Mwandishi APIGWA risasi na Polisi

Huyu mwandishi alikuwa akifanya nini mpaka akapigwa risasi.tatizo la waandishi wetu ni limbukeni.panapokuwa na vurugu wao hukaa upande wa wanaofanya vurugu.hivi risasi ikipigwa ataachwa.haya ndio yaliyomkuta yule mwandishi iringa.na wengi wao wanashabikia vurugu.habu kuweni na utaratibu wa kukaa nyuma ya polisi ndipo ufanye coverage yako.ni waandishi wa bongo tuu ndio wanaopigwa risasi na polisi ukiona hivyo ujue tatizo si polisi bali ni waandishi wenyewe.

Swahiba huujui uandishi na hata tukio la kuuawa kwa Daudi Mwangosi, ndiyo maana unasema wanakuwa upande wa vurugu kwa kukusaidia tafuta gazeti la Tanzania Daima la septemba 9 utajua namna mwangosi alivyouawa na utajua kama alikuwa katika watu waliokuwa wanashambuliwa na polisi.
kuhusu huyu aliyepigwa risasi na Polisi huko Kunduchi ni kwamba alikuwa Chumbani kwake na mkewe na kwa ufupi ni kwamba askari walielekezwa kwa mtu aliyekuwa akihisiwa kuwauzia madawa ya kulevya vijana, walienda pale kwa lengo la kuchukua fedha na siyo kukamata. mitakupa sababu moja ya msingi kwamba waipewa taarifa mapema juu ya mtu huyo, wakajiandaa kwenda kuonana nae siyo kumkamata kwa kuwa hawakutoa taarifa kituoni kama wataenda kufanya kazi hiyo, na kwa kuwa mlengwa ni mwanamke kama wangetoa taarifa wangepewa askari mwanamke wa kwenda kufanya upekuzi kwa mtuhumiwa ili waweze kumfikisha mahakamani kwa ushahidi watakaoupata, hakuna utetezi hapo taarifa hazikuwa za ghafla juu ya yule wanayemhitaji hawakumshirikisha hata mwenyekiti wa mtaa wajumbe wa mtaa au hata shahidi mwqingine kwa sababu ya kutaka kulinda uhalifu wao usijulikane bahati mbaya kwao wakaingia katika chumba cha mwandishi aliyekuwa amelala na mkewe
 
Ndugu wanaJF naona huko tuendako watz watapoteza imani na police nakuwindana kama nyoka na kisigino cha binadamu, binadamu na kichwa cha nyoka.police ni ndugu zetu tunaomba wabadilke,watende kwa weledi na si hisia au mashinikizo .
 
Ni kama unaendelea kuonyesh ujinga wako kwa jazba na kutokujibu hoja mkuu. Angalia isijekuwa wewe ni mpumbvu

Ni hoja gani aliyoitoa hapo?kwamba yeye ndo alikuwa anafatilia maendeleo ya darasani ya kila mtu aliyeingia au anayetaka kuingia POLISI,ni nani alikwambia kwamba jeshi la POLISI halina wasomi,sio kosa la mtu ukajumlisha na watu wote hata hawa POLISI ni binadamu kama sisi kukosea kupo,anatakiwa aeleze ni nini kifanyike na sio kuleta kashfa za kijinga
UJIPANGE NA WEWE ACHA KUKURUPUKA!
 
Wakati wanawapiga Waislamu mlikuwa mnawasifia Leo mnawachukia kwa sababu ni mwandishi wa gazeti lenu.Mkuki kwa nguruwe tena angekufa ndo uchungu ungekuwa mzuri
polisi ni majambazi wanaotumia kodi zetu kutuua, kutuibia na kutujeruhi. Tatizo ni sisi wenyewe tunawaendekeza
 
Nakubaliana nawe Tumaini Makene ila pengine ni wakati muafaka pia wakuangalia hawa polisi wetu wanapataje ajira zao kwani inaonekana wengi wao ni kama wajinga fulani hivi wanaoamini upolisi ni silaza ya kutishia raia.

Ukisoma magazeti ya leo, unapata picha ya jinsi kamanda wa mkoa anavyohangaika kuwatetea mapolisi wahalifu. Namfahamu Shabani na kama kuna mwandishi mpole, na ambaye unapata shida ya kumfikiria kuwa katika genge la majambazi, basi Shabani ni mmoja wao. Kawaida, ningetegemea polisi wetu wangekuwa wamefikia viwango vya kistaarabu kiasi kwamba wanapogonga ktk mlango wa mtu basi waseme kama wafanyavyo ktk nchi za watu.

Utasikia polisi anapogonga akijitaja kuwa yeye ni polisi na akiingia tu cha kwanza ni kukuonyesha kitambulisha chake cha kazi kama atakuwa amevalia nguo za kiraia. Sisi hapa tunagongewa utadhani kuna ugomvi harafu mtu akiingia tu ananza maneno ya kejeli utadhani asipofanya hivyo hautamjua kuwa yeye ni polisi. Kibaya zaidi, na inauma sana unapoletewa kejeli zakishenzi na mtu ambaye PAYE unayokatwa wewe kwa mwezi mmoja ni sawa na mishahara ya watu kama yeye wanne au watano na dnipo unapojiuliza kuwa hizi kejeli siyo za kawaida. Inawezekana wapo wanaovuta kwanza kabla ya kwenda kumkamata mtuhumiwa.

Ni lazima wabadilike kwani haya ya Shabani yamejulikana kutokana na nafasi yake ktk jamii lakini wapo wengi wanaofanyiwa ushenzi kama huu ila hawana pakusemea na sana sana tunakuja kutangaziwa kuwa polisi walipoingia ndani mtuhumiwa akachukuwa bastola kumbe maskini wa Mungu alishika tu panga akadhani yuko mikononi mwa mwa jamabazi (ni polisi waliovalia kiraia na hawajapenda kujitambulisha).
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: Ame
Wakati wanawapiga Waislamu mlikuwa mnawasifia Leo mnawachukia kwa sababu ni mwandishi wa gazeti lenu.Mkuki kwa nguruwe tena angekufa ndo uchungu ungekuwa mzuri

tena waandishi wa habar hawahawa ndio wanaowasapot askari kuwanyanyasa raia na kudiriki mtu kumwita gaid, lakini mimi naona huyu mwandishi kumbe ndio gaidi mkumbwa na alistahili kufa ila ana bahati sana
 
Mie kwa mtazamo wangu mdogo nafikiri imefikia wakati iwekwe kwenye Katiba kuwa angalau wanaoenda Polisi wawe na div two na three tu kwani jeshi la Polisi sasa hivi wengi ni waliofeli mitihani ya kidato cha nne yaani div four na zero waliofoji vyeti ndio wengi humo hivyo unakuta hawana busara yaani jeshi hilo badala ya kuwa jeshi la kuwasaidia wananchi ndilo linawamaliza ni kama kikundi fulani cha uhalifu na hawakemewi hata wakiua mtu Inajenga picha mbaya kati ya raia na jeshi hilo unajengwa uhasama kati yao kwa sababu wao wanabeba silaha za moto hamna jitihada za kuwazuia wasipoteze maisha ya raia wasio na hatia bila ya sababu za msingi.
Litengenezwe jeshi la polisi zuri lenye malipo mazuri na zana nzuri na lisionee na kuua raia wasio na hatia na jeshi la watu walioelimika tofauti na saa hivi ni kikundi tu cha wahuni fulani waliofeli ndio wanapelekwa kuwa polisi na ndio sababu hawaoni taabu kutumia nguvu kubwa pasipofaa au viongozi wao nao wanamatatizo na iwekwe namna ya kuwajibika kwa kujiuzulu inapotokea mtu wa chini yako kafanya makosa
 
tena waandishi wa habar hawahawa ndio wanaowasapot askari kuwanyanyasa raia na kudiriki mtu kumwita gaid, lakini mimi naona huyu mwandishi kumbe ndio gaidi mkumbwa na alistahili kufa ila ana bahati sana

Indian na Wingu ni lini mtaacha mawazo ya kipumbavu? Linapojadiliwa suala crusial mnaleta mambo ya udini hivi mbona mmetuchosha kusikia mambo ya dini yenu? Ni nani hana dini? Na je wanaokufa kwa kuuwawa na mapolisi ni Waislamu tu? Tumechoka kusikia mambo ya dini yenu kuweni wastaarabu na wenye akili za kujenga hoja na si kuwa na mawazo mgando kila wakati HII NCHI NI YETU WOTE HAKUNA MWENYE HATI MILIKI
 
Last edited by a moderator:
Indian na Wingu ni lini mtaacha mawazo ya kipumbavu? Linapojadiliwa suala crusial mnaleta mambo ya udini hivi mbona mmetuchosha kusikia mambo ya dini yenu? Ni nani hana dini? Na je wanaokufa kwa kuuwawa na mapolisi ni Waislamu tu? Tumechoka kusikia mambo ya dini yenu kuweni wastaarabu na wenye akili za kujenga hoja na si kuwa na mawazo mgando kila wakati HII NCHI NI YETU WOTE HAKUNA MWENYE HATI MILIKI
ni hatar chombo chochote cha habar kumwita mtu gaid hata hao wamarekani hawafanyi hayo nani mkosefu hapa huyu muandishi alitaka znz iweje baada ya kusema hayo. yeye je leo alopigwa risasi unataka tumwite vipi, hapa hakuna udini na kama tumeleta sisi basi hawa waandishi ndio wameuanza, bora angekufa tu
 
Last edited by a moderator:
Baadhi yetu tumefika hospitali. Tulikuwa na mmoja wa wana JF senior. Alinikuta pale. Alikuwepo mwandishi mwenzake na Shaban na mfanyakazi mwenzake mwingine. Kisha akaja mwandishi mwenzake mwingine na pia akafika Absalom Kibanda, Mhariri Mtendaji wa Tanzania Daima na Mwenyekiti wa TEF.

It is just another sad story kwa kweli kama wengine walivyokwisha kusema hapa. Waandishi tumeweza kuzungumza na mke wa Shaban, Mama Jay. Kitu ambacho hakiingii akilini eti polisi wa anti crime hawawezi hata ku spot exactly chumba cha mhalifu wanayemtafuta kwa mabunduki na mabastola, wanaanza kupita wanauliza uliza kwa wapangaji wenzake.

Wanaelekezwa mlango au chumba cha mtuhumiwa wanayemtafuta, Mama Jay. Bado wanakosea mlango, wanaenda kugonga kwa Mama Jay mwingine, bila tahadhari wala kujitambulisha wanaingia ndani wote kishari, kisha wanafyatua risasi kumuelekea Mama Jay (mke wa Shaban), ambaye ananusuriwa na kitendo kile cha wao kuingia kwa kasi kwa kupamia mlango kama wahalifu, anadondoka, risasi zinapigwa zinampata mwandishi wa habari, kama unavyoona kwenye picha, almanusura impate kwenye moyo. Fikiria nini yangekuwa matokeo yake. Risasi kupiga moyoni.

Kisha askari hao ambao tulitarajia wawe weledi hasa linapokuja suala la uhai wa mtu, wanaambiwa hapo si kwa Mama Jay mnayemtafuta, mbona tuliwaelekeza mlango ule pale. Kama hiyo haitoshi, askari mmoja akataka kuitoa ile risasi kwa Shaban kwa mikono. Kufuta ushahidi? Bahati nzuri Shaban aligoma, muda huu wangesharuka. Yangekuwa mambo ya kupigwa na vitu vizito. Imeshindikana.

Nane, maana hatujui filamu hii itageuzwa namna gani baadae hata kufikia tisa na kumi, wakati wanaondoka pale nyumbani kwa Shaban, akipelekwa hospitali, wakapishana na Mama Jay mtuhumiwa aliyekuwa anawindwa na hao anti crime police. Maana inasemekana wakati zogo likiendelea alikimbilia kibanda fulani mtaani hapo hapo. Wameoneshwa Mama Jay mliyekuwa mnamtafuta si huyo hapo, wala...hawakuwa na habari naye tena.

No body is safe. This is not an issue of somebody. Nchi inageuzwa pole pole, police state.

polisi si watu wa kuwa nao karibu kabisa iwe kwa mema ama mabaya ni watu hatari sana na wao hutumia kauri ya kulikuwa na mapambano ama majibishano ya risasi ili kudhihirisha ama kuwaaminisha watu kuwa aliye uwawa ama aliyejeruhiwa ni jambazi,hatuwezi kuwa na jeshi la polisi linalotumika kuuwa watu wasio na makosa yeyote yale.TUMECHOKA tena mtu aliyepewa madaraka makubwa anadanganya umma,na bahati nzuri aliyejeruhiwa hajafa,je angekufa nini kingeongelewa?
nimemsikia mwandishi huyo bwana shaban akiongelea swala hilo ktk radio ebony fm,inasikitisha kwa kweli.
 
Back
Top Bottom