Mwandishi APIGWA risasi na Polisi

Mwandishi APIGWA risasi na Polisi

Nimeuamia sana kuona polisi wanarudia kosa lile lile la kutumia risasi kama fimbo kwa raia wake.Issue hapa siyo kumjeruhi mwandishi bali raia yeyote yule kumpiga risasi eti kwa makosa,kwakweli watanzania inabidi tufikirie tena utendaji kazi wa viongozi wakuu wa polisi.Kuna haja ya baadhi yao kuwajibika.
 
Sioni haja ya kuwa na Police Force Tanzania, Sioni Haja ya kuwa na Chuo cha police Tanzania, nina sababu za kusema hivyo. Si tu kwa matukio kama haya machache tunayoyajua, bali kwa matukio mengi tusiyoyajua wala kuyaona....!!
Nawasilisha!!

 
Ni vijimambo tuu..! Uzuri ni kwamba vina mwisho, tuunganishe nguvu katika kuufikia huo mwisho mapema
 
Umeniambia maneno mabaya sana kama vile mie nafurahia mauaji.

Haya yaishe hayo Ritz, kule SHINYANGA wameua tena, this time wameua mahabusu, nenda jukwaa la habari na hoja mchanganyiko.
 
Last edited by a moderator:
DSN,umeeleza vizuri kupoza hasira za Pasco na wengine,Lakini umeharibu kuleta siasa ktk suala la maisha mwanadamu.Unaposema wana ujuzi wa kufanya Investigation za kifisadi"wafanye na Journal Investigation una maana lifanyiwe kazi kisiasa?je mwandishi huyo angekuwa wa gazeti la uhuru ungesema hivyo?!!au kwa sababu ni mwandishi wa Tz daima?!!!.Think Twice"
 
DSN Nijuavyo mimi amani inapopotea mahali popote duniani jua imesababishwa na fujo(kuvunja/kuvuruga utaratibu),police wetu wa Tanzania hapa wamekuwa mstari wa mbele kufanya fujo/vurugu(kuvunja utaratibu),sidhani kama sheria zinazowaongoza wao ktk utendaji wao wa kazi zinawaruhusu moja kwa moja kuua(kwa namna yeyote ile) sasa inakuwaje mmevamia tu ktk nyumba ya mtu kabla hata hajatoka mmeingia na mlango na kufyatua risasi!!!?

Siungi mkono uvunjaji wa amani ndogo nchini kwetu lakini pia siungi mkono polisi kuua raia kama kuku wanapoteza maana ya ulinzi kwa sisi wananchi wao.Polisi waache kuvuruga utaratibu(fujo)nasi wananchi tutafuata sheria bila tatizo lolote.
 
Last edited by a moderator:
Nimeuamia sana kuona polisi wanarudia kosa lile lile la kutumia risasi kama fimbo kwa raia wake.Issue hapa siyo kumjeruhi mwandishi bali raia yeyote yule kumpiga risasi eti kwa makosa,kwakweli watanzania inabidi tufikirie tena utendaji kazi wa viongozi wakuu wa polisi.Kuna haja ya baadhi yao kuwajibika.

Ni kweli kabisa hivi ni nani wakututetea ??? tunakuwa kama watoto yatima kwa serikali yetu !!!!! inatisha sana
 
Tumaini Makene Kaka Makene waandishi hawako makini tangu tangu serikali ya awamu ya nne mwaka 2005!,kuanzia mwaka huo ndio nimeanza kuona u-seriousness katika ukatili dhidi ya waandishi wa habari,hapa sio kwamba natoa lawama kwa serikali hiyo hapana!,lakini pia sizungumzii kujeruhiwa,ama kuuawa tu kwa wandishi wa habri,lakini nazungumzia hata mazingira y utendaji kzi wao nao sio mzuri,kil mara utasikia mwandishi mahali fulani ametishiwa,mra kauiwa kufanya kazi,na mengine yanayofanana na hayao.

Kwa hiyo naungana na wewe kwamba kwa sasa waandishi wa habari wako katika hali ya htari sana,na ni vyema serikali ikaliona hili na kuchukua hatua za haraka katika kuhakikisha kwamba waandishi wa habari anakuwa ktika hali salama,vinginevyo hali kama hizi zinazoendelea dhidi ya waandishi wa habari zitawafanya waamini kwamba kuna ajenda ya siri nyuma yo!!!
 
Last edited by a moderator:
Kwa kweli watanzania hatuko salama! Pole sana Mwandishi wa habari.
 
Polisi ni kama CCM, ni wezi, majambazi, wauaji, mafisadi, taja ubaya wowote hapa duniani utaukuta CCna jeshi lao la Polisi.
 
Hainiingii akilini hapa!! Kwa kawaida ukimpata mhalifu unatakiwa kumweka chini ya ulinzi na kama anakimbia unapaswa kumpiga risasi ya mguuni ili asife upate kupata unachokitafuta!! Sasa kitendo cha kumlenga mtu kifuani maana yake ni nini? Halafu mtu anajitetea mimi si mama Jay halafu bado unaendelea kumpiga wakati yeye hana hata njiti ya kibiriti ya kujikinga?? Walitaka kumuua huyo mama Jay inaelekea deal zimeumana!!!! Pilissmm mnatesa wazalendo wasio na hatia!! Jamani Rais ajaye wa chama pinzani naomba uanze kwa kulivunja jeshi la polisi na anzisha crush programme CCP. Mbona Nyerere aliweze kulivunja jeshi wakati ule. Ni lazima maamuzi magumu yafanyike ili nchi ipate kurudi katika heshima yake.
 
Polisi wanatekeleza mpango dhalimu wa mtawala,ni vyema wananchi tuikatae ccm ili 2015 tubadilishe mfumo wa jeshi dhalimu la polisi ccm.
 
Tusiwalaumu polisi...nchi hii ina utawala na yanapotokea mambo kama haya na tawala zimenyamaza ina maana kwa namna moja zinafurahishwa na mambo haya,nitashangaa kama kuna mwandishi ambaye hadi sasa atakuwa anaishabikia CCM.

HII SIO BAHATI MBAYA.
 
Huyo kapigwa risasi au mtoa mada unataka kuleta uzushi?

Huyu mwandishi alikuwa akifanya nini mpaka akapigwa risasi.tatizo la waandishi wetu ni limbukeni.panapokuwa na vurugu wao hukaa upande wa wanaofanya vurugu.hivi risasi ikipigwa ataachwa.haya ndio yaliyomkuta yule mwandishi iringa.na wengi wao wanashabikia vurugu.habu kuweni na utaratibu wa kukaa nyuma ya polisi ndipo ufanye coverage yako.ni waandishi wa bongo tuu ndio wanaopigwa risasi na polisi ukiona hivyo ujue tatizo si polisi bali ni waandishi wenyewe.

Kamanda acha uzushi polisi wanafanya kazi yao vizuri ya kulinda huwezi kutegemea kutokuwapo matukio machache kama hayo hawa sio polisi wa Vaitican hapa wanalinda usalama wa raia; matukio ya ujambazi ni mengi na wanapoingia kazini lazima waingie kwa nguvu zote; hivi na wewe kwa akili yako huyo jamaa kapigwa risasi au ndio kama kawaida yenu uzushi @ work

Vijana wanafanya kazi nzuri tu ya kulinda raia na mali zao; you must be very naive to suggest that police have the order to kill; whatever happened is an isolated case you can`t avoid them; our polices work under pressure; and do you believes that dude injury was caused by bullet? That`s a damn cr@p!!!


Sisi tupo yetu MACHO na MASIKO siku yakiwakuta mtakuja tu hapahapa mbiombio, ZOMBA alikuwa mbishi sana, siku yakamkuba BABAMKWE akawekwa ndani na POLICCM, akaja hapa mbiombio .
Na sisi hatuna hiyana tulimsaidia harakati kuanzia kwa waziri hadi kwa IGP na kafanikiwa BABA MKWE akachiwa( na yeye kapata UNYUMBA maan inaonekana mke aligoma mpaka Baba atoke POLCCM" jokin")

Kwahiyo kwanyinyi INSHALAAH MUNGU si KIKWETE tupo hapa siku mtakuja na vilio na tutawasaidia kama kawaida yetu kwani sisi ni WAUNGWANA.
 
Naona walidhamilia kuua, jereha lipo upande wa kushoto (maeneo ya moyo).

Ugua pole mwandishi S. Matutu.
 
Back
Top Bottom