NADHARIA Mwanamke kuwa katika Hedhi inasababisha kunyauka kwa mboga na matunda

Taarifa hii ni nadharia tu, tumeitolea ufafanuzi kwa kadiri ilivyowezekana
Kuna madai mengi mtaani yanayosema kuwa mwanamke akiwa kwenye hedhi husababisha kunyauka kwa mboga na matunda ikitokea amechuma. Mdau mmoja wa JamiiForums amendika pia kuhusu suala hili.

Menstruation.jpg


Baadhi ya tamaduni huwazuia kabisa wanawake wasichume vitu hivyo. Kisayansi, madai haya yana ukweli?
 
Tunachokijua
Hedhi ni tendo la kiasili na kibaiolojia linalotokea kwa mwanamke baada ya kufikia umri wa kuvunja ungo. Tendo hili huwa na umuhimu mkubwa katika kupima uimara wa afya ya uzazi ya mwanamke. Huundwa kwa damu, ute wa mlango wa kizazi, majimaji ya uke, tishu za mji wa uzazi, madini ya chuma, sodium, calcium, phosphate na chloride

Kwa mujibu wa UNICEF, 26% ya wanawake wote duniani wapo kwenye umri unaoruhusu tendo hili litokee maishani mwao.

Tamaduni za nchi nyingi duniani huchukulia hedhi kama jambo lisilofaa kutokana na uwepo wa nadharia nyingi zisizo na uthibitisho wa kisanyansi. Utafiti uliofanywa na UNICEF kwenye nchi za Afghanistan, Bangadesh, Ethiopia, Ghana na Indonesia unathibitisha ukubwa wa tatizo hili. Mfano nchini Afghanistan, wasichana hukatazwa kula nyama, mboga za majani pamoja na kunywa maji ya baridi. Aidha, hukatazwa pia kuosha vyombo na nguo.

Kwa Tanzania, tamaduni za jamii nyingi hukataza wasichana kuchuma mboga wala pilipili, baadhi hukatazwa kubeba mtoto mchanga kwa madai ya kumdhuru au hata kumsababishia homa na maambukizi na wengine huambiwa kukaa mbali na Wanyama kwa kuwa wanaweza kushambuliwa nao. Hii ni mifano michache tu kati ya mingi.

Ukweli wake kisayansi
Kisayansi, tendo la hedhi haliwezi kwa namna yoyote ile kukausha mboga, kupukutisha pilipili, kuchafua maji pamoja na kusababisha maambukizi ya aina yoyote kwa mtoto mchanga. Hizi ni nadharia zisizo na mashiko kisayansi.

UNICEF na WHO wanataja ukosefu wa elimu ya kutosha kwenye jamii zetu kama chanzo namba moja kinachofanya mitazamo na nadharia hizi ziendelee kushika kasi kwenye jamii zetu.

Kisayansi, madai haya sio sahihi. Hedhi ni kitu kinachopaswa kuchukuliwa kama jambo la kawaida kwenye maisha ya binadamu na baadhi ya wanyama kwani ndiyo msingi wa muendelezo wa kuuleta uhai mpya duniani.

Kwa msingi wa hoja hizi umejijenga kiimani, JamiiForums inachukulia suala hili kama nadharia inayopaswa kuchunguzwa zaidi ili kupata uthibitisho unaoweza kupimwa kwa njia zilizo wazi.
Hedhi ni tendo la kiasili na kibaiolojia linalotokea kwa mwanamke baada ya kufikia umri wa kuvunja ungo. Tendo hili huwa na umuhimu mkubwa katika kupima uimara wa afya ya uzazi ya mwanamke.

Kwa mujibu wa UNICEF, asilimia 26 ya wanawake wote duniani wapo kwenye umri unaoruhusu tendo hili litokee maishani mwao.

Tamaduni za nchi nyingi duniani huchukulia hedhi kama jambo lisilofaa kutokana na uwepo wa nadharia nyingi zisizo na uthibitisho wa kisanyansi. Utafiti uliofanywa na UNICEF kwenye nchi za Afghanistan, Bangadesh, Ethiopia, Ghana na Indonesia unathibitisha ukubwa wa tatizo hili.Mfano nchini Afghanistani, wasichana hukatazwa kula nyama, mboga za majani pamoja na kunywa maji ya baridi.

Aidha, hukatazwa pia kuosha vyombo na nguo.

Kwa Tanzania, tamaduni za jamii nyingi hukataza wasichana kuchuma mboga wala pilipili, baadhi hukatazwa kubeba mtoto mchanga kwa madai ya kumdhuru au hata kumsababishia homa na maambukizi pa wengine huambiwa kukaa mbali na Wanyama kwa kuwa wanaweza kushambuliwa nao. Hii ni mifano michache tu kati ya mingi.

View attachment 2331035
Kisayansi, madai haya siyo sahihi. Hedhi ni kitu kinachopaswa kuchukuliwa kama jambo la kawaida kwenye maisha ya binadamu na baadhi ya wanyama kwani ndiyo msingi wa muendelezo wa kuuleta uhai mpya duniani.
 
imani potofu, hedhi ni dalili ya uhai - hedhi ni baraka !! kumbuka lile ni yai ambalo limekosa rutubisho hivyo linajitoa kuweka mazingira saafi ili yai jingine lisongee ...
Mkeo au mpenzi wako akiwa kwa hedhi ndiyo wakati mzuri wa kumkubatia - mpe penzi loote mahaba ya kumwaga - ile ni suna.
 
Hedhi ni tendo la kiasili na kibaiolojia linalotokea kwa mwanamke baada ya kufikia umri wa kuvunja ungo. Tendo hili huwa na umuhimu mkubwa katika kupima uimara wa afya ya uzazi ya mwanamke.

Kwa mujibu wa UNICEF, asilimia 26 ya wanawake wote duniani wapo kwenye umri unaoruhusu tendo hili litokee maishani mwao.

Tamaduni za nchi nyingi duniani huchukulia hedhi kama jambo lisilofaa kutokana na uwepo wa nadharia nyingi zisizo na uthibitisho wa kisanyansi. Utafiti uliofanywa na UNICEF kwenye nchi za Afghanistan, Bangadesh, Ethiopia, Ghana na Indonesia unathibitisha ukubwa wa tatizo hili.Mfano nchini Afghanistani, wasichana hukatazwa kula nyama, mboga za majani pamoja na kunywa maji ya baridi.

Aidha, hukatazwa pia kuosha vyombo na nguo.

Kwa Tanzania, tamaduni za jamii nyingi hukataza wasichana kuchuma mboga wala pilipili, baadhi hukatazwa kubeba mtoto mchanga kwa madai ya kumdhuru au hata kumsababishia homa na maambukizi pa wengine huambiwa kukaa mbali na Wanyama kwa kuwa wanaweza kushambuliwa nao. Hii ni mifano michache tu kati ya mingi.

Semeni hivii sayansi haijapata ufumbuzi wa hiyo nadharia kwamba bado inaendlea kufanyiwa uchunguzi sio kukanusha kwamba sayansi inalikataa hlo jambo, labda miaka ijayo ltapata uthibitisho kupitia sayansi hyohyo utajuaje
 
Mwanamke akiwa kwenye hedhi anaesabika ni najisi Kwa mujibu wa biblia na Quran! Haya madai ya vitu kama mchachai, pilipili, majani ya maboga kukauka yakiguswa na mwanamke alliye kwenye hedhi ni ya kweli!
Mimi ni mwanaume.
Huu ni upuuzi wa kiwango cha hali ya juu kabisaa.
Kila siku kuwaonea tu mama na dada zetu.
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom