Nyati
JF-Expert Member
- Mar 6, 2009
- 2,528
- 1,917
Mwanamke mmoja amepigwa risasi ya mkononi kutokana na uzembe wake mwenyewe.
Mwanamke huyo alifika maeneo ya TRA ambako kuna tawi la CRDB - Mapato na kupaki gari eneo lisiloruhusiwa. Askari walimuelekeza eneo hilo haliruhusi kupaki gari lakini alikataa na kuingia ndani ya bank kwa ajili ya shughuli za bank anazozijua yeye.
Askari hao walimfuata tena ndani na kumwambia akatoe gari lakini mwanamke huyo kwa nyodo alimjibu askari huyo aachane nae.
Kuona hivyo askari walikwenda kutoa upepo kwenye matairi ya gari yake ili kama alikuwa na watu wengine wenye nia mbaya wahindwe kutekeleza mpango wao.
Yule mwanamke aliporudi na kukuta gari yake imetokewa upepo alliukiza watu na kuambiwa ni askari waliotoa upepo. Basi alikwenda moja kwa moja kwenye gari na kutoa bastola kisha akaenda kwa askari polisi waliopo huku akiwatisha atawaua. Katika hali ya taharuki yule mwanamke akakoki bunduki kwa lengo la kuitumia na ndipo askari akipomuhai risasi ya mkononi.
Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio mwanamke huyo hajulikani alipata wapi ujasiri wa aliyoyafanya.
Hii nimecopy toka Blog moja: kwani nami yalinikuta Makambako nikiwa safarini ambapo nilenda ATM kukawa hakuna pesa basi nikaingia benki NBC na kupanga foleni iliyokuwa ndefu. Wakati nakaribia akaja mama mmoja mweupe ambaye ali-anti-log (kukaa mbele yangu wakati hakuwepo) kumwuliza akasema eti aongei nami bali meneja
Mama mmoja amepigwa risasi na polisi kujeruhiwa vibaya maeneo ya mapato arusha.chanzo cha tukio hilo kinasema kwamba mama huyo alifika maeneo hayo na kupaki gari yake akitaka kuingia bank lakini akaambiwa eneo hilo halifai kupaki gari,Mama huyo alipaki gari na kuingia bank alipotoka alikuta gari lake limetolewa upepo na ndipo vurugu ilianzaa baina yake yeye na polisi.Vurugu ilipokuwa kubwa mama huyo aliwaambia polisi kwamba wasimtishie bunduki hata yeye anayo na alipotaka kuitoa polisi wakampiga risasi.Mama huyo ni muuzaji maarufu wa madini jijini arusha.Mama huyo amekimbizwa hospitali na yupo chumba cha upasuaji.CHANZO CLOUDS FM