Dalton elijah
JF-Expert Member
- Jul 19, 2022
- 207
- 453
Askari wa Jeshi la wanahewa la Marekani ambaye alijichoma moto siku ya Jumapili nje ya Ubalozi wa Israeli huko Washington kupinga operesheni ya kijeshi ya serikali ya Kiyahudi huko Gaza amekufa, Pentagon ilisema hapo jana (Jumatatu).
Msemaji wa Jeshi la Wanahewa Rose Riley alisema mtu huyo "alifariki kutokana na majeraha yake na kuaga dunia jana usiku. Tutatoa maelezo zaidi saa 24 baada ya jamaa yake wa karibu kufahamishwa."
Idara ya Huduma ya Moto na Dharura ya D.C. (EMS) ilisema kwenye mtandao wa X kwamba walijibu wito kuhusu mtu aliyekuwa amewaka moto nje ya ubalozi kabla ya saa saba mchana saa za ndani siku ya Jumapili, na kukuta miale ya moto imezimwa na kitengo cha Huduma ya siri.
Mwanahewa huyo, akiwa amevalia sare za kijeshi, alirekodi maandamano hayo mbele ya ubalozi huo akisema "Sitakuwa mshiriki tena katika mauaji ya halaiki," alipiga kelele,, akimaanisha operesheni ya kijeshi ya Israel huko Gaza.
“Free Palestine,” alifoka mfanyakazi wa anga huku akijimwagia petroli na kujiwasha moto, kabla ya kuanguka chini.
Mhudumu huyo ametambuliwa na Idara ya Polisi ya Metropolitan ya D.C. kama Aaron Bushnell mwenye umri wa miaka 25 wa San Antonio, Texas.
Tukio hilo limekuja wakati mzozo kati ya Israel na Hamas unatarajiwa kuingia mwezi wa tano, huku kukiwa na shinikizo linaloongezeka, ikiwa ni pamoja na kutoka Marekani, inayoitaka Israel kutoendesha operesheni ya ardhini kusini mwa Gaza, ambako zaidi ya raia milioni 1 wa Palestina sasa wanaishi.
Chanzo: China News