Mwandamanaji mmoja yuko katika hali mbaya baada ya kujichoma moto nje ya ubalozi mdogo wa Israel katika jimbo la Georgia nchini Marekani.Polisi walisema mwandamanaji huyo alitumia petroli, na bendera ya Palestina ilipatikana katika eneo la tukio, nje ya ubalozi mdogo wa Israel mjini Atlanta.
Jinsia na umri wa mtu huyo bado haijawekwa wazi.
Mlinzi aliyejaribu kuingilia kati tukio hilo pia alijeruhiwa.
Kulingana na polisi, mwandamanaji huyo alifika katikaubalozi huo mdogo hicho saa 12:17 kwa saa za ndani (17:17 GMT).
"Tunaamini jengo hili ni salama na hatuoni tishio lolote hapa," Mkuu wa Polisi wa Atlanta Darin Schierbaum alisema. "Tunaamini hiki kilikuwa kitendo cha maandamano ya kisiasa."
Mlinzi huyo aliungua kwenye kifundo cha mkono na mguu, Mkuu wa Zimamoto wa Atlanta Roderick Smith aliwaambia waandishi wa habari.
Mwandamanaji na mlinzi walipelekwa hospitali na wanaendelea na kupata nafuu.
Katika taarifa,Naibu balozi wa Israel kusini-mashariki mwa Marekani, Anat Sultan-Dadon, alisema kuwa ujumbe wa kidiplomasia "unasikitishwa na tukio mtu kujichoma moto kwenye lango la jengo la ofisi".
"Inasikitisha kuona chuki na uchochezi dhidi ya Israeli ukionyeshwa kwa njia ya kutisha," aliongeza kusema.