Mwanamke bora kuliko wote duniani ni Bikira Maria, ukitaka ndiyo hivyo, usipotaka ndiyo hivyo

MIXOLOGIST

JF-Expert Member
Mar 1, 2016
12,695
31,499



Lk 1:46-50 SUV​

Mariamu akasema, Moyo wangu wamwadhimisha Bwana, Na roho yangu imemfurahia Mungu, Mwokozi wangu; Kwa kuwa ameutazama Unyonge wa mjakazi wake. Kwa maana, tazama, tokea sasa Vizazi vyote wataniita mbarikiwa; Kwa kuwa Mwenye nguvu amenitendea makuu, Na jina lake ni takatifu. Na rehema zake hudumu vizazi hata vizazi Kwa hao wanaomcha.

Heri ya sikukuu ya wanawake duniani.
 
Mimi sijaharamisha kiumbe cha mungu.

Kumbukumbu la torati sijaandika mimi.

Labda kama mungu wenu anabadilikabadilika.

Kwenye kumbukumbu la torati anakataza kwenye agano jipya anaruhusu.

Mungu wa ajabu kabisa!
Sisi wakristu tulisha graduate huko, haramu ni kile kimtokacho mtu asema bwana wetu Yesu Kristu kasome injili ya Mathayo 15:11
 
Na mungu aliyesema msile nguruwe kwenye kumb la torati ni mungu wa kina nani?

Au mungu wa wapagani?
Mungu amesema mambo mengi kwa watu wengi na kwa wakati ufahao. Mungu ni mlezi, kila wakati ameleta neno lifaalo kwa makusudi maalumu. Ila ujumbe wa Yesu ni ujumbe wa uokovu, ni namna gani uishi ili uurithi ufalme wa Mungu
 
Mungu amesema mambo mengi kwa watu wengi na kwa wakati ufahao. Mungu ni mlezi, kila wakati ameleta neno lifaalo kwa makusudi maalumu. Ila ujumbe wa Yesu ni ujumbe wa uokovu, ni namna gani uishi ili uurithi ufalme wa
Maneno mengi ujajibu swali!

Mungu aliyeruhusu mle nguruwe kwenye agano jipya na Mungu aliyekataza msile nguruwe kwenye agano la kale ni Mungu mmoja au mungu wawili tofauti?

Mungu wenu ana sifa ya kubadilikabadilika?
 
Maneno mengi ujajibu swali!

Mungu aliyeruhusu mle nguruwe kwenye agano jipya na Mungu aliyekataza msile nguruwe kwenye agano la kale ni Mungu mmoja au mungu wawili tofauti?

Mungu wenu ana sifa ya kubadilikabadilika?
Mungu yuko flexible mkuu na hiyo ndiyo sifa yake kuu, he ls the wisdom. Kila neno lake lilitoka kwa sababu maalum.Kama vile alivyo mpa Adam mke mmoja na nyinyi akawaambie muoe wanne. Hali kadhalika sisi akatuambia haramu si kiingiacho bali kitokacho yaani kwa sasa yeye ha-focus kwenye vitu physical bali spiritual.

Alitoa amri zake kumi na hizo ndizo tunapaswa kuzingatia, ata ukila nyoka au nnge au kunguru, it doesnt matter, je matendo yako kwa jirani yako ni yapi?'

 
Mimi sijaharamisha kiumbe cha mungu.

Kumbukumbu la torati sijaandika mimi.

Labda kama mungu wenu anabadilikabadilika.

Kwenye kumbukumbu la torati anakataza kwenye agano jipya anaruhusu.

Mungu wa ajabu kabisa!
ni kifungu gani kwenye agano jipya ambacho kinaruhusu ulaji wa hiko unachosema? sidhani kama umeisoma Biblia kweli, anyways, kitaje nami nikione vinginevyo itakuwa umeropoka tu
 
View attachment 2541216


Lk 1:46-50 SUV​

Mariamu akasema, Moyo wangu wamwadhimisha Bwana, Na roho yangu imemfurahia Mungu, Mwokozi wangu; Kwa kuwa ameutazama Unyonge wa mjakazi wake. Kwa maana, tazama, tokea sasa Vizazi vyote wataniita mbarikiwa; Kwa kuwa Mwenye nguvu amenitendea makuu, Na jina lake ni takatifu. Na rehema zake hudumu vizazi hata vizazi Kwa hao wanaomcha.

Heri ya sikukuu ya wanawake duniani.
Ubora wake ni upi mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom