukio hilo.


Picha Zote na Habari na Dande Francis

 
Wanasema kirahisi kuwa walikuwa wanasaka majambazi, walitonywa kuna majambazi wakavamia nyumba ya Mwandishi eti katika kusukumana ndio bastola ikafyatuka risasi ikampata Mwandishi, polisi hawasemi majambazi yapo wapi waliyokuwa wanayasaka, hawakupita kwa mwenyekiti wa mtaa, walivamia nyumbani kwa mwandishi. wanasema Mwandishi alijilinda kwa panga akamjeruhi Askari, hawaonyeshi Askari huyo yuko wapi? amejeruhiwa vipi? Jamani Maswali kibao mimi nimechoshwa na Ujinga wa Polisi na Ujambazi wanaofanya.

.
Hivi jeshi lote kuanzia mwema kuna aliyewahi kusema ukweli walau mmoja tu toka ajiunge nalo? Kila kukicha bla bla bla tu na ameri wao ni kucheka cheka tu.
Mungu tuepushie mbali hawa mumian.
Utashangaa zaidi ikiwa utasikia kuwa hao waliowajulisha kuwa nyumba hiyo ina majambazi, wamewatoroka.
.
 
Watanzania msilalamike, tulieni. Acheni polisi wafanye kazi yao! Hiyo serikali ya CCM mliiweka wenyewe madarakani. Tulieni mnyooshwe vizuri hadi hapo mtakapoondoa ushabiki wa Yanga na Simba katika siasa!
 

Hivi inaruhusiwa KUSHITAKI UZEMBE wa POLISI as a LAWSUIT na kulipwa $$$ ?
Naona kama kitu kama HICHO KIPO BASI wataacha kuvifyatua fyatua
 
Poleni sana waandishi wa habari nchini Tanzania.

Tatizo ni kwamba mlisema hamuandiki taarifa zozote zinazohusu jeshi la Polisi tokea kipindi kile cha mauaji ya marehemu MWangosi.

Na kwa unafiki mkaendelea kuandika na TV kutangaza mambo ya jeshi la polisi.

Polisi wa Tanzania wana visasi na waandishi wa habari na mkifanya masihala watatumaliza hao.



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Back
Top Bottom